< Estera 2 >

1 Poslije tih događaja, kako mu se utiša gnjev, kralj Ahasver sjeti se Vaštije, onoga što je ona učinila i što je bilo odlučeno protiv nje.
Baadaye, wakati hasira ya Mfalme Ahasuero ilikuwa imetulia, alimkumbuka Vashti na kile alichokuwa amekifanya na alilokuwa ameamuru juu yake.
2 Rekoše tada momci što služahu kralja: "Neka se potraže za kralja mlade djevojke, djevice lijepa izgleda.
Kisha watumishi waliomhudumia mfalme walipendekeza, “Na ufanyike utafiti kwa ajili ya wanawali mabikira wazuri wa sura kwa ajili ya mfalme.
3 Kralj neka odredi u svim pokrajinama svojega kraljevstva povjerenike da mu sakupe sve djevice pristala izgleda u tvrđavi grada Suze, u haremu, pod upravom Hegeja, kraljeva eunuha, čuvara žena. On će se pobrinuti za njihovu njegu.
Mfalme na ateue maafisa katika kila jimbo la himaya yake kuwaleta hao wanawali wote wazuri wa sura katika nyumba ya wanawake katika ngome ya mji wa Shushani. Kisha wawekwe chini ya utunzaji wa Hegai, towashi wa mfalme, msimamizi wa wanawake; na wapewe matunzo yote ya urembo.
4 Ona djevojka koja se najviše svidi očima kraljevim neka kraljuje umjesto Vaštije." Bijaše to po volji kralju, i on tako uradi.
Kisha yule ambaye atampendeza mfalme na awe malkia badala ya Vashti.” Shauri hili likampendeza mfalme, naye akalifuata.
5 U tvrđavi grada Suze bio je neki Židov koji se zvao Mordokaj, sin Jaira, sina Šimeja, sina Kišova, iz plemena Benjaminova.
Basi katika mji wa ngome ya Shushani palikuwa na Myahudi wa kabila ya Benyamini, jina lake Mordekai mwana wa Yairi, mwana wa Shimei, mwana wa Kishi,
6 On je bio protjeran iz Jeruzalema među prognanicima koje je babilonski kralj Nabukodonozor odveo zajedno s judejskim kraljem Jekonijom.
ambao walichukuliwa uhamishoni kutoka Yerusalemu na Mfalme Nebukadneza wa Babeli, wakiwa miongoni mwa waliochukuliwa mateka pamoja na Mfalme Yekonia wa Yuda.
7 On je odgajao Hadasu, to jest Esteru, kćerku strica svoga, jer ona ne imađaše ni oca ni majke. Djevojka je bila pristala i lijepa izgleda. Poslije smrti njezina oca i njezine majke Mordokaj je uze k sebi kao kćerku.
Mordekai alikuwa na binamu yake msichana aliyeitwa Hadasa, ambaye alimlea kwa kuwa hakuwa na baba wala mama. Msichana huyu, ambaye pia alijulikana kwa jina la Esta, alikuwa na umbo na sura ya kupendeza, naye Mordekai alimtunza kama binti yake mwenyewe baada ya baba yake na mama yake kufariki.
8 Kako se začu za kraljevu riječ i njegovu naredbu, mnogo se djevojaka sabra u tvrđavi grada Suze pod Hegejevim nadzorom. Tako dovedoše i Esteru u kraljevu palaču, pod nadzor Hegeja, čuvara žena.
Wakati agizo na amri ya mfalme lilitangazwa, wanawali wengi waliletwa kwenye ngome ya mji wa Shushani na kuwekwa chini ya uangalizi wa Hegai. Pia Esta alipelekwa katika jumba la mfalme na akakabidhiwa Hegai, aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake.
9 Djevojka se svidje njegovim očima, steče ona njegovu naklonost i on se pobrinu za njezino uljepšavanje i uzdržavanje. Uz to joj dade sedam najvrednijih ropkinja kraljevskog dvora i premjesti je, skupa s djevojkama, u najudobnije prostorije harema.
Msichana huyu alimpendeza na kupata kibali mbele zake. Mara moja akaanza kumpa matunzo ya uzuri na chakula maalum. Alimpa Esta vijakazi saba waliochaguliwa kutoka jumba la kifalme, na kumhamishia yeye pamoja na vijakazi wake katika sehemu bora zaidi katika nyumba ya wanawake.
10 Estera ne spomenu ni naroda ni obitelji kojoj je pripadala, jer joj Mordokaj bijaše zabranio da to učini.
Esta alikuwa hajadhihirisha uraia wala kabila lake, kwa sababu Mordekai alikuwa amemkataza.
11 Svakoga je dana Mordokaj šetao pred dvorištem harema da bi doznao kako se Estera osjeća i kako se prema njoj odnose.
Kila siku Mordekai alikuwa akitembeatembea karibu na ua wa nyumba ya wanawake kujua Esta alivyoendelea na kuona yaliyokuwa yakitendeka kwake.
12 Svaka je djevojka morala ući kralju kad je na nju, prema uredbi za žene, došao red, to jest nakon dvanaest mjeseci. Jer tada se završavalo razdoblje njihova uljepšavanja: šest mjeseci uljem iz mirne, a šest mjeseci balzamom i ostalim pomastima za žensku njegu.
Kabla zamu ya msichana haijafika ya kwenda kwa Mfalme Ahasuero, ilimbidi atimize miezi kumi na miwili ya matunzo ya urembo kama ilivyokuwa imepangwa. Kwa miezi sita walikuwa wajipake mafuta ya manemane, na miezi sita kujipaka manukato na vipodozi.
13 Pa kad bi djevojka ulazila kralju, bilo joj je dopušteno da sa sobom iz harema u kraljevsku palaču ponese sve što bi zatražila.
Basi hivi ndivyo ambavyo msichana angeingia kwa mfalme: Kila kitu alichohitaji aliruhusiwa kuchukua kutoka nyumba ya wanawake na kwenda navyo katika jumba la mfalme.
14 Ona bi ulazila uvečer, a ujutro bi se vraćala u drugi harem, pod nadzorom Šaašgaza, kraljeva eunuha, čuvara priležnica. Više se ne bi vraćala kralju, osim ako bi je posebno zaželio i dozvao je k sebi poimence.
Jioni angekwenda pale na asubuhi kurudi sehemu nyingine ya nyumba ya wanawake katika utunzaji wa Shaashgazi, towashi wa mfalme ambaye alikuwa mkuu wa masuria. Hangeweza kurudi kwa mfalme mpaka apendezwe naye na kuagiza aitwe kwa jina lake.
15 Kada dođe red na Esteru, kćerku Abihajla, koji je bio stric Mordokaja koji ju je bio pokćerio, da uđe kralju, ona ne zatraži ništa osim onoga što joj bijaše rekao Hegej, kraljev eunuh, čuvar žena. Ipak je pobuđivala udivljenje svih koji su je gledali.
Zamu ya Esta ilipofika kwenda kwa mfalme (msichana ambaye Mordekai alikuwa amemlea, binti wa Abihaili mjomba wake), Esta hakutaka vitu zaidi ya vile ambavyo Hegai, towashi wa mfalme aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake alivyokuwa amemshauri. Naye Esta alipata kibali kwa kila mtu aliyemwona.
16 Esteru, dakle, uvedoše kralju Ahasveru, u njegovu kraljevsku palaču, u desetom mjesecu, mjesecu Tebetu, sedme godine njegova vladanja.
Esta alipelekwa kwa Mfalme Ahasuero katika makao ya mfalme mwezi wa kumi, yaani mwezi wa Tebethi, katika mwaka wake wa saba wa kutawala.
17 Kralj zavolje Esteru više od svih drugih žena; više nego sve ostale djevice ona mu omilje i predobi ona njegovu naklonost. I položi on na njezinu glavu kraljevsku krunu, pa mjesto Vaštije ona posta kraljicom.
Basi ikawa mfalme alivutiwa na Esta kuliko wanawake wengine wote, naye akapata upendeleo na kibali kuliko mabikira wengine. Kisha akamvika taji la kifalme kichwani mwake na kumfanya malkia badala ya Vashti.
18 Nakon toga priredi kralj u čast Estere veliku gozbu za svoje knezove i službenike; svim pokrajinama odredi odmor i razda darove kraljevski darežljivo.
Mfalme akafanya karamu kubwa, karamu ya Esta, kwa wakuu wake wote na maafisa. Mfalme alitangaza mapumziko katika majimbo yake yote na kugawa zawadi kwa ukarimu wa kifalme.
19 Kad su drugi put djevojke bile sakupljene, Mordokaj sjeđaše na vratima kraljevim.
Wakati mabikira walikusanyika mara ya pili, Mordekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme.
20 Estera ne oda ni naroda ni obitelji iz koje je potjecala, kao što joj Mordokaj bijaše naredio. Estera se i dalje držala svih Mordokajevih uputa kao kad se nalazila pod njegovim skrbništvom.
Lakini Esta alikuwa ameficha siri ya kabila lake na uraia wake, kama Mordekai alivyokuwa amemwambia, kwa maana aliendelea kufuata maelekezo ya Mordekai kama alivyokuwa akifanya alipokuwa akimlea.
21 U ono vrijeme kad je Mordokaj sjedio na vratima kraljevim, Bigtan i Tereš, dva kraljeva dvoranina, čuvari praga, planuše gnjevom i počeše snovati da podignu ruku na kralja Ahasvera.
Wakati Mordekai alikuwa ameketi kwenye lango la mfalme, Bigthana na Tereshi, maafisa wawili wa mfalme waliokuwa walinzi wa lango, walikasirika na kupanga njama ya kumuua Mfalme Ahasuero.
22 Za tu njihovu namjeru sazna Mordokaj. On je dojavi kraljici Esteri, a Estera je u Mordokajevo ime saopći kralju.
Lakini Mordekai aligundua hila hii na kumwambia Malkia Esta, ambaye baadaye alimwarifu mfalme, huku akimsifu Mordekai.
23 Sve se izvidje i otkri se zavjera, pa obojica budu obješena o stup. To se pred kraljem zapisa u knjizi Ljetopisa.
Taarifa hiyo ilipochunguzwa na kuonekana kuwa kweli, maafisa hao wawili waliangikwa juu ya miti ya kunyongea. Haya yote yaliandikwa katika kitabu cha kumbukumbu mbele ya mfalme.

< Estera 2 >