< Ezekiel 34 >

1 I dođe mi riječ Jahvina:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 “Sine čovječji, prorokuj protiv Izraelovih pastira, prorokuj im i reci: 'Ovako govori Jahve Gospod: Jao pastirima Izraelovim koji napasaju sami sebe! Ne moraju li pastiri napasati stado?
“Mwanadamu, tabiri juu ya wachungaji wa Israeli, tabiri na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wa wachungaji wa Israeli ambao hujitunza wenyewe tu! Je, haiwapasi wachungaji kutunza kundi la kondoo?
3 Mlijekom se hranite, vunom odijevate, ovnove tovne koljete, a stada ne pasete.
Mnakula mafuta ya wanyama, mnavaa mavazi ya sufu na kuchinja kondoo walionona, lakini hamlitunzi kundi.
4 Nemoćnih ne krijepite, bolesnih ne liječite, ranjenih ne povijate, zalutalih natrag ne dovodite, izgubljenih ne tražite, nego nasilno i okrutno njima gospodarite.
Hamkuwatia nguvu walio dhaifu wala hamkuwaganga wenye maradhi wala kuwafunga waliojeruhiwa. Hamkuwarudisha waliotangatanga wala kuwatafuta wale waliopotea. Badala yake mmewatawala kwa ukali na kwa ukatili.
5 I tako se ovce raspršiše nemajuć' pastira, i raspršene postadoše plijen zvijerima.
Hivyo walitawanyika kwa sababu hapakuwepo mchungaji, nao walipotawanyika, wakawa chakula cha wanyama wa mwitu wote.
6 Ovce lutaju po svim gorama i visokim bregovima; po svoj su zemlji raspršene ovce moje i nitko za njih ne pita, nikoga nema da ih traži.'
Kondoo wangu walitawanyika, wakatangatanga kwenye milima yote na kwenye kila kilima kirefu. Kondoo wangu walitawanyika juu ya uso wa dunia yote bila kuwa na yeyote wa kuwaulizia wala wa kuwatafuta.
7 Zato, pastiri, čujte riječ Jahvinu:
“‘Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana:
8 'Tako mi života, riječ je Jahve Gospoda: zato što ovce moje postadoše plijen i hrana zvijerima, nemajuć' pastira, dok pastiri moji ovaca mojih ne traže nego sami sebe pasu, a ne pasu stada mojega -
Kwa hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa sababu kondoo zangu wamekosa mchungaji na hivyo wametekwa nyara na kuwa chakula cha wanyama wote wa mwituni na kwa sababu wachungaji wangu, hawakuwatafuta kondoo zangu, bali wachungaji wamejitunza wenyewe, nao hawakuwalisha kondoo zangu,
9 zato, pastiri, čujte riječ Jahvinu:
kwa hiyo enyi wachungaji, sikieni neno la Bwana:
10 Ovako govori Jahve Gospod: 'Evo me na pastire! Ovce svoje tražit ću iz ruku njihovih i neću im dati da mi više stado pasu ni da sami sebe pasu: istrgnut ću ovce iz usta njihovih, neće im više biti hrana.'
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na wachungaji nami nitawadai kondoo zangu mikononi mwao. Nitawafukuza kutoka kwenye kuchunga kundi langu, ili wachungaji wasiendelee kujitunza wenyewe. Nitaokoa kondoo zangu kutoka kwenye vinywa vyao, nao kondoo hawatakuwa tena chakula chao.
11 Jer ovako govori Jahve Gospod: 'Evo me, sam ću potražiti ovce svoje i sam ću ih pasti!
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitawaulizia kondoo wangu na kuwatafuta.
12 Kao što se pastir brine za ovce svoje kad se nađe uza stado raspršeno, i ja ću se pobrinuti za svoje ovce i skupit' ih iz svih mjesta u koje se raspršiše u dan oblaka i mraka.
Kama vile mchungaji atafutavyo kundi lake lililotawanyika wakati akiwa pamoja nalo, hivyo ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawaokoa kutoka mahali pote walipokuwa wametawanyikia katika siku ya mawingu na giza nene.
13 Izvest ću ih iz naroda, skupit ću ih iz zemalja i dovesti ih u zemlju njihovu da ih pasem na gorama izraelskim, po svim dolinama i travnjacima.
Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mbalimbali, nami nitawaleta katika nchi yao wenyewe. Nitawalisha kwenye milima ya Israeli, katika mabonde na mahali pote panapokalika katika nchi.
14 Past ću ih na izvrsnim pašama, ovčinjaci će im biti na visokim gorama izraelskim; ondje će počivati u dobrim ovčinjacima i past će na sočnim pašama, po gorama izraelskim.
Nitawachunga kwenye malisho mazuri na miinuko ya mlima wa Israeli patakuwa mahali pao pa malisho. Huko watajipumzisha kwa amani katika nchi ya malisho mazuri, nao watajilisha huko katika malisho tele katika milima ya Israeli.
15 Sam ću pasti ovce svoje i sam ću im dati počinka - riječ je Jahve Gospoda.
Mimi mwenyewe nitawachunga kondoo zangu na kuwafanya wapumzike, asema Bwana Mwenyezi.
16 Potražit ću izgubljenu, dovesti natrag zalutalu, povit ću ranjenu i okrijepiti nemoćnu, bdjeti nad pretilom i jakom - past ću ih pravedno.'
Nitawaulizia kondoo waliopotea na kuwaleta waliotangatanga. Nitawafunga waliojeruhiwa na kuwatia nguvu walio dhaifu lakini wale waliojikinai na wenye nguvu nitawaangamiza. Nitalichunga kundi kwa haki.
17 A vama, ovce moje, ovako govori Jahve Gospod: 'Evo me da sudim između ovce i ovce, između ovnova i jaraca!
“‘Kwa habari yenu, enyi kundi langu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo, kati ya kondoo dume na mbuzi.
18 Zar vam je malo pasti na dobroj paši te ostatak paše nogama gazite? Malo vam je piti bistru vodu te ostatak nogama mutite?
Je, haiwatoshi ninyi kujilisha kwenye malisho mazuri? Je, ni lazima ninyi kuyakanyaga pia malisho yenu yaliyobaki kwa miguu yenu? Je, haiwatoshi ninyi kunywa maji safi? Je, ni lazima kuyachafua maji mengine kwa miguu yenu?
19 A moje ovce moraju pasti što vi nogama izgaziste, piti što vi nogama zamutiste.'
Je, ni lazima kundi langu wajilishe kwa yale mliyoyakanyaga na kunywa maji mliyoyachafua kwa miguu yenu?
20 Stoga ovako govori Jahve Gospod: 'Evo me da sudim između ovce pretile i mršave!
“‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi awaambialo: Tazama, mimi mwenyewe nitahukumu kati ya kondoo wanono na waliokonda.
21 Jer bokovima i plećima, bodući rogovima, slabe ovce guraste dok ih ne izguraste.
Kwa sababu mmewapiga kikumbo na kuwapiga kwa pembe zenu kondoo wote walio dhaifu mpaka wakawafukuza,
22 Ja ću izbaviti ovce svoje da više ne budu plijenom i sudit ću između ovce i ovce.
nitaliokoa kundi langu na hawatatekwa nyara tena. Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo.
23 Postavit ću im jednoga pastira koji će ih pasti, slugu svoga Davida: on će ih sam pasti i bit će im pastir,
Nitaweka juu yao mchungaji mmoja, mtumishi wangu Daudi, naye atawachunga, atawachunga na kuwa mchungaji wao.
24 a ja, Jahve, bit ću njihov Bog, i moj sluga David bit će im knez. Ja, Jahve, rekoh!
Mimi Bwana nitakuwa Mungu wao, naye mtumishi wangu Daudi atakuwa mkuu miongoni mwao. Mimi Bwana nimenena.
25 I sklopit ću s njima Savez mira i uklonit ću iz zemlje sve divlje zvijeri, i živjet će mirno u pustinji i spavati po šumama.
“‘Nitafanya nao Agano la amani na kuwaondoa wanyama wa mwitu kutoka nchi yao ili kondoo wangu waweze kupumzika nyikani na msituni kwa salama.
26 Njih i sve oko brda svojega učinit ću blagoslovom i dat ću im na vrijeme kišu, i bit će to kiša blagoslova.
Nitawabariki wao pamoja na maeneo yanayozunguka kilima changu. Nitawanyeshea mvua kwa majira yake, kutakuwepo mvua za baraka.
27 I drveće će poljsko donositi plodove, a zemlja će dati rod svoj. I oni će mirno živjeti u svojoj zemlji i znat će da sam ja Jahve kad slomim palice jarma njihova i kad ih izbavim iz ruku onih što ih podjarmiše.
Miti ya shambani itatoa matunda yake na ardhi itatoa mazao yake, watu watakaa salama katika nchi yao. Watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya nira zao na kuwaokoa kutoka mikono ya wale waliowafanya watumwa.
28 I neće više biti plijenom narodima, i zvijeri ih više neće žderati, nego će mirno živjeti i nitko ih neće plašiti.
Hawatatekwa tena nyara na mataifa, wala wanyama pori hawatawala tena. Wataishi kwa salama, wala hakuna yeyote atakayewatia hofu.
29 I učinit ću da im probuja slavni nasad, i glad ih više neće zatirati, u zemlji više neće podnositi rug narodÄa.
Nitawapa nchi yenye sifa kutokana na mazao yake, hawatapatwa na njaa katika nchi tena wala hawatadharauliwa na mataifa.
30 I znat će da sam ja, Jahve, Bog njihov, s njima i da su oni, dom Izraelov, narod moj - riječ je Jahve Gospoda.
Ndipo watakapojua kuwa Mimi, Bwana, Mungu wao, niko pamoja nao, na kwamba wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana Mwenyezi.
31 Vi, ovce moje, vi ste stado paše moje, a ja sam Bog vaš' - riječ je Jahve Gospoda.”
Ninyi ni kondoo wangu, kondoo wa malisho yangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu, asema Bwana Mwenyezi.’”

< Ezekiel 34 >