< 2 Ljetopisa 33 >
1 Manašeu je bilo dvanaest godina kad se zakraljio. Pedeset i pet godina kraljevao je u Jeruzalemu.
Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na mbili alipoanza kutawala, alitawala miaka hamsini na tano katika Yerusalemu.
2 Činio je što je zlo u Jahvinim očima, povodeći se za gnusobama naroda što ih je Jahve protjerao pred sinovima Izraelovim.
Akafanya yalikuwa uovu katika macho ya Yahwe, kama yalivyo mambo ya machukizo ya mataifa ambao Yahwe alikuwa amewafukuza mbele ya watu wa Israeli.
3 Obnovio je uzvišice što ih bijaše oborio otac mu Ezekija, podigao je žrtvenike Baalu, načinio ašere i stao se klanjati svoj nebeskoj vojsci i služiti joj.
Kwa maana alizijenga tena sehemu za juu ambazo baba yake Hezekia alikuwa amezibomoa, na akajenga madhabahu kwa ajili ya mabaali, akatengeneza sanaamu za Maashera, na akaziinamia chini nyota zote za mbinguni na kuziabudu.
4 Podigao je žrtvenike i u Domu Jahvinu, za koji bijaše rekao Jahve: “U Jeruzalemu će prebivati Ime moje zauvijek.”
Manase akajenga madhbahu za kipagani katika nyumba ya Yahwe, ingawa Yahwe alikuwa amemwamuru, “Ni katika Yerusalemu ambamo jina langu litawekwa milele”.
5 Sagradio je žrtvenike svoj nebeskoj vojsci u oba predvorja Doma Jahvina.
Alijenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika vile viwanja viwili vya nyumba ya Yahwe.
6 I sinove je svoje proveo kroz oganj u dolini Hinomova sina. Vračao je, gatao, čarao, stvorio bajače i opsjenare i uopće učinio premnogo zla u Jahvinim očima razjarujući ga.
Katika bonde la Beni Hinomu akawaweka wanaye katika moto. Akafanya misemo ya ubashiri, na uchawi, akassoma utabiri; akashauriana na wale waliozungumza na wafu na wale waliozungumza na na roho. Akafanaya maaovu mengi katika mcho ya Yahwe na alimfanya Mungu akasirike.
7 Načinio je idolski lik i posadio ga u Domu Božjem, za koji Bog bijaše rekao Davidu i njegovu sinu Salomonu: “U ovom Domu i u Jeruzalemu, koji sam izabrao među svim izraelskim plemenima, postavit ću Ime svoje zauvijek.
Ile sanamu ya Maashera aliyokuwa amefanya, akaipeleka katika nyumba ya Mungu. Ni kuhusu nyumba hii ambayo Mungu alikuwa amesema kwa Daudi na Selemani mwanaye; alikuwa amesema, “Ni katika nyumba hii na katika Yerusalemu, ambao nimeuchangua kutoka makabila yote ya Israeli, kwamba nitaliweka jina langu milele.
8 Neću više dati da noga Izraelaca uzmakne iz zemlje koju sam dao u baštinu vašim očevima, samo ako budu držali i provodili u djelo sve što sam im zapovjedio: sav Zakon, uredbe i običaje dane preko Mojsija.”
Sitawaondoa tena watu wa Israeli katina nchi hii ambayo niliitoa kwa babu zao, ikiwa tu watakuwa makini katika kuyashika yote niliyowaamuru, kuzishika sheria zangu, amri zangu, na sheria zangu nilizowapa kupitia Musa.”
9 Ali je Manaše zaveo Judejce i Jeruzalemce te su radili još gore nego narodi što ih je Jahve iskorijenio pred sinovima Izraelovim.
Manase akawaongoza Yuda na wakaaji wa Yerusalemu hata kufanya uovu zaidi kuliko hata watu wa mataifa ambao Yahwe alikuwa amewateketeza mbele za Israeli.
10 Jahve je opominjao Manašea i njegov narod, ali oni nisu poslušali.
Yahwe akasema kwa Manase, na kwa watu wake wote, lakini hawakumsikiliza.
11 Stoga je Jahve doveo na njih vojskovođe asirskoga kralja. Uhvativši Manašea kukama, svezali su ga u dvoje mjedene verige i odveli u Babilon.
Kwa hiyo Yahwe akaleta juu yao maamri jeshsi wa jeshi la Ashuru, ambao walimchukua Manase katika minyonyoro, wakamfunga kwa pingu, na wakampeleka Babeli.
12 Kad se našao u nevolji, počeo se moliti za milost Jahvi, svome Bogu, ponizivši se veoma pred Bogom otaca.
Manase alipokuwa katika dhika, alimuomba Yahwe, Mungu wake, na akajinyenyekesha sana mbele za Mungu wa babu zake.
13 Molio se i Bog mu se smilovao te usliša njegovu prošnju i vrati ga u Jeruzalem u kraljevstvo. Manaše tada spozna da je Jahve Bog.
Akaomba kwake; na Mungu akamsikiliza, na Mungu akasikia kuomba kwake na akamrudisha Yerusalemu, katika ufalme wake. Kisha Manase akafahamu kwamba Yahwe alikuwa Mungu.
