< 1 Samuelova 9 >

1 Živio u ono vrijeme jedan čovjek u Benjaminovu plemenu po imenu Kiš, sin Abiela, sina Serora, sina Bekorata, sina Afijahova; bio je iz plemena Benjaminova, čovjek imućan.
Kulikuwako Mbenyamini mmoja, mtu maarufu, ambaye aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia wa Benyamini.
2 Imao je sina po imenu Šaula, koji je bio mlad i lijep. Među sinovima Izraelovim nije bilo ljepšega čovjeka od njega: za glavu bijaše viši od svega naroda.
Alikuwa na mwana aliyeitwa Sauli, kijana anayevutia sana, hakuwepo aliyelingana naye miongoni mwa Waisraeli, alikuwa mrefu kuliko wengine wote.
3 Uto se Kišu, Šaulovu ocu, izgubilo nekoliko magarica, pa Kiš reče svome sinu Šaulu: “Uzmi sa sobom jednoga momka pa ustani i idi tražiti magarice!”
Basi punda wa Kishi baba yake Sauli walipotea, naye Kishi akamwambia mwanawe Sauli, “Mchukue mmoja wa watumishi mwende pamoja naye kuwatafuta punda.”
4 I prođoše oni Efrajimovu goru i prođoše zemlju Šališu, ali ne nađoše ništa; prođoše zemlju Šaalim, ali magarica ne bijaše ondje; prođoše i zemlju Benjaminovu, ali ne nađoše ništa.
Hivyo akapita katika nchi ya vilima ya Efraimu na katika eneo la Shalisha, lakini hawakuwapata. Wakaendelea katika sehemu ya Shaalimu, lakini punda hawakuwepo huko. Kisha wakapita katika nchi ya Benyamini, lakini hawakuwapata.
5 Kad su došli u zemlju Suf, reče Šaul momku koji ga je pratio: “Hajde, vratimo se da se ne bi otac okanio magarica i zabrinuo se za nas!”
Walipofika sehemu ya Sufu, Sauli akamwambia mtumishi aliyekuwa pamoja naye, “Njoo, sisi na turudi, au baba yangu ataacha kufikiria juu ya punda na kuanza kufadhaika kutuhusu sisi.”
6 A on mu odgovori: “Eno, u onom ondje gradu živi čovjek Božji; to je vrlo ugledan čovjek: što god rekne, sve se zacijelo ispunja. Pođimo, dakle, k njemu, možda će nas uputiti u ono zbog čega smo pošli na put.”
Lakini mtumishi akajibu, “Tazama, katika mji huu yupo mtu wa Mungu, anayeheshimiwa sana na kila kitu asemacho hutokea kweli. Sasa na twende huko. Huenda atatuambia twende njia ipi.”
7 A Šaul reče svome momku: “Ako zaista pođemo onamo, što ćemo ponijeti čovjeku? Kruha je nestalo u našim torbama, nemamo dara da ponesemo čovjeku Božjem. Što mu možemo dati?”
Sauli akamwambia mtumishi wake, “Kama tukienda, tutampa nini huyo mtu? Chakula kimekwisha kwenye mifuko yetu. Hatuna zawadi ya kumpelekea huyo mtu wa Mungu. Je tuna nini?”
8 A momak opet progovori i reče Šaulu: “Gle, imam u ruci četvrt šekela srebra: dat ću ga Božjem čovjeku da nas uputi kamo bismo išli.”
Mtumishi akamjibu Sauli tena, akasema, “Tazama, nina fedha robo shekeli. Hiyo nitampa huyo mtu wa Mungu ili aweze kutuambia twende kwa njia ipi.”
9 Nekoć se u Izraelu, kad bi išli pitati Boga za savjet, govorilo: “Hajde, pođimo k vidiocu!” Jer koga danas zovu prorokom nekoć se zvao vidjelac. -
(Zamani katika Israeli, kama mtu alikwenda kuuliza neno kwa Mungu, angalisema, “Njoo na twende kwa mwonaji,” kwa sababu nabii wa sasa alikuwa akiitwa mwonaji.)
10 Šaul odvrati svome momku: “Dobro veliš. Hajdemo!” I krenuše u grad gdje je živio čovjek Božji.
Sauli akamwambia mtumishi wake, “Vyema, njoo na twende.” Basi wakaenda mjini alipokuwepo huyo mtu wa Mungu.
11 Kad su se penjali usponom prema gradu, sretoše djevojke koje su izašle da zahvate vode. I zapitaše ih: “Je li gore vidjelac?” -
Walipokuwa wakipanda mlima kwenda mjini, wakakutana na baadhi ya wasichana wanakuja kuchota maji, nao wakawauliza, “Je, mwonaji yuko?”
12 One im odgovore ovako: “Jest, vidjelac je pred vama. Upravo je stigao u grad, jer danas narod ima žrtvu na uzvišici.
Wakajibu, “Yuko, yu mbele yenu amewatangulia, sasa fanyeni haraka, ndiyo tu amekuja mjini kwetu leo, kwa kuwa watu wana dhabihu huko mahali pa juu.
13 Čim uđete u grad, naći ćete ga još prije nego što se popne na uzvišicu da sudjeluje na žrtvenoj gozbi. Narod neće jesti dok on ne dođe, jer on mora blagosloviti žrtvu, a onda će tek uzvanici jesti. Zato idite odmah gore, jer ćete ga sada još naći.”
Mara tu mwingiapo mjini, mtamkuta kabla hajapanda kwenda mahali pa juu kula. Watu hawataanza kula mpaka atakapofika kwa sababu ni lazima kwanza yeye abariki dhabihu, ndipo wale walioalikwa watakapokula. Pandeni sasa, mtamkuta kwa wakati huu.”
