< Izlazak 5 >

1 Poslije toga odu Mojsije i Aron pa reknu faraonu: “Ovako veli Jahve, Bog Izraelov: 'Pusti narod moj da ode i u moju čast slavi svetkovinu.'”
Baada ya mambo haya kutokea, Musa na Aruni walienda kwa Farao na kumwambia, ““Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli anasema: 'Waache watu wangu waende, ili wapate kunifanyia karamu jangwani.'”
2 “Tko je taj Jahve da ga ja poslušam”, odvrati faraon, “i pustim Izraelce? Ja toga Jahvu ne znam niti ću pustiti Izraelce.”
Farao akasema, “Yahwe ni nani? Kwa nini mimi nisikiliz sauti yake na kuwaacha Israeli waende? Mimi simjui Yahwe; na la zaidi, sitawaacha Israeli waende.”
3 “Bog Hebreja objavio nam se”, rekoše. “Zato nas pusti da odemo tri dana hoda u pustinju i prinesemo žrtvu Jahvi, Bogu svome, da se na nas ne obori pomorom ili mačem.”
Wakasema, “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tuache twende safari jangwani kwa siku tatu ili tutoe sadaka kwa Yahwe Mungu wetu ili asituadhibu kwa mapigo au kwa upanga.”
4 Nato im odvrati egipatski kralj: “Mojsije i Arone, zašto odvraćate svijet od njegovih dužnosti? Idite na svoj posao.
Lakini mfalme wa Misri aliwaambia, “Musa na Aruni, kwa nini mnawatoa watu kazini mwao? Nendeni kazini kwenu.”
5 Sad kad se svjetina tako umnožila”, nastavi faraon, “vi biste ih od posla odvratili?”
Pia alisema, “Sasa kuna Waebrania wengi nchini mwetu, na ninyi mnawafanya waache kazi zao.”
6 Istoga dana izda faraon naredbu nadglednicima i bilježnicima:
Siku ile ile, Farao alitoa amri kwa wasimamizi na wanyapara wa wale watu. Akasema,
7 “Ne pribavljajte više ovome narodu slame kao do sada. Neka idu sami i sebi je skupljaju.
“Tofauti na ilivyokuwa mwanzo, “Tofauti ni ilivyokuwa awali, msiwapatie tena watu majani ya kutengenezea tofali. Waacheni wao waende kujitafutia majani wenyewe.
8 A zahtijevajte od njih istu količinu opeke koju su pravili i dosad. Ne smanjujte je! Lijenčine su. Zato viču: 'Hajdemo prinijeti žrtvu Bogu svome!'
Ingawa wanapaswa kuleta hesabu sawa ya matofali watakayotengeneza kama ilivyokuwa awali. Msipokee pungufu, kwasababu wao ni wavivu. Ndiyo maana wanapiga kelele na kusema, 'turuhusu tuende tukamtolee sadaka Mungu wetu.'
9 Navalite poslove na taj svijet: neka rade, da ne obraćaju pažnje klevetama!”
Waongezeeni kazi wanaume ili wasipate tena muda wa kusikiliza maneno ya upotoshaji.”
10 Sad dođu nadglednici naroda i njegovi bilježnici te svijetu objave: “Ovako poručuje faraon: 'Neću vam više nabavljati slame.
Kwa hiyo viongozi wa watu na waangalizi wao waliwajulisha watu. Walisema, “Hivi ndivyo farao amesema: 'Sitawapeni tena malighafi.
11 Vi sami morate ići i tražiti je gdje god je možete naći. Ali zato neću smanjiti vaš posao.'”
Nyinyi wenyewe mtaenda kutafuta majani popote mtakapopata, lakini kazi zenu hazitapunguzwa.
12 Stoga se narod raziđe po svoj zemlji egipatskoj da skuplja strnjiku namjesto slame.
Basi watu hao wakatawanyika katika nchi yote ya Misri ili wapate kukusanya matakataka badala ya majani.
