< 2 Kraljevima 9 >

1 Prorok Elizej pozva jednoga od proročkih sinova i reče mu: “Opaši se, uzmi sa sobom ovu posudu s uljem pa idi u Ramot Gilead.
Nabii Elisha akamwita mmoja wa watoto wa manabii na kumwambia, “Vaa kwa kwa safari, halafu chukua hii chupa ndogo ya mafuta kwenye mikono yako na uende Romoth Geliadi.
2 Kad onamo stigneš, potraži Jehua, sina Jošafatova, sina Nimšijeva. Kad ga nađeš, izvedi ga između njegovih drugova i uvedi ga u pokrajnju sobu.
Wakati utakapofika, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi, na uende ukaingie na kumfanya ainuke kutoka miongoni mwa rafiki zake, na ukampeleke katika chumba cha ndani.
3 I uzmi posudu s uljem, izlij mu je na glavu i reci: 'Ovako veli Jahve: Pomazao sam te za kralja izraelskoga.' Zatim otvori vrata i bježi, ne oklijevaj.”
Kisha chukua ile chupa ya mafuta na imiminie kwenye kichwa chake na kusema, 'Yahwe anasema hivi: “Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. “Halafu fungua mlango, na kukimbia; usichelewe.”
4 Tada mladi prorok ode u Ramot Gilead.
Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Romoth Geliadi.
5 Kad je stigao, zapovjednici vojske upravo su sjedili na okupu. On reče: “Imam ti riječ reći, zapovjedniče!” Jehu upita: “Komu od nas?” On odgovori: “Tebi, zapovjedniče!”
Wakati alipofika, kumbe, wale manahodha wa lile jeshi walikuwa wamekaa. Hivyo yule nabii kijana akasema, “Nimekuja mara moja naneno kwako, nahodha.” Yehu akajibu, “kwa yupi katika sisi?” Yule nabii kijana akajibu, “Kwako nahodha.”
6 Jehu tada ustade i uđe u kuću. Mladi mu čovjek izli ulje na glavu i reče mu: “Ovako veli Jahve, Bog Izraelov: 'Pomazao sam te za kralja nad Jahvinim narodom, nad Izraelom.
Basi Yehu akainuka na kwenda kwenye nyumba, na yule nabii akammiminia mafuta kwenye kichwa chake na kumwambia Yehu, “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: 'Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Yahwe, juu ya Isaraeli.
7 Ti ćeš pobiti obitelj Ahaba, gospodara tvoga, a ja ću osvetiti krv svojih slugu proroka i krv sviju službenika Jahvinih na Izebeli
Wewe lazima uiue familia ya Ahabu bwana wako, ili niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe, ambao waliokuwa wameuawa kwa mkono wa Yezebeli.
8 i na svoj obitelji Ahabovoj. Iskorijenit ću Ahabu sve što mokri uza zid, robove i slobodnjake u Izraelu.
Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu, yeyote awe mtumwa au mtu huru.
9 Učinit ću s domom Ahabovim kao s domom Jeroboama, sina Nebatova, i kao s domom Baše, sina Ahijina.
Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama nyumba ya Yerobohamu mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
10 A Izebelu će proždrijeti psi na polju jizreelskom i nitko je neće pokopati.'” - Zatim otvori vrata i pobježe.
Mbwa watamla Yezebeli katika Yezreeli, na hakutakuwa na mtu wa kumzika.” Kisha nabii akafungua mlango na kukimbia.
11 Jehu iziđe k časnicima svoga gospodara. Oni ga upitaše: “Je li sve u miru? Zašto je ta budala dolazila k tebi?” On im odgovori: “Znate čovjeka i besjedu njegovu.”
Kisha Yehu akatoka kwenda kwa watumishi wa bwana wake, na mmoja akamwambia, “Je kila kitu kiko sawa? Kwa nini huyu mwenda wazimu amekuja kwako?” Yehu akawajibu, “Mnamjua huyo mtu na mambo asemayo.”
12 Oni rekoše: “Ne znamo! Kazuj nam!” On im reče: “Govorio mi je tako i tako i rekao mi: 'Ovako veli Jahve: Pomazao sam te za kralja nad Izraelom.'”
Wakasema, “Huo ni uongo. Tuambie.” Yehu akajibu, “Alisema hivi na vile juu yangu, na pia akasema, 'hivi ndivyo Yahwe asemavyo: Nimekumiminia mafuta kama mfalme juu ya Israeli.””
13 Odmah oni uzeše svoje ogrtače i prostriješe ih pred njim po stepenicama, zatrubiše u rogove i povikaše: “Jehu je kralj!”
Kisha kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu juu ya madaraja. Wakapiga baragumu na kusema, “Yehu ni mfalme.”
