< 2 Kraljevima 24 >

1 U njegovo je vrijeme došao Nabukodonozor, kralj babilonski, i Jojakim mu je bio podložan tri godine, zatim se ponovno pobunio protiv njega.
Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
2 Ovaj pak posla protiv njega kaldejske pljačkaške čete, aramejske, moapske i amonske, sve ih posla protiv Judeje da je opustoše, potvrđujući riječ koju je Jahve bio objavio po slugama svojim prorocima.
Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
3 To se dogodilo Judeji prema prijetnji Jahvinoj da će je istrijebiti ispred svoga lica zbog grijeha Manašeovih: zbog svega što je Manaše učinio
Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
4 i zbog nedužne krvi koju je prolio, natopio Jeruzalem krvlju nedužnom. Jahve nije htio oprostiti.
ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
5 Ostala povijest Jojakimova i sve što je učinio, zar sve to nije zapisano u knjizi Ljetopisa judejskih kraljeva?
Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
6 Jojakim je počinuo kraj svojih otaca, a njegov sin Jojakin zavlada mjesto njega.
Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 Egipatski kralj nije više izlazio iz zemlje, jer je babilonski kralj osvojio od Egipatskog potoka do rijeke Eufrata sve što je pripadalo egipatskom kralju.
Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
8 Jojakinu je bilo osamnaest godina kad se zakraljio i kraljevao je tri mjeseca u Jeruzalemu. Materi mu je bilo ime Nehušta, kći Elnatana, i bila je iz Jeruzalema.
Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
9 On je činio što je zlo u očima Jahvinim, sve kao što je činio i njegov otac.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
10 U ono vrijeme krenu ljudstvo babilonskog kralja Nabukodonozora protiv Jeruzalema i grad je bio opkoljen.
Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
11 Dođe i babilonski kralj Nabukodonozor da napadne grad, dok ga je njegovo ljudstvo opsjedalo.
Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
12 Tada je judejski kralj Jojakin izišao pred babilonskoga kralja: on, njegova majka, njegove sluge, njegove vojskovođe i dvorani, a babilonski kralj zarobi ga - osme godine svoga kraljevanja.
Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
13 On je odnio sve iz riznice Doma Jahvina i iz riznica kraljevskog dvora i razbio je sve zlatne predmete koje je Salomon, kralj Izraela, načinio za Svetište Jahvino. Tako se ispunila riječ Jahvina.
Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
14 Odveo je u progonstvo sav Jeruzalem, sve vojskovođe i sve vrsne ratnike, oko deset tisuća prognanika, sa svim kovačima i bravarima. Jedino je preostao najsiromašniji narod zemlje.
Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
15 Odveo je Jojakina u Babilon; tako isto i kraljevu majku i sve žene kraljeve, njegove dvorane, plemenitaše zemlje, sve ih je odveo iz Jeruzalema u progonstvo u Babilon.
Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
16 Sve sposobne ljude, njih sedam tisuća na broju; kovače i bravare, tisuću na broju; sve ljude sposobne za boj, sve ih je kralj babilonski odveo u Babilon, u sužanjstvo.
Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
17 Babilonski je kralj postavio za kralja mjesto Jojakina njegova strica Mataniju, ali mu je promijenio ime u Sidkija.
Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
18 Sidkiji je bila dvadeset i jedna godina kad se zakraljio, a kraljevao je jedanaest godina u Jeruzalemu. Materi mu bijaše ime Hamitala, kći Jeremije, i bila je iz Libne.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
19 Činio je što je zlo u očima Jahvinim, sve kao što je činio Jojakin.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
20 To je zadesilo Jeruzalem i Judu zbog gnjeva Jahvina; Jahve ih napokon i odbaci ispred lica svoga. Sidkija se pobuni protiv babilonskog kralja.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

< 2 Kraljevima 24 >