< Ponovljeni zakon 23 >

1 Neka se u Jahvinu zajednicu ne prima onaj komu je stučena mošnjica ili odrezano udo.
Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
2 Ni mješanac neka se ne prima u Jahvinu zajednicu; neka se njegovi ne primaju u zajednicu Jahvinu ni do desetog koljena.
Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
3 Neka ne ulazi u Jahvinu zajednicu ni Amonac ni Moabac; nitko od njihovih, čak ni u deseto koljeno, ne smije nikad u zajednicu Jahvinu.
Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
4 A sve zato što nisu izašli pred vas s kruhom i vodom kad bijaste na putu izišavši iz Egipta; i što su za novce najmili sina Beorova, Bileama iz Petora u Aram Naharajimu, da te prokune.
Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
5 Ali Jahve, Bog tvoj, ne htjede uslišati Bileama nego ti Jahve, Bog tvoj, prometnu prokletstvo u blagoslov jer te ljubi Jahve, Bog tvoj.
Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
6 Nikad ne promiči njihovo blagostanje i njihovo dobro u sve dane svoje dovijeka.
Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
7 Nemoj prezirati Edomca, jer je on brat tvoj. Ne preziri ni Egipćanina, jer si bio došljak u zemlji njegovoj.
Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
8 Njihovi potomci u trećem naraštaju mogu se primiti u Jahvinu zajednicu.
Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
9 Kad pođeš s taborom na svoje neprijatelje, čuvaj se od svakoga zla.
Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
10 Ako je među tvojima tko postao nečist zbog noćnog izljeva, neka iziđe iz tabora i neka se ne vraća u nj.
Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
11 A predvečer neka se u vodi opere te u smiraje može opet u tabor.
Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
12 Imaj izvan tabora mjesto gdje ćeš ići napolje.
Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
13 Sa svojom opremom nosi i lopaticu: njome ćeš, kad ideš napolje, iskopati rupu i poslije zatrpati svoju nečist.
Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
14 TÓa Jahve, Bog tvoj, ide posred tvoga tabora da te štiti i da ti predaje neprijatelje. Stoga i tvoj tabor treba da bude svet: neka Jahve ne zapazi u tebe ništa nedolično, da se ne bi odvratio od tebe.
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
15 Ne smiješ gospodaru izručivati roba koji je od svoga gospodara utekao k tebi.
Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
16 Neka boravi s tobom u tvojoj sredini, u mjestu što ga odabere u jednome od tvojih gradova gdje mu se svidi. Nemoj s njime loše postupati.
Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
17 Neka ne bude svetišne bludnice među izraelskim kćerima i neka ne bude svetišnog bludnika među izraelskim sinovima!
Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
18 Ne donosi u Dom Jahve, Boga svoga, ni za kakav zavjet bludničine plaće ni pasjeg novca, jer je oboje odvratno Jahvi, Bogu tvome.
Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
19 Ne traži kamata od svoga brata, niti kamata za novac, niti kamata na jestvine, niti kamata na bilo što gdje se obično traže.
Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
20 Od tuđinca možeš tražiti kamate, ali ih od svoga brata nemoj tražiti, da ti Jahve, Bog tvoj, udijeli blagoslov u svakom pothvatu tvoje ruke u zemlji u koju ideš da je zaposjedneš.
Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
21 Kad zavjetuješ kakav zavjet Jahvi, Bogu svome, ne oklijevaj da ga ispuniš. Zacijelo će ga Jahve, Bog tvoj, od tebe tražiti; i bio bi ti grijeh.
Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
22 Ako se ne zavjetuješ, neće ti biti grijeh.
Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
23 Ali ispuni ono što prijeđe preko tvojih usana, zavjet koji si svojim ustima slobodno učinio Jahvi, Bogu svome.
Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
24 Ako uđeš u vinograd svoga susjeda, slobodno ti je zobati grožđa do mile volje, ali u svoj sud ne smiješ stavljati.
Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
25 Ako uđeš u žito svoga susjeda, možeš kidati klasove rukom, ali ne smiješ prinositi srpa susjedovu žitu.
Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

< Ponovljeni zakon 23 >