< Ponovljeni zakon 2 >

1 Onda se okrenusmo i pođosmo u pustinju prema Crvenome moru, kako mi je Jahve naredio. Dugo smo se vrtjeli oko gore Seira.
Kisha tukageuka nyuma na kusafiri kuelekea jangwani kwa njia inayoelekea Bahari ya Shamu, kama Bwana alivyonielekeza. Kwa muda mrefu tulitembea kuzunguka vilima katika nchi ya Seiri.
2 I reče mi Jahve:
Kisha Bwana akaniambia,
3 'Dosta ste se vrtjeli oko ovoga brda. Okrenite prema sjeveru!'
“Umetembea kuzunguka hii nchi ya vilima kwa muda wa kutosha; sasa geukia kaskazini.
4 I narodu naloži ovako: 'Sad ćete proći preko područja svoje braće, potomaka Ezavovih, koji žive u Seiru. Oni se vas boje, ali vi dobro pripazite;
Wape watu maagizo haya: ‘Mko karibu kupita katikati ya nchi ya ndugu zako ambao ni wazao wa Esau, ambao wanaishi Seiri. Watawaogopa, lakini mwe waangalifu.
5 s njima ne zamećite boja jer vam neću dati ni stope njihove zemlje: goru Seir predao sam Ezavu u vlasništvo.
Msiwachokoze kwa vita kwa maana sitawapa ninyi sehemu yoyote ya nchi yao, hata sehemu ya kutosha kuweka wayo wenu juu yake. Nimempa Esau nchi ya vilima ya Seiri kama yake mwenyewe.
6 Hranu od njih kupujte za novac da imate što jesti; i vodu za piće kupujte od njih za novac.'
Mtawalipa fedha kwa chakula mtakachokula na maji mtakayokunywa.’”
7 Ta Jahve te, Bog tvoj, blagoslovio u svim djelima tvojih ruku; on je bdio nad tvojim putovanjem onom velikom pustinjom; ovih četrdeset godina Jahve, Bog tvoj, bijaše s tobom i ništa ti nije nedostajalo.
Bwana Mungu wenu amewabariki kwa kazi yote ya mikono yenu. Amewalinda katika safari yenu katikati ya jangwa hili kubwa. Kwa miaka hii arobaini Bwana Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi, na hamkupungukiwa na kitu chochote.
8 Tako smo svoju braću, potomke Ezavove što žive u Seiru, zaobišli putem što vodi u Arabu, Elat i Esjon Geber, a onda udarismo prema Moapskoj pustinji.
Basi tulipita kwa ndugu zetu wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri. Tuligeuka kutoka njia ya Araba ambayo inatokea Elathi na Esion-Geberi, tukasafiri kufuata njia ya jangwa la Moabu.
9 Tada mi zapovjedi Jahve: 'Nemoj uznemirivati Moapce niti s njima zameći boja, jer ništa od njihove zemlje neću dati u tvoje vlasništvo: Lotovim sinovima predao sam Ar u posjed.'
Kisha Bwana akaniambia, “Usiwasumbue Wamoabu kwa vita, kwa kuwa sitawapa sehemu yoyote ya nchi yao. Nimetoa nchi ya Ari kwa wazao wa Loti kama milki yao.”
10 Prije su ondje živjeli Emijci. Bio je to moćan narod i brojan; krupna stasa kao i Anakovci.
(Waemi walikuwa wakiishi huko hapo zamani, watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki.
11 Poput Anakovaca, i njih smatraju Refaimcima, ali ih Moapci nazivaju Emijcima.
Kama walivyokuwa Waanaki, hao pia walikuwa kama Warefai, lakini Wamoabu waliwaita Waemi.
12 Isto su tako u Seiru živjeli prije Horijci, ali su ih Ezavovi potomci izvlastili, istrijebili ih i naselili se na njihovo, kako je, uostalom, učinio Izrael sa zemljom - baštinom svojom - koju mu je Jahve predao.
Wahori waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau waliwafukuza. Waliwaangamiza Wahori na kukaa mahali pao, kama Waisraeli walivyofanya katika nchi ambayo Bwana aliwapa kama milki yao.)