14 Tako Jehu, sin Jošafata, sina Nimšijeva, skova urotu protiv Jorama - Joram je tada branio Ramot Gilead sa svim Izraelcima protiv Hazaela, aramejskog kralja.
Katika njia hii Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akafanya njama juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiilinda Ramothi Gileadi, yeye na Israeli yote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu,
15 Ali se kralj Joram vratio u Jizreel da liječi rane koje su mu zadali Aramejci u boju s Hazaelom, aramejskim kraljem. - I reče Jehu: “Ako vam je po volji, neka nitko ne utekne iz grada da odnese vijest u Jizreel.”
lakini mfalme Yoramu alikuwa amesharudi kwa Yezreeli ili kuponywa yale majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami, wakati akiwa anapigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akawaambia watumishi wa Yoramu, “kama hili ndilo wazo lako, kisha usimwache mtu aondoke na kwenda nje ya mji, ili aende kupeleka habari hii Yezreeli.”
16 Jehu se tada pope na kola i ode prema Jizreelu, jer je Joram ondje bolovao, i Ahazja, kralj judejski, došao ga posjetiti.
Basi Yehu akaendesha gari la farasi mpaka Yezreeli; kwa kuwa Yoramu alikuwa amelala huko. Basi Ahazi mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka chini kuonana na Yoramu.
17 Stražar koji je stajao na kuli u Jizreelu, videći da dolazi Jehuova četa, javi: “Vidim nekakvu četu.” Joram naredi: “Uzmi konjanika i pošalji ga pred njih da upita: je li sve s mirom.”
Mlinzi alikuwa amesimama juu ya mnara katika Yezreeli, akaliona lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo; akasema, “Naona kundi la watu wanakuja.” Yoramu akasema, “Chukua mwendesha farasi, na umtume akakutane nao; mwambie aseme, “Je mnakuja kwa amani?””
18 Ode konjanik preda nj i reče: “Ovako veli kralj: je li sve s mirom?” - Jehu odgovori: “Što te briga je li s mirom! Hajde za mnom.” Stražar javi: “Glasnik je stigao do njih, ali se ne vraća.”
Hivyo mwendesha farasi akatoka kumlaki; akasema, “Mfalme asema hivi: Je mnakuja kwa amani?”' Basi Yehu akasema, “Wewe una nini na amani? Geuka na unifuate nyuma.” Kisha yule mlinzi akamwambia mfalme, Yule mjumbe ameshaonana nao, lakini anarudi.”
19 Kralj posla drugoga konjanika. Taj dođe k njima i upita: “Ovako veli kralj: je li sve s mirom?” - Jehu mu odgovori: “Što te briga je li s mirom! Hajde za mnom.”
Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao na kusema, “Mfalme asema hivi: 'Je mnakuja na amani?”' Yehu akajibu, “Wewe una nini na amani? Geuka na kunifuata nyuma.
20 Stražar opet javi: “Došao je do njih, ali se ne vraća. A vožnja je kao vožnja Jehua, sina Nimšijeva: vozi kao mahnit!”
Tena yule mlinzi akatoa taarifa, “Amekwisha kuonana nao, lakini hatorudi. Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo; anaendesha kwa kasi.”
21 Joram reče: “Preži!” I upregoše u njegova kola. Joram, kralj Izraela, i judejski kralj Ahazja iziđoše, svaki u svojim kolima, u susret Jehuu. Susretoše ga u polju Nabota Jizreelca.
Hivyo Yoramu akasema, “Andaa gari langu la farasi liwe tayari.” Wakaandaa gari lake la farasi, na Yoramu mfalme wa Israeli na Ahazi mfalme wa Yuda akaendesha, kila mmoja kwenye gari lake la farasi, kumlaki Yehu. Wakamkuta kwenye mali ya Nabothi Myezreeli.
22 Kad Joram ugleda Jehua, upita ga: “Je li sve u miru, Jehu?” Ovaj odgovori: “Kakvu miru dok traju bludništva tvoje majke Izebele i njena mnoga čaranja!”
Wakati Yoramu alipomuona Yehu, alisema, “Je unakuja katika hali ya amani, Yehu?” Akajibu, “Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?”
23 Joram okrenu i udari u bijeg govoreći Ahazji: “Izdaja, Ahazja!”
Basi Yoramu akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia na kumwambia Ahazia, “Kuna udanganyifu, Ahazia.
24 Jehu se lati luka, ustrijeli Jorama među pleća: strijela mu prođe posred srca te se on sruši u kola.
Ndipo Yehu akauvuta upinde wake kwa nguvu zake zote na kumpiga Yoramu kati ya mabega yake; mshale ukaenda kwenye moyo wake, akaanguka chini kwenye gari lake la farasi.