14 Poslije toga sagradio je vanjski zid Davidovu gradu zapadno od Gihona, od doline pa do Ribljih vrata, i opasao zidom Ofel, izvevši ga vrlo visoko. Postavio je bojne vojvode u svim tvrdim gradovima u Judi.
Baada ya hayo, manase akajenga ukuta wa nje ya mji wa Daudi, upande wa magharibi wa Gihoni, katika bonde, hadi kwenye lango la Samaki. Akauzungushia mlima wa Ofeli na akaupandisha ukuta hadi usawa mrefu sana. Akaweka maamri jeshi jasiri katika ngome zote za miji ya Yuda.
15 Osim toga, uklonio je iz Jahvina Doma tuđinske bogove, onaj idolski lik i sve žrtvenike što ih bijaše posagradio na gori Jahvina Doma i u Jeruzalemu i sve ih baci izvan grada.
Akaipeleka mbali miungu yote ya kigeni, akaondoa sanamu zote kwenye nyumba ya Yahwe, na madhabahu zote ambazo alikuwa amejenga juu ya mlima wa nyumba ya Yahwe na katika Yerusalemu, na kuvitupa nje ya mji.
16 Zatim opet podiže Jahvin žrtvenik i žrtvova na njemu žrtve pričesnice i zahvalnice. Zapovjedi i Judejcima da služe Jahvi, Bogu Izraelovu.
Akaijenga tena madhabahu ya Yahwe na juu yake akatoa sadaka za amani na sadaka za shukrani; akamwamuru Yuda amtumikie Yahwe, Mungu wa Israeli.
17 Ipak je narod još žrtvovao po uzvišicama, ali samo Jahvi, svojem Bogu.
Hata hivyo watu bado walitoa sadaka mahali pa sehemu za juu, lakini kwa Yahwe, Mungu wao pekee.
18 Ostala Manašeova djela i njegova molitva Bogu, riječi koje su mu govorili vidioci u ime Jahve, Izraelova Boga, zapisane su u Povijesti izraelskih kraljeva.
Katika mambo mengine kuhusu Manase, maombi yake kwa Mungu wake, na maneno ya waonaji ambao walisema kwake katika jina la Yahwe, Mungu wa Israeli, tazama, yameandikwa miongoni mwa matendo ya wafalme wa Israeli.
19 Njegova molitva i kako je bio uslišan, svi njegovi grijesi i njegova nevjera te mjesta na kojima je pogradio uzvišice, podigao ašere i idole prije nego što se ponizio - sve je to zapisano u povijesti Hozajevoj.
Katika matukio hayo kuna historia ya maombi yake, na jinsi Mungu alivyoguswa na maomabi hayo. Pia kuna kumbu kumbu ya dhambi zake zote na makosa yake, na sehemu ambako alikuwa amejenga sehemu za juu na kuzisimamisha Maashera na sanamu za kuchonga, kambla ya kujinyenyekesha mwenyewe — na imeandikwa kuhusu hayo katika tarehe ya waonaji. (Maandishi ya kale yanasema hivi, “tarehe ya Hozai,” ambayo ni maandishi ya kifungu asili. Lakini matoleo mengi ya kisasa yamesahihisha na kusomeka “tarehe ya waonaj” Pia, matoleo machache ya kisasa yanasema “tarehe ya waonaji”.).
20 Tada Manaše počinu kraj svojih otaca. Sahranili su ga u dvoru. Na njegovo se mjesto zakraljio sim mu Amon.
Kwa hiyo Manase akalala na babu zake, na wakamzika katika nyumba yake mwenyewe. Amoni, mwaye, akawa mfalme katika nafasi yake.
21 Dvadeset su i dvije godine bile Amonu kad se zakraljio, a kraljevao je dvije godine u Jeruzalemu.
Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na mbili alipoanza kutawala; alitawala miaka miwili katika Yerusalemu.
22 Činio je što je zlo u Jahvinim očima, kao i otac mu Manaše, jer je svim idolima koje bijaše načinio njegov otac Manaše on prinosio žrtve i služio im.
Akafanya yaliyokuwa uovu katika macho ya Yaahwe, kama Manase, baba yake, alivyofanya. Amoni alitoa sadaka katika sanamau zote za kuchonga ambazo alitengeneza Manase baba yake, na aliziabudu.
23 Ali se nije ponizio pred Jahvom kako se ponizio otac mu Manaše, nego je još i umnožio svoju krivicu.
Hakujinyenyekesha mbele za Yahwe, kama baba yake Manase alivyokuwa amefanya. Badala yake, Amoni huyu huyu alifanya makosa zaidi na zaidi.
24 Tada se protiv njega urotiše njegove sluge i ubiše ga u dvoru.
Watumishi wake wakapanga njama wa zidi yake na wakamua katika nyumba yake mwenyewe.
25 Ali je prosti puk pobio sve one koji se bijahu urotili protiv kralja Amona i na njegovo mjesto zakraljio sina mu Jošiju.
Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliofanya njama zidi ya Mfalme Amoni, na wakamfanya Yosia, mwanaye, mfalme katika nafasi yake.