< 2 Ljetopisa 9 >

1 Uto kraljica od Sabe ču glas o Salomonu; hoteći iskušati Salomona zagonetkama, dođe u Jeruzalem s mnogobrojnom pratnjom i s devama koje su nosile miomirise, mnogo zlata i dragulja. Došavši k Salomonu, porazgovori se s njim o svemu što joj bijaše na srcu.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
2 Salomon joj odgovori na sva pitanja; nije bilo Salomonu sakriveno ništa da joj ne bi umio objasniti.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
3 Kad kraljica od Sabe vidje njegovu mudrost, dvor koji bijaše sagradio,
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
4 jela na njegovu stolu, odaje njegove i dvorane, otmjenost njegove posluge i njihova odijela, i njegove peharnike i njihova odijela, i njegove paljenice koje je prinosio u Jahvinu domu, zastade joj dah.
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
5 Tada reče kralju: “Istina je bila što sam u svojoj zemlji čula o tebi i o tvojoj mudrosti.
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
6 Ali nisam htjela vjerovati što se pripovijeda dokle god nisam došla i vidjela na svoje oči; i doista, ni pola mi nije bilo rečeno o tvojoj velikoj mudrosti; nadvisio si glas koji sam slušala.
Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
7 Blago tvojim ljudima i tvojim slugama koji stoje pred tobom i slušaju tvoju mudrost!
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
8 Neka je blagoslovljen Jahve, tvoj Bog, komu si tako omilio da te postavio na svoje prijestolje da kraljuješ umjesto Jahve, svojega Boga, jer Bog tvoj ljubi Izraela da bi ga održao dovijeka; i zato je postavio tebe za kralja da činiš pravo i pravicu.”
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
9 Dala je tada kralju sto i dvadeset zlatnih talenata i mnogo miomirisa i dragulja. Nikad više nije bilo takvih miomirisa kakve je kraljica od Sabe dala kralju Salomonu.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
10 Hiramove sluge, koje su sa Salomonovim slugama donosile zlata iz Ofira, dovezle su također sandalovine i dragulja.
(Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
11 Kralj je napravio i citre i harfe za pjevače: nikad se prije nisu vidjele takve stvari u zemlji judejskoj.
Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
12 Kralj Salomon dade kraljici od Sabe što je zaželjela i zatražila, izuzev ono što je sama donijela kralju. Potom ona krenu i sa slugama ode u svoju zemlju.
Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
13 Zlato što je dolazilo Salomonu svake godine bilo je teško šest stotina šezdeset i šest zlatnih talenata,
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
14 osim onoga što je dolazilo od trgovaca i putujućih prodavača. I svi su arapski kraljevi i zemaljski upravitelji Salomonu donosili zlato i srebro.
mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
15 Kralj Salomon načini dvjesta štitova od kovanoga zlata; za svaki je štit upotrijebio šest stotina šekela kovanoga zlata;
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
16 i načini trista štitića od kovanoga zlata; za svaki je štitić utrošio trista zlatnih šekela. Kralj ih je pohranio u kuću zvanu Libanonska šuma.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
17 Kralj je napravio i veliko prijestolje od bjelokosti i obložio ga čistim zlatom.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
18 Prijestolje je imalo šest stepenica i zlatno podnožje sastavljeno s prijestoljem, i ručice s obiju strana prijestolja, a kraj ručica stajala dva lava.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
19 Dvanaest je lavova stajalo s obiju strana onih šest stepenica. Takvo što nije bilo izrađeno ni u jednom kraljevstvu.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
20 Sve posude iz kojih je pio kralj Salomon bijahu zlatne i sve posuđe u kući zvanoj Libanonska šuma bijaše od suhoga zlata; srebro se smatralo bezvrijednim u Salomonovo vrijeme.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
21 Kraljeve su lađe išle u Taršiš s Hiramovim slugama; svake treće godine vraćale su se i dolazile taršiške lađe donoseći zlato i srebro, slonovu kost, majmune i paune.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
22 Tako je kralj Salomon natkrilio sve zemaljske kraljeve bogatstvom i mudrošću.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
23 Svi su zemaljski kraljevi željeli vidjeti Salomona i čuti mudrost koju mu je Bog ulio u srce.
Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
24 Svatko mu je donosio dar, srebrno i zlatno posuđe, haljine, oružje i miomirise, konje i mazge, iz godine u godinu.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
25 Salomon je imao četiri tisuće konjskih jasala i bojnih kola i dvanaest tisuća konjanika, koje je rasporedio po gradovima bojnih kola i kod kralja u Jeruzalemu.
Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
26 Vladao je nad svim kraljevima od Rijeke do zemlje filistejske i do egipatske međe.
Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
27 Kralj je učinio da u Jeruzalemu bude srebra kao kamenja, a cedrova kao divljih smokava što rastu u Judejskoj nizini.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Salomon je uvozio konje iz Musrija i iz svih zemalja.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
29 Ostala djela Salomonova, od prvih do posljednjih, zapisana su u povijesti proroka Natana, u proročkoj knjizi Šilonjanina Ahije i u proročkoj besjedi vidioca Adona o Nebatovu sinu Jeroboamu.
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
30 Salomon je vladao u Jeruzalemu nad svim Izraelom četrdeset godina.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
31 Potom je počinuo kod otaca i sahranili su ga u gradu oca mu Davida, a na njegovo se mjesto zakraljio sin mu Roboam.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Ljetopisa 9 >