13 A nadglednici ih gonili: “Morate svakoga dana svršiti jednako posla kao i onda dok ste slamu dobivali.”
Wasimamizi wao wakawahimiza na kusema, “Malizeni kazi zenu, sawa na wakati ule majani yalipokuwapo.”
14 A bilježnike koje faraonovi nadglednici bijahu postavili nad Izraelcima tukli su i korili: “Zašto niste ni jučer ni danas napravili opeke koliko i prije?”
Wanyapara wa Farao wakawapiga wasimamizi wa Waisraeli, watu walewale ambao waliwaweka kuwa wasimamizi wa watumishi. Wale Wanyapara wakakazana kuwauliza, “Kwanini hamjatimiza idadi ya matofali inayotakiwa kwenu, siku ya jana na hata leo kama ambavyo mlifanya siku za nyuma?”
15 Onda bilježnici Izraelaca odu i potuže se faraonu: “Zašto ovako postupaš sa svojim slugama?
Basi Wanyapara wa wana wa Israeli wakamwendea Farao na kumlilia. Walisema, “Kwanini unawatendea watumishi wako hivi?
16 Tvoje sluge više ne dobivaju slame, a ipak se od nas traži: napravite opeku? Čak i tuku tvoje sluge, a kriv je tvoj narod!”
Sisi watumishi wako hatupewi majani tena, lakini bado wanatuambia sisi, “Tengenezeni tofali!' Sisi watumwa wako tunapigwa sasa, lakini kosa hilo ni la watu wako.”
17 “Lijenčine ste vi! Lijenčine!” - odgovori faraon. “Stoga i kažete: 'Hajdemo da prinesemo žrtvu Jahvi!'
Lakini Farao akasema, “Ninyi ni wavivu! Wavivu ninyi! Ninyi mwasema, 'Turuhusu twende kumtolea Yahwe sadaka.'
18 Nosite se na posao! Slama vam se neće davati, ali morate praviti određene količine opeke.”
Sasa rudini kazini. Hamtapewa majani tena, lakini mnapaswa kutengeneza idadi ile ile ya matofali.”
19 Bilježnici Izraelaca nađu se na muci zbog naredbe: “Svakodnevnu količinu opeke ne smijete smanjiti!”
Wanyapara wa wana wa Israeli wakagundua ya kuwa walikuwa kwenye shida kubwa mara walipoambiwa, “Hamtapunguza kamwe idadi ya matofali mnayotengeneza kila siku.”
20 Otišavši od faraona, naiđu na Mojsija i Arona, koji su ih čekali.
Wakakutana na Musa na Haruni, waliokuwa wamesimama nje ya Ikulu wakati wanatoka kwa Farao.
21 “Neka vas Jahve ima na oku i sudi vam!” - dobace im. “Omrazili ste nas kod faraona i njegovih dvorana; dali ste im mač u ruke da nas pobiju.”
Wakawaambia Musa na Haruni, “Yahwe awatazame ninyi na kuwaadhibu, kwa sababu mmetufanya sisi kuonekana wabaya mbele ya Farao na watumishi wake. Mmetia upanga mikononi mwao ili watuue.”
22 Mojsije se vrati Jahvi i reče: “Zašto, Gospodine, nanosiš štetu svome puku? Zašto si me poslao?
Musa akarudi kwa BWANA na kumwambia, “Bwana, kwanini umewatenda mabaya watu hawa? Kwanini kunituma mimi kwanza?
23 Otkad sam ja stupio pred faraona i progovorio mu u tvoje ime, on još gore postupa s ovim narodom. A ti ništa ne poduzimaš da izbaviš svoj narod.”
Tangu nilipokuja kwa Farao kusema naye kwa jina lako, amewatenda mabaya watu hawa, wala hujawaokoa watu wako hata kidogo.”

< Izlazak 5 >