14 Oni otiđoše gore u grad. Kad su ulazili na vrata, Samuel ih susrete polazeći na uzvišicu.
Wakapanda mjini, nao walipokuwa wakiingia mjini, tazama, Samweli alikuwa akija kuelekea walikokwenda mahali pa juu.
15 A dan prije nego što je Šaul došao bijaše Jahve objavio Samuelu:
Basi siku moja kabla Sauli hajaja, Bwana alikuwa amemfunulia Samweli jambo hili:
16 “Sutra u ovo doba poslat ću k tebi čovjeka iz Benjaminove zemlje. Ti ćeš ga pomazati za kneza nad mojim narodom Izraelom. On će izbaviti moj narod iz ruke filistejske. Vidio sam nevolju svoga naroda i njegov je vapaj dopro do mene.”
“Kesho wakati kama huu nitakupelekea mtu kutoka nchi ya Benyamini. Umtie mafuta awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli, ndiye atakayewakomboa watu wangu na mkono wa Wafilisti. Nimewaangalia watu wangu, kwa kuwa kilio chao kimenifikia.”
17 A kad je Samuel ugledao Šaula, Jahve mu progovori: “Evo ti čovjeka za koga ti rekoh: 'Taj će vladati nad mojim narodom.'”
Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekuambia habari zake, kwamba yeye atawatawala watu wangu.”
18 Šaul pristupi Samuelu na vratima i reče: “Daj mi kaži gdje je vidiočeva kuća.”
Sauli akamkaribia Samweli langoni na kumuuliza, “Tafadhali, je, waweza kuniambia mahali nyumba ya mwonaji ilipo?”
19 A Samuel odgovori Šaulu: “Ja sam vidjelac. Pođi preda mnom na uzvišicu, danas ćete sa mnom jesti. Sutra ću te ujutro otpustiti i sve ću ti kazati što ti je na srcu.
Samweli akamjibu Sauli, “Mimi ndiye mwonaji, panda utangulie mbele yangu mpaka mahali pa juu, kwa kuwa leo itakupasa kula pamoja nami na asubuhi nitakuruhusu uende na nitakuambia yale yote yaliyo moyoni mwako.
20 A za magarice koje su ti se izgubile prije tri dana ne uznemiruj se jer su se našle. Uostalom, kome pripada sve što je najdragocjenije u Izraelu? Zar ne tebi i svemu domu tvoga oca?”
Kuhusu wale punda uliowapoteza siku tatu zilizopita, usifadhaike kwa habari yao; wamepatikana. Ni kwa nani ambaye shauku yote ya Israeli imeelekea, kama si kwako na jamaa yote ya baba yako?”
21 A Šaul odgovori ovako: “Nisam li ja od Benjaminova plemena, najmanjega plemena Izraelova? A moj rod nije li najneznatniji između svih rodova Benjaminova plemena? Zašto mi, dakle, govoriš takve riječi?”
Sauli akajibu, “Je, mimi si Mbenyamini, kutoka kabila dogo kuliko yote ya Israeli, nao ukoo wangu si ndio mdogo kuliko koo zote za kabila la Benyamini? Kwa nini uniambie jambo la namna hiyo?”
22 Samuel uze Šaula i njegova momka, odvede ih u sobu i dade im mjesto u pročelju među uzvanicima, kojih je bilo tridesetak.
Kisha Samweli akamleta Sauli na mtumishi wake ndani ukumbini na kuwaketisha mahali pa heshima zaidi miongoni mwa wale waliokuwa wamealikwa; jumla yao walikuwa kama watu thelathini.
23 Zatim Samuel reče kuharu: “Donesi dio koji ti dadoh i za koji ti rekoh da ga staviš na stranu.”
Samweli akamwambia mpishi, “Leta ile sehemu ya nyama niliyokupa, ile niliyokuambia iweke kando.”
24 Kuhar uze but, donese ga i stavi pred Šaula, a Samuel mu reče: “Evo, pred tobom je ono što je sačuvano za tebe. Jedi, jer to ti je sačuvano baš za ovu zgodu.” Tako je u onaj dan Šaul jeo sa Samuelom.
Hivyo mpishi akachukua mguu pamoja na kile kilichokuwa juu yake akaiweka mbele ya Sauli. Samweli akasema, “Hiki ndicho ambacho kimewekwa kwa ajili yako. Ule, kwa sababu kilitengwa kwa ajili yako kwa tukio hili, tangu niliposema, ‘Nimewaalika wageni.’” Naye Sauli akala pamoja na Samweli siku ile.
25 Potom odande siđoše u grad. Ondje prostriješe Šaulu na krovu.
Baada ya kushuka kutoka mahali pa juu na kufika mjini, Samweli alizungumza na Sauli juu ya dari ya nyumba yake.
26 I on leže na počinak. Čim je svanula zora, Samuel zovnu Šaula (na krovu) govoreći: “Ustani da te otpustim!” Kad je Šaul ustao, izađoše obojica, on i Samuel.
Walipoamka mapema alfajiri, Samweli akamwita Sauli darini, akamwambia, “Jiandae, nami nitakuaga uende zako.” Sauli alipokuwa tayari yeye na Samweli wakatoka nje pamoja.
27 Kad su došli na kraj grada, reče Samuel Šaulu: “Kaži momku neka pođe naprijed pred nama! A ti stani sada da ti objavim riječ Božju.”
Hata walipokuwa wakiteremka kuelekea mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi atangulie mbele yetu.” Naye mtumishi akafanya hivyo. “Lakini subiri hapa kwa kitambo kidogo, ili nipate kukupa ujumbe kutoka kwa Mungu.”

< 1 Samuelova 9 >