< 2 Solunjanima 3 >
1 Uostalom, molite, braćo, za nas da riječ Gospodnja trči i proslavlja se kao i u vas
Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
2 i da se oslobodimo nezgodnih i opakih ljudi. Jer nemaju svi vjere!
Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
3 Ali, vjeran je Gospodin koji će nas učvrstiti i sačuvati od Zloga.
Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
4 A uzdamo se, u Gospodinu, u vas: da vršite i da ćete vršiti ono što vam zapovijedamo.
Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
5 A Gospodin neka upravi srca vaša k ljubavi Božjoj i postojanosti Kristovoj.
Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
6 Zapovijedamo vam, braćo, u ime Gospodina Isusa Krista da se klonite svakoga brata što živi neuredno i ne po predaji koju primiste od nas.
Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
7 Ta sami znate kako nas treba nasljedovati. Jer dok bijasmo među vama, nismo živjeli neuredno:
Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
8 ničiji kruh nismo badava jeli, nego smo u trudu i naporu noću i danju radili da ne bismo opteretili koga od vas.
wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
9 Ne što ne bismo imali prava, nego da vam sebe damo za uzor koji ćete nasljedovati.
Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
10 Doista, dok bijasmo u vas, ovo vam zapovijedasmo: Tko neće da radi, neka i ne jede!
Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
11 A čujemo da neki od vas žive neuredno: ništa ne rade, nego dangube.
Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
12 Takvima zapovijedamo i zaklinjemo ih u Gospodinu Isusu Kristu: neka s mirom rade i svoj kruh jedu.
Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
13 Vama pak, braćo, neka ne dodija činiti dobro.
Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
14 Ako li se tko ne pokorava našoj riječi u ovoj poslanici, zabilježite ga, ne drugujte s njime, da se postidi,
Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
15 ali ga ne smatrajte neprijateljem, nego ga urazumljujte kao brata.
Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16 A sam Gospodin mira dao vam mir zauvijek i na svaki način! Gospodin sa svima vama!
Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
17 Pozdrav mojom rukom, Pavlovom. Ovo je znak u svakoj poslanici: ovako pišem.
Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
18 Milost Gospodina našega Isusa Krista sa svima vama!
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.