25 Jehu reče svome dvorjaniku Bidkaru: “Digni ga i baci na njivu Nabota Jizreelca. Sjeti se: kad smo ja i ti jahali za njegovim ocem Ahabom, kako Jahve izreče protiv njega:
Ndipo Yehu akamwambia Bidkari nahodha wake, “Mchukue na mtupie kwenye shamba la Nabothi Myezreeni. Fikiria kuhusu vile ambavyo wewe na mimi tulivyoendesha pamoja baada ya Ahabu baba yake, Yahwe aliuweka juu unabii dhidi yake:
26 'Kunem se: kako sinoć vidjeh krv Nabotovu i krv njegovih sinova,' riječ je Jahvina, 'tako ću ti vratiti isto na ovome polju,' riječ je Jahvina. Digni ga, dakle, i baci ga na to polje, prema riječi Jahvinoj.”
Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya watoto wake - asema Yahwe - na nitahakikisha unalipia hili shamba - asema Yahwe. Sasa basi, mchukue na mtupe kwenye hili shamba, sawa sawa na neno la Yahwe.”
27 Kada je to vidio judejski kralj Ahazja, pobježe prema Bet Haganu, ali ga je Jehu gonio i naredio: “Ubijte i njega!” Ranili su ga u kolima na brdu Guru, koje se nalazi kod Jibleama. Ali je umakao u Megido i ondje umrije.
Wakati Ahazi yule mfalme wa Yuda alipoliona hili, akakimbia kwa njia ya Bethi Hagani. Lakini Yehu akamfuata, na kusema, “Muulie humo kwenye gari la farasi,” na wakampiga mahali pa kupandia Guri, karibu na Ebleamu. Ahazi akakimbilia Megido na kufia pale.
28 Njegove su ga sluge u kolima prenijele u Jeruzalem i sahranile ga u grobnici kraj njegovih otaca, u Davidovu gradu.
Watumishi wake wakaubeba mwili wake kwa magari ya farasi kwenda Yerusalemu na kumzika kwenye kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
29 Jedanaeste godine kraljevanja Jorama, sina Ahabova, Ahazja postade kralj nad Judejom.
Basi ilikuwa mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu huyo Ahazia akaanza kutawala juu ya Yuda.
30 A Jehu bijaše ušao u Jizreel. Kad je to čula Izebela, namaza oči, uresi glavu i pogleda s prozora.
Wakati Yahu alipokuja kwa Yezebeli, Yezebeli akasikia juu ya hilo, akapaka wanja kwenye macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri, na kuchungulia kwenye dirisha.
31 I kad je Jehu ulazio na vrata, ona reče: “Kako je, Zimri, ubojico svoga gospodara?”
Kadiri Yehu alipokuwa akiingia kwenye lango, akamwambia, “Je unakuja kwa amani, wewe Zimri, muuaji wa bwana wako?”
32 Jehu okrenu lice prema prozoru i reče: “Tko je sa mnom, tko?” I dva-tri dvoranina pogledaše prema njemu.
Yehu akatazama juu ya dirisha na kusema, “Ni nani yuko upande wangu? Nani?” Matowashi wawili au watatu wakachungulia nje.
33 On reče: “Bacite je dolje.” I oni je baciše. Njena je krv poprskala zidove i konje, koji je pogaziše.
Basi Yehu aksema, “Mtupeni chini.” Hivyo wakamtupa Yezebeli chini, na damu yake nyingine ikamwagika kwenye ukuta na farasi, na Yehu akamkanyaga kanyaga chini ya miguu.
34 Ušao je on, jeo i pio, a zatim naredio: “Pogledajte onu prokletnicu i sahranite je, jer je bila kraljevska kći.”
Basi Yehu akaingia hiyo sehemu, akala na kunywa. Kisha akasema, “Mtazamani sasa huyu mwanamke aliyelaaniwa na kumzika, kwa kuwa ni binti wa mfalme.”
35 I odoše da je sahrane, ali ne nađoše ništa od nje, osim lubanje, nogu i ruku.
Wakaenda kumzika, lakini hawakumkuta ila fuvu, miguu, na viganga vya mikono yake.
36 Vratiše se i javiše, a Jehu reče: “To je riječ koju je Jahve objavio preko svoga sluge Ilije Tišbijca: 'U polju jizreelskom psi će proždrijeti Izebelino tijelo.
Basi wakarudi na kumwambia Yehu. Akasema, “Hili ndilo neno la Yahwe ambalo ameliongea kupitia Eliya Mtishbi, likisema, 'Katika nchi Yezreeli mbwa ataula mwili wa Yezebeli,
37 Izebelino truplo bit će kao gnoj u polju, da se neće moći kazati: Ovo je Izebela.'”
na mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema, “Huyu ni Yezebeli.””

< 2 Kraljevima 9 >