< Ponovljeni zakon 1 >
1 Ovo su riječi što ih je Mojsije upravio svemu Izraelu s onu stranu Jordana - u pustinji, u Arabi nasuprot Sufu, između Parana i Tofela, Labana, Hazerota i Di Zahaba -
Haya ni maneno ambayo Musa aliyasema kwa Israeli wote ng'ambo ya jangwa la Yordani, katika tambarare ya mto wa Yordani juu ya Suph, katikati mwa Paran, Topheli, Laban, Hazeroth, na Di Zahab.
2 od Horeba do Kadeš Barnee, Seirskom gorom, jedanaest dana hoda.
Ni safari ya siku kumi na moja toka Horabu kupitia njia ya mlima wa Seir kwenda Kadeshi Barnea.
3 Bilo je to godine četrdesete, prvog dana mjeseca jedanaestoga, kad Mojsije reče Izraelcima sve što mu je Jahve za njih naređivao.
Ilitokea kwenye mwaka wa nne, mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, Musa alizungumza kwa watu wa Israeli, kuambia yote yale Yahwe aliyomwamuru kuhusu wao.
4 Pošto je porazio amorejskoga kralja Sihona, koji je živio u Hešbonu, i bašanskoga kralja Oga, koji je živio u Aštarotu i Edreju,
Hii ilikuwa baada ya Yahwe kumvamia Sihoni mfalme wa Amoria, ambaye aliishi huko Heshboni, na Ogi mfalme wa Bashani, ambaye aliishi huko Ashtarothi ya Edrei.
5 dakle s onu stranu Jordana, u zemlji moapskoj, poče Mojsije razlagati ovaj Zakon. Govoraše on:
Ng'ambo ya Yordani, katika nchi ya Moabu, Musa alianza kutangaza maelekezo haya, akisema,
6 “Jahve, Bog naš, reče nam na Horebu: 'Dosta ste boravili na ovome brdu.
“Yahwe Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, akisema, umeishi vya kutosha katika milima ya nchi hii.
7 Krenite na put! Idite u gorski kraj Amorejaca i svih njihovih susjeda, u Arabu, u Gorje, u Šefelu i u Negeb, na morsku obalu, u zemlju kanaansku i u Libanon, sve do Velike rijeke, rijeke Eufrata.
Geuka na uanze safari yako, na uende kwenye nchi ya milima ya Amorites, na kwenye maeneo yote karibu na tambarare ya mto Yordani, katika nchi ya milima, na nyanda za chini, huko Negev, na pwani - nchi ya Wakanani na huko Lebanoni mbali ya mto mkuu wa Euphratesi.
8 Eto, pred vas stavljam ovu zemlju. Idite, dakle, i zauzmite zemlju za koju se Jahve zakle ocima vašim, Abrahamu, Izaku i Jakovu, da će je dati njima i njihovu potomstvu poslije njih.'
Tazama, nimetenga nchi kwa ajili yako, nenda ndani na umiliki nchi ambayo Yahwe aliapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka na Yakobo, kuwapa na uzao wao baada yao.
9 Tada sam vam rekao: 'Ne mogu vas voditi sam.
Nilisema nawe kwa wakati huo, nikisema, siwezi nikakubeba peke yangu,
10 Jahve, Bog vaš, toliko vas je razmnožio da vas danas ima kao zvijezda na nebu.
Yahwe Mungu wako amekuzidisha, na tazama, leo umekuwa umati wa nyota angani.
11 Neka vas Jahve, Bog vaših otaca, umnoži još tisuću puta! Neka vas blagoslivlja kako vam je obećao!
Yahwe aweza, Mungu wa baba zako, kukufanya wewe mara elfu moja zaidi ya ulivyo, na kukubariki, kama alivyokuahidi!
12 Ali kako bih ja sam mogao nositi vaš teret, vaše breme i vaše sporove?
Lakini inawezekanaje mimi peke yangu kubeba shehena zako, mizigo yako, na migogoro yako?
13 Izaberite stoga iz svojih plemena ljude pametne, iskusne i ugledne da vam ih postavim za poglavare.'
Chukua wanaume wa hekima, wanaume waelewa, na wanaume walio na sifa nzuri toka kila kabila, nitawafaya kuwa vichwa juu yenu.
14 Vi ste mi odgovorili: 'Dobro je što predlažeš.'
Mlinijibu na kusema, 'Jambo ulilolisema ni zuri kwetu kufanya.'
15 Zato sam uzeo prvake iz vaših plemena, ljude pametne i ugledne, te ih postavio za poglavare: tisućnike, stotnike, pedesetnike, desetnike i vaše plemenske nadglednike.
Kwa hiyo nilichukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wa hekima, na wanaume wenye sifa nzuri, na nikawafanya kuwa vichwa juu yenu, jemedari kwa elfu, jemedari kwa hamsini, jemedari kwa kumi, na maakida, kabila kwa kabila.
16 U to isto vrijeme naložio sam i vašim sucima: 'Saslušajte svoju braću; sudite pravedno između čovjeka i njegova brata ili pridošlice.
Niliwaamuru waamuzi wenu kwa wakati huo, kusema, 'Zikiliza mabishano kati ya ndugu zenu, na muhukumu ya haki kati ya ndugu na ndugu zake, na mgeni aliye pamoja naye.
17 U suđenju nemojte biti pristrani; saslušavajte maloga kao i velikoga. Ne bojte se nikoga! TÓa sud je Božji! Ako vam koji slučaj bude pretežak, iznesite ga meni, da ga ja razvidim.'
Hamtaonesha upendeleo kwa yeyote katika mgogoro, mtasikia madogo na makubwa pia. Hamtaogopa uso wa mtu, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Migogoro iliyo migumu kwenu, mtaniletea mimi, na mimi nitaisikiliza.
18 Tako sam vam onda naložio sve što vam je činiti.
Niliwaamuru kwa wakati huo mambo yote mtakayofanya.
19 Krenusmo iz Horeba i, na putu u gorske krajeve Amorejaca, kako nam je naredio Jahve, Bog naš, prijeđosmo svu onu veliku i strašnu pustinju koju ste vidjeli. Stigosmo u Kadeš Barneu.
Tulisafiri toka Horebu na kwenda kupitia jangwa lile kubwa lote na lenye kutisha lile mliloliona, katika njia yetu kuelekea nchi ya milima huko Amorites, kama Yahwe Mungu wetu alivyotuamuru sisi, na tukaja Kadeshi ya Barnea.
20 Tada vam rekoh: 'Došli ste u gorski kraj Amorejaca, koji nam Jahve, Bog naš, daje.
Niliwambia, mmekuja kwenye nchi ya milima ya Amorites, ambayo Yahwe Mungu wetu anatupa sisi.
21 Eto, Jahve, Bog tvoj, stavio je preda te tu zemlju. Ustaj! Zaposjedni je, kako ti je rekao Jahve, Bog otaca tvojih. Ne boj se! Ne strahuj!'
Tazama, Yahwe Mungu wenu amekwisha weka nchi mbele yenu; nenda juu, muimiliki, kama Yahwe, Mungu wa baba zenu, amekwisha zungumza nanyi, msiogope wala kukata tamaa.
22 Svi ste onda došli k meni i rekli: 'Pošaljimo pred sobom ljude da izvide zemlju i jave nam o putu kojim ćemo ići i o gradovima u koje ćemo doći.'
Kila moja wenu alikuja kwangu na kusema, 'Basi tutume watu mbele yetu, ili kwamba waweze kupepeleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea sisi neno kuhusiana na njia ya wapi tuvamie, na kuhusiana na miji tutakayoingia.
23 Svidje mi se što rekoste. Zato uzeh dvanaest ljudi između vas, po jednoga iz svakog plemena.
Shauri hilo lilinibariki mimi, 'Nilichukua watu kumi na mbili kutoka kwenu, mtu moja kwa kila kabila.
24 Krenuli su na pogorje, stigli do Eškolske doline te izvidjeli kraj.
Waligeuka na kwenda juu ya nchi ya milima, kufika kwenye bonde la Eshcol na kufanya upepelezi wa kina.
25 I nabraše plodova one zemlje, donesoše ih k nama i javiše: 'Zemlja koju nam daje Jahve, Bog naš, dobra je.'
Walichukua baadhi ya mazao ya ardhi mikononi mwao na kuleta kwetu, Pia walileta neno na kusema, 'Ni nchi nzuri ambayo Yahweh Mungu wetu anatupa sisi'
26 Ali vi niste htjeli onamo; pobunili ste se protiv naredbe Jahve, Boga svoga.
Bado mlikataa kushambulia, lakini mliasi dhidi ya amri ya Yahwe Mungu wenu.
27 Rogoborili ste u svojim šatorima i govorili: 'U svojoj mržnji na nas Jahve nas je izveo iz zemlje egipatske da nas preda u ruke Amorejaca, kako bi nas posve uništili.
Mlilalamika katika mahema yenu na kusema, “Ni kwa sababu Yahwe alituchukia sisi kwa kuwa ametutoa katika nchi ya Misri, kuteweka katika mikono ya Amorites kutuangamiza.
28 Kamo da idemo? Naša su braća ubila u nama srčanost kad rekoše: Narod je i veći i jači nego mi; gradovi su veliki, i zidine im sežu do nebesa. A vidjeli smo ondje i Anakovce.'
Tuende wapi sasa? Ndugu zetu wamefanya mioyo yetu kuyeyuka, kusema, Hao watu ni wakubwa na warefu zaidi yetu, miji yao ni mikubwa na imeimarishwa kwenda mbinguni; zaidi ya yote, tumewaona wana wa Anakim huko”
29 'Ne bojte se!' - rekoh vam. - 'Ne plašite ih se!
Kisha nikasema nao, msitishwe wala msiwaogope.
30 Jahve, Bog vaš, koji ide pred vama, borit će se za vas kako je to učinio na vaše oči u Egiptu.'
Yahwe Mungu wenu, ambaye aenda mbele yenu, atawapigania, kama yote aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu,
31 A vidio si, uostalom, i u pustinji, gdje te Jahve, Bog tvoj, cijeloga puta što ste ga prevalili dok ste stigli do ovoga mjesta, nosio kao što čovjek nosi svoga sinčića.
na pia katika jangwa, ambapo mmekwisha muona Yahwe Mungu wenu jinsi alivyowabeba, kama mtu abebavyo mtoto wake, kokote mlikoenda mpaka kufika hapa.'
32 Ali, unatoč tome, vi niste imali pouzdanja u Jahvu, Boga svoga,
Bado licha ya neno hili hakumwamini Yahwe Mungu wenu,
33 u onoga koji je na putu išao pred vama da vam potraži mjesto za taborovanje - u ognju obnoć da vam osvijetli put kojim ćete ići, a obdan u oblaku.
aliyeenda mbele yenu kwenye njia kutafuta eneo kwa ajili yenu kuweka kambi, katika moto kwa usiku, katika mawingu kwa mchana.
34 Jahve ču graju vašu i zakle se u svojoj srdžbi:
Yahwe alisikia sauti ya maneno yenu na alikasirika; aliapa na kusema,
35 'Ni jedan jedini od ovih ljudi, od ovoga opakog naraštaja, neće vidjeti ove dobre zemlje za koju sam se zakleo da ću je dati vašim ocima.
Hakika hakuna mmoja ya hawa watu wa kizazi hiki kiovu wataona nchi nzuri ambayo niliapa kuwapa babu zao,
36 Izuzimam Kaleba, sina Jefuneova. On će je vidjeti; njemu i njegovim potomcima dat ću zemlju kojom je išao, jer je vjerno slijedio Jahvu.'
kasoro Kalebu mwana wa Jephuneeh; yeye ataiona. Yeye nitampa nchi ambayo amekwisha kuikanyanga, na watoto wake, kwa sababu alimfuata Yahwe kwa ukamilifu.'
37 Zbog vas se Jahve i na mene razljutio te mi rekao: 'Ni ti onamo nećeš ući.
Pia Yahweh alinikasirikia mimi kwa sababu yenu, kusema, 'Wewe pia hautaingia huko,
38 Ući će onamo Jošua, sin Nunov, koji te služi. Njega ti osokoli, jer će on uvesti Izraela u posjed.
Yoshua mwana wa Nuh, ambaye amesimama mbele yako, yeye ataingia, mtie moyo, kwani yeye atawaongoza Israeli kuimiliki.
39 A i vaši mališani, o kojima rekoste da će postati roblje, sinovi vaši koji još ne znaju razlikovati dobro i zlo, oni će u nju ući; njima ću je u posjed dati.
Zaidi ya yote, watoto wenu wadogo, ambao mlisema watakuwa waathirika, ambao leo hawana elimu ya uzuri au ubaya-wataenda ndani huko. Wao nitawapa nchi hiyo, na wataimiliki.
40 A vi se okrenite i zaputite u pustinju, prema Crvenome moru!'
Lakini ninyi, geuka na muuanza safari kwenda jangwani kwa kuambaa njia ya bahari ya mianzi'.
41 Vi ste mi tada odgovorili riječima: 'Sagriješili smo protiv Jahve. Poći ćemo gore i boriti se kako nam je Jahve, Bog naš, zapovjedio.' Svaki od vas dohvati svoje oružje i nepromišljeno pođe gore u brda.
Kisha mlinijibu na kusema kwangu, 'Tumetenda dhambi dhidi ya Yahwe, tutaenda juu na kupigana, tutafuata yote ambayo Yahwe Mungu wetu ametuamuru sisi kufanya'. Kila mtu miongoni mwenu aliweka silaha za vita, na mlikuwa tayari kuvamia nchi ya milima.
42 Onda mi Jahve reče: 'Kaži im: Ne idite gore i ne stupajte u borbu da vas ne poraze vaši neprijatelji jer ja nisam među vama.'
Yahwe alisema nami, 'Waambie, msivamie na kupigana, kwa kuwa sitakuwa pamoja nanyi, na mtashindwa na adui zenu'.
43 Tako sam vam i govorio, ali niste poslušali. Oprli ste se zapovijedi Jahvinoj i, puni drskosti, krenuli u brda.
Nilizungumza nanyi kwa njia hii, lakini hamkunisikiliza, Mliasi dhidi ya amri ya Yahwe, mlikuwa wenye kiburi na mlivamia nchi ya milima.
44 Ali Amorejci, koji žive u onome gorju, udariše na vas, pognaše vas, za vama se natisnuše kao pčele te su vas tukli od Seira do Horme.
Lakini Amorites, ambayo waliishi katika nchi hiyo ya milima, walitoka dhidi yenu na kuwafukuza kama nyuki, na kuwapiga chini huko Seir, mbali kama Hormah.
45 Vrativši se, plakali ste pred Jahvom, ali Jahve nije slušao vašega jauka niti je okrenuo svoga uha k vama.
Mlirudi na kulia mbele ya Yahwe; lakini Yahwe hakusikiliza sauti zenu, wala hakuwa makini kwenu.
46 U Kadešu vam valjade ostati dugo vremena, onoliko koliko ste već ostali.
Kwa hiyo mlibaki Kadeshi siku nyingi, siku zote mlibaki huko.