13 'A sada ustanite i prijeđite preko potoka Zereda!' I prijeđosmo potok Zered.
Bwana akasema, “Sasa ondokeni mvuke Bonde la Zeredi.” Hivyo tukavuka bonde.
14 Vrijeme što smo išli od Kadeš Barnee pa dok smo prešli preko potoka Zereda iznosilo je trideset i osam godina - sve dok nije izumro iz tabora sav onaj naraštaj ljudi sposobnih za borbu, kako im se Jahve i zakleo.
Miaka thelathini na minane ilipita tangu wakati tulipoondoka Kadesh-Barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi. Kwa wakati huo kile kizazi chote cha wanaume kuanzia wale wawezao kwenda vitani kilikuwa kimekufa, kama Bwana alivyokuwa amewaapia.
15 I zbilja! Ruka Jahvina bila je protiv njih: istrebljivala ih je isred tabora dok ih nije nestalo.
Mkono wa Bwana uliwakabili hadi alipowaangamiza wote huko kambini.
16 I tako, kad je smrt istrijebila iz naroda sve ljude sposobne za borbu,
Ikawa baada ya mtu wa mwisho kuanzia wale wawezao kwenda vitani kufa,
17 reče mi Jahve:
Bwana akaniambia,
18 'Danas prelaziš moapsku zemlju Ar.
“Leo utapita katika nchi ya Moabu huko Ari.
19 A onda ćeš se približiti Amoncima. Nemoj ih uznemirivati niti s njima zameći boja. Ništa, naime, od zemlje Amonaca neću ustupiti tebi u vlasništvo jer sam je već predao u posjed Lotovim potomcima.'
Utakapokuja kwa Waamoni, msiwasumbue wala kuwachokoza kwa vita, kwa kuwa sitawapa ardhi yoyote iliyo ya Waamoni kuwa milki yenu. Nimeitoa kama milki ya wazao wa Loti.”
20 I nju smatraju refaimskom zemljom. U njoj su prije živjeli Refaimci, koje Amonci zovu Zamzumijcima.
(Hiyo pia ilidhaniwa kuwa nchi ya Warefai waliokuwa wakiishi huko, lakini Waamoni waliwaita Wazamzumi.
21 Bio je to narod moćan i brojan; krupna stasa kao i Anakovci. No Jahve ih uništi pred Amoncima - koji ih izvlastiše i naseliše se na njihovo,
Walikuwa watu wenye nguvu na wengi, warefu kama Waanaki. Bwana akawaangamiza kutoka mbele ya Waamoni, ambao waliwafukuza na kukaa mahali pao.
22 kako je, uostalom, učinio i potomcima Ezavovim, koji su nastanjeni u Seiru, kad je pred njima uništio Horijce, koje su oni otjerali s posjeda i do danas žive na njihovim mjestima.
Bwana alikuwa amefanya vivyo hivyo kwa wazao wa Esau, ambao waliishi Seiri, wakati alipowaangamiza Wahori watoke mbele yao. Waliwafukuza na wao wakaishi mahali pao mpaka leo.
23 I Avijce, koji su živjeli po zaseocima sve do Gaze, istrijebiše Kaftorci koji su došli iz Kaftora te se naseliše na njihovo mjesto.
Nao Waavi ambao waliishi katika vijiji mpaka Gaza, Wakaftori waliokuja kutoka Kaftori waliwaangamiza na kukaa mahali pao.)
24 'Ustajte! Na put krenite i prijeđite preko potoka Arnona. U ruke ti, eto, predajem Amorejca Sihona, kralja hešbonskoga, i njegovu zemlju. Počni s osvajanjem; izazovi ga na boj!
“Ondoka sasa na uvuke Bonde la Arnoni. Tazama, nimemweka mikononi mwako Sihoni Mwamori, mfalme wa Heshboni na nchi yake. Anza kuimiliki nchi hiyo na umwingize katika vita.
25 Od danas počinjem ugoniti strah i trepet pred tobom u narode koji su pod svim nebesima, tako da će strepiti i tresti se pred tobom kad god čuju glas o tebi.'
Siku hii ya leo nitaanza kuwatia hofu na woga mataifa yote chini ya mbingu wawaogope ninyi. Watakaposikia taarifa zenu, watatetemeka na kufadhaika kwa sababu yenu.”
26 Tada sam iz pustinje Kedmot uputio glasnike kralju hešbonskom Sihonu s miroljubivim riječima:
Kutoka jangwa la Kedemothi nilituma wajumbe wenye maneno ya amani kwa Sihoni mfalme wa Heshboni kusema,
27 'Pusti da prođem preko tvoje zemlje. Samo ću proći putem, ne skrećući ni desno ni lijevo.
“Turuhusu tupite katika nchi yako. Tutapita katika barabara kuu, hatutageuka kuume wala kushoto.
28 Hranu mi prodavaj za novac da mogu jesti; i vodu za piće davaj mi za novac. Pusti me samo da pješice prođem,
Tuuzie chakula tule na maji tunywe kwa thamani yake katika fedha. Turuhusu tu tupite kwa miguu,
29 da prijeđem preko Jordana u zemlju koju nam daje Jahve, Bog naš - kao što su mi dopustili potomci Ezavovi, nastanjeni u Seiru, i Moapci, što žive u Aru.'
kama wazao wa Esau ambao wanaishi Seiri na Wamoabu ambao wanaishi Ari walivyotufanyia, mpaka tuvuke Yordani kuingia nchi ambayo Bwana Mungu wetu anatupatia.”
30 Ali hešbonski kralj Sihon ne htjede nas pustiti preko svoga; jer Jahve, Bog tvoj, duh mu zaslijepi a srce otvrdnu, da ga preda u tvoje šake, gdje je i danas.
Lakini Sihoni mfalme wa Heshboni alikataa kuturuhusu kupita. Kwa kuwa Bwana Mungu wako alikuwa ameifanya roho yake kuwa ngumu na moyo wake kuwa mkaidi ili amweke kwenye mikono yenu, kama alivyofanya sasa.
31 Tada mi reče Jahve: 'Eto sam počeo da ti izručujem Sihona i njegovu zemlju. Počni osvajanje da mu zemljom zagospodariš.'
Bwana akaniambia, “Tazama, nimeanza kuwapa Mfalme Sihoni na nchi yake kwako. Sasa anzeni kuishinda na kuimiliki nchi yake.”
32 Kod Jahasa presrete nas Sihon.
Wakati Sihoni pamoja na jeshi lake lote walipokuja kukutana nasi katika vita huko Yahazi,
33 Navali on i sav njegov narod. Ali Jahve, Bog naš, predade nam ga, tako da potukosmo njega, njegove sinove i sav njegov narod.
Bwana Mungu wetu alimweka mikononi mwetu, nasi tukamwangamiza pamoja na wanawe na jeshi lake lote.
34 Tada osvojismo sve njegove gradove i prokletstvom udarismo sve gradove s ljudima, ženama i djecom, ništa ne štedeći,
Kwa wakati ule tuliteka miji yake yote na kuiangamiza kabisa: wanaume, wanawake na watoto. Hatukumwacha yeyote.
35 izuzev stoke, koju uzesmo kao plijen, skupa s plijenom iz gradova što smo ih osvojili.
Lakini mifugo na nyara tulizoziteka kutoka ile miji tulijichukulia wenyewe.
36 Od Aroera, koji se nalazi na obali potoka Arnona, i od grada koji je u njegovoj dolini pa do Gileada nije bilo grada koji bi nam odolio: sve nam ih je Jahve, Bog naš, predao.
Kutoka Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kutoka mji ulio ndani ya bonde, hata mpaka Gileadi, hapakuwa na mji hata mmoja uliokuwa na nguvu kutushinda. Bwana Mungu wetu alitupa yote.
37 Jedino se nisi primicao zemlji Amonaca, kraju uz potok Jabok, i gradovima u pogorju, kako je Jahve, Bog naš, odredio.
Lakini kulingana na amri ya Bwana Mungu wetu, hamkujiingiza katika nchi yoyote ya Waamoni, wala katika sehemu yoyote iliyo kandokando ya Mto Yaboki, wala katika miji iliyoko katika vilima.

< Ponovljeni zakon 2 >