< 1 Samuelova 23 >
1 Javiše onda Davidu: “Filistejci opsjedaju Keilu i pljačkaju gumna.”
Wakamwambia Daudi, “Tazama, Wafilisti wanaupiga Keila na wanapora nafaka inayopurwa.”
2 David tada upita Jahvu: “Treba li da idem na Filistejce i hoću li ih potući?” A Jahve odgovori Davidu: “Idi, potući ćeš Filistejce i oslobodit ćeš Keilu.”
Hivyo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, na akamuuliza,” Je, niondoke niwapige hawa Wafilisti? BWANA akamwambia Daudi, “Nenda ukawapige Wafilisti na kuokoa Keila.”
3 Ali rekoše Davidu ljudi njegovi: “Gle, mi smo već ovdje, u Judi, u neprestanom strahu; što će tek biti ako odemo u Keilu protiv filistejskih četa!”
Daudi akaambiwa na watu wake, “Angalia, hapa Yuda tunaogopa. Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?”
4 Zato David još jednom upita Jahvu, a Jahve mu odgovori ovako: “Ustani i siđi u Keilu jer ću predati Filistejce u tvoje ruke!”
Ndipo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, bado tena, BWANA akamjibu, “Amka, uteremke hadi Keila. Maana nitakupatia ushindi dhidi ya Wafilisti.”
5 David onda krenu sa svojim ljudima u Keilu, udari na Filistejce, otjera njihovu stoku i zada im težak poraz. Tako je David oslobodio građane Keile. -
Daudi na watu wake wakaenda Keila na kupigana na Wafilisti. Wakahamisha ng'ombe wao na kuwapiga kwa mauaji makubwa mno. Hivyo Daudi akawaokoa wenyeji wa Keila.
6 Kad je ono Ebjatar, Ahimelekov sin, pobjegao k Davidu, on je došao u Keilu noseći u ruci oplećak.
Abiathari mwana wa Ahimeleki alipokuwa amekimbilia kwa Daudi huko Keila, alibeba naivera mkononi mwake.
7 Kad su Šaulu javili da je David ušao u Keilu, reče Šaul: “Bog ga je predao u moje ruke jer se sam uhvatio u zamku kad je ušao u grad s vratima i prijevornicama.”
Sauli aliambiwa kwamba Daudi amekwenda Keila. Sauli akasema, “Mungu amemweka mkononi mwangu. Bila shaka amefungiwa ndani kwa sababu ameingia katika mji ulio na malango na makomeo.”
8 I Šaul sazva sav narod na oružje da ide na Keilu i da opkoli Davida i njegove ljude.
Sauli akayaita majeshi yake yote kwa ajili ya vita, waende hadi Keila, wamteke Daudi na watu wake.
9 Kad je David doznao da mu Šaul snuje zlo, reče svećeniku Ebjataru: “Donesi oplećak!”
Daudi alijua kwamba Sauli alikuwa anapanga njama za kumdhuru yeye. Ndipo akamwambia kuhani Abiathari kuhani, “Ulete hapa naivera.”
10 Nato se David pomoli: “Jahve, Bože Izraelov, tvoj je sluga čuo da Šaul sprema navalu na Keilu da razori grad zbog mene.
Kisha Daudi akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, mtumishi wako hakika amesikia kwamba Sauli anatafuta namna ya kuja Keila, ili auteketeze mji kwa ajili yangu.
11 Hoće li Šaul doći kao što je tvoj sluga čuo? Jahve, Bože Izraelov, odgovori svome sluzi!” A Jahve odgovori: “Doći će!”
Je, watu wa Keila watanisalimisha mkononi mwake? Je, Sauli atashuka hadi huko, kama mtumishi wako alivyosikia? BWANA, Mungu wa Israeli, nakusihi, tafadhali mwambie mtumishi wako. “BWANA akasema, “Atakuja huko.”
12 David opet upita: “Hoće li me prvaci Keile predati, mene i moje ljude, u Šaulove ruke?” A Jahve odgovori: “Predat će vas!”
Kisha Daudi akauliza, “Je, watu wa Keila watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli?” BWANA akasema, “Watu hao watawasalimisha kwao.”
13 Tada David ustade sa svojim ljudima, bijaše ih oko šest stotina; iziđoše iz Keile te lutahu kojekuda. A kad su Šaulu javili da je David utekao iz Keile, odusta od vojnog pohoda.
Kisha Daudi na watu wake, waliokuwa kama mia sita, walitoka na kwenda mbali na Keila, na wakazunguka kila sehemu. Kisha Sauli akaambiwa kwamba Daudi ametoroka kutoka Keila, hivyo akasitisha kumfuatia.
14 David se skloni u pustinju u gorska skloništa; nastani se na gori u pustinji Zifu. Šaul ga je neprestano tražio, ali ga Bog ne predade u njegove ruke.
Daudi alikaa ngomeni katika jangwa, kwenye nchi ya milima katika jangwa la Zifu. Kila siku Sauli alimtafuta, lakini Mungu hakumweka mkononi mwake.
15 David se bojao što je Šaul izišao na vojnu da napadne na njegov život. Zato je David ostao u pustinji Zifu, u Horši.
Daudi aliona kwamba Sauli amejitokeza kuangamiza maisha yake; basi Daudi alikuwa katika jjangwa la Zifu huko Horeshi.
16 Tada Šaulov sin Jonatan krenu na put i dođe k Davidu u Horšu i ohrabri ga u ime Božje.
Kisha Yonathani, mwana wa Sauli, akaamuka akaenda kwa Daudi huko Horshi, naye akamtia moyo amtumainie Mungu.
17 Reče mu: “Ne boj se, jer te neće stići ruka moga oca Šaula. Ti ćeš kraljevati nad Izraelom, a ja ću biti drugi do tebe; i moj otac Šaul zna to dobro.”
Akamwambia, “Usiogope. Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, na mimi nitakuwa msaidizi wako. Baba yangu Sauli pia anajua hivyo.”
18 I sklopiše njih dvojica savez pred Jahvom. David osta u Horši, a Jonatan ode svojoj kući.
Basi wote wawili wakafanya agano mbele za BWANA. Kisha Daudi alibaki Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani.
19 Jednoga dana dođoše Zifejci k Šaulu u Gibeu i javiše mu: “David se krije kod nas u gorskim skloništima u Horši, na brdu Hakili, što je južno od Ješimona.
Nndipo Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea wakisema, “Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ngome huko Horeshi, juu ya mlima wa Hakila, ulioko kusini mwa Yeshimoni?
20 Sada, kralju, kad god zaželiš sići, siđi, a naše je da ga predamo u ruke kralju.”
Basi uje, mfalme! Kulingana na matakwa yako, uje! Kazi yetu itakuwa kumtia katika mkono wa mfalme.”
21 A Šaul odgovori: “Blagoslovio vas Jahve što ste me požalili!
Sauli akasema, “Mbarikiwe na BWANA. Kwa sababu mmenihurumia.
22 Idite, dakle, raspitajte se još i dobro razvidite mjesto kamo ga donesu njegovi hitri koraci; rekli su mi da je vrlo lukav.
Nendeni, mhakikishe sawasawa. Tafuteni na kujua maficho yake yako wapi na ni nani amemwona huko. Nimeambiwa kwamba yeye ni mjanja sana.
23 Zato pretražite sve rupe u koje se zavlači, pa se vratite k meni kad budete pouzdano znali. Tada ću ja poći s vama, pa ako bude gdje u zemlji, ići ću za njegovim tragom po svim Judinim rodovima.”
Kwa hiyo chunguzeni, mjue sehemu zote anakojificha. Baadaye rudini kwangu mkiwa na taarifa kamili, na kisha nitaongozana nanyi. Ikiwa yupo katika nchi, nitamtafuta kutoka miongoni mwa elfu zote za Yuda.”
24 Tada krenuše na put i odoše u Zif, pred Šaulom. David je sa svojim ljudima bio u pustinji Maonu u Arabi, južno od Ješimona.
Ndipo wakaamka na kwenda hadi Zifu mbele ya Sauli. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa katika jangwa la Maoni, huko Araba upande wa kusini mwa Yeshimoni.
25 Potom i Šaul pođe sa svojim ljudima da traži Davida. Kad su to javili Davidu, siđe on u klanac koji leži u pustinji Maonu. Šaul to doznade i krenu u potjeru za Davidom u pustinju Maon.
Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta Daudi. Na Daudi akaambiwa habari hiyo, hivyo akateremka hadi kwenye mlima wa miamba na akakaa katika jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hivyo, akamfukuza Daudi katika Jangwa la Maoni.
26 Šaul je sa svojim ljudima išao jednom stranom planine, a David sa svojim ljudima drugom stranom planine. David se silno žurio da umakne Šaulu. Kad je Šaul sa svojim ljudima htio prijeći na drugu stranu da opkoli Davida i njegove ljude i da ih pohvata,
Sauli akaenda akawa upande mmoja wa mlima, na Daudi na watu wake walikuwa wakienda upande mwingine wa mlima. Daudi kwa haraka akatoweka akae mbali na Sauli. Kwa sababu Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake wawakamate,
27 dođe glasnik Šaulu s porukom: “Dođi brže, Filistejci provališe u zemlju!”
mjumbe mmoja akaja kwa Sauli na kusema, “Njoo, harakisha maana Wafilisti wamepanga uvamizi juu ya nchi.”
28 Tada Šaul odusta od potjere za Davidom i okrenu se protiv Filistejaca. Zato se prozvalo ono mjesto “Klanac razlaza”.
Kwa hiyo Sauli akarudi asimfuatie Daudi na akaenda kupambana na Wafilisti. Kwa hiyo sehemu ile iliitwa Mwamba wa Maficho