< Izlazak 7 >

1 Mojsiju je Jahve odgovorio: “Vidi! Faraonu ću te nametnuti kao božanstvo; tvoj brat Aron bit će tvoj prorok.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
2 Ti kazuj sve što ti naređujem, a tvoj brat Aron neka faraonu ponovi da pusti Izraelce te odu iz njegove zemlje.
Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
3 Ja ću učiniti da otvrdne srce faraonu i umnožit ću znakove i čudesa u zemlji egipatskoj.
Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
4 Kako vas faraon neće poslušati, ja ću staviti svoju ruku na Egipat: strašno kažnjavajući, izbavit ću svoje čete, narod svoj, Izraelce, iz egipatske zemlje.
hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
5 Kad pružim svoju ruku na Egipat i izvedem Izraelce iz njihove sredine, tada će Egipćani spoznati da sam ja Jahve.”
Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
6 Mojsije i Aron poslušaše: kako im je Jahve naredio, upravo tako učiniše.
Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
7 Mojsiju je bilo osamdeset, a Aronu osamdeset i tri godine kad su faraonu postavili svoje zahtjeve.
Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
8 Još doda Jahve Mojsiju i Aronu:
Bwana akamwambia Mose na Aroni,
9 “Kad faraon zatraži od vas da izvedete kakvo znamenje, ti reci Aronu da uzme svoj štap i baci ga pred faraona, a štap će se pretvoriti u zmiju.”
“Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
10 Dođu Mojsije i Aron pred faraona i učine kako im je Jahve naredio. Aron baci pred faraona i njegove službenike svoj štap, koji se pretvori u zmiju.
Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
11 Zovne faraon mudrace i vračare. I zaista, egipatski vračari svojim vračanjem učine isto:
Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
12 svaki baci svoj štap, koji se pretvori u zmiju. Ali Aronov štap proguta njihove štapove.
Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
13 Faraon bijaše tvrdokorna srca: ne htjede poslušati Mojsija i Arona, kako je Jahve i kazao.
Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
14 Tada Jahve reče Mojsiju: “Faraonovo je srce okorjelo; odbija da pusti narod.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
15 Ujutro pođi k faraonu. Kad izađe k vodi, stani preda nj na obali Rijeke. Uzmi u ruku štap što se bio u zmiju pretvorio.
Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
16 Reci mu: 'Jahve, Bog Hebreja, poslao me k tebi s porukom da pustiš moj narod da mi iskaže štovanje u pustinji. Ali sve dosad ti nisi poslušao.
Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
17 Ovako Jahve poručuje: Ovim ćeš spoznati da sam ja Jahve. Gledaj! Štapom koji imam u ruci mlatnut ću po vodi u Rijeci i pretvorit će se u krv.
Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
18 Ribe će u Rijeci pocrkati; Rijeka će se usmrdjeti, i grstit će se Egipćanima piti vodu iz Rijeke.'”
Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
19 Još Jahve reče Mojsiju: “Reci Aronu da uzme svoj štap i pruži svoju ruku povrh egipatskih voda: njihovih rijeka, njihovih prokopa, njihovih jezeraca, svih njihovih vodenih stjecišta, da se pretvore u krv; po svoj zemlji egipatskoj neka je krv, čak i u drvenim i kamenim posudama.”
Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
20 Mojsije i Aron učiniše kako im je Jahve naredio. Podiže Aron svoj štap i naočigled faraona i njegovih službenika mlatnu po vodi u Rijeci. Sva se voda u Rijeci prometnu u krv.
Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
21 Ribe u Rijeci pocrkaše; Rijeka se usmrdje, tako da Egipćani nisu mogli piti vodu iz Rijeke; krv bijaše po svoj zemlji egipatskoj.
Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
22 Ali egipatski vračari svojim vračanjem učiniše isto. Tako faraon ostade tvrdokorna srca: nije htio poslušati Mojsija i Arona, kako je Jahve i kazao.
Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
23 Faraon se okrenu i ode u svoj dvor, ne uzimajući ni to k srcu.
Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
24 Svi su Egipćani počeli kopati oko Rijeke tražeći pitke vode jer nisu mogli piti vode iz Rijeke.
Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 Kad je prošlo sedam dana kako je Jahve udario po Rijeci,
Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.

< Izlazak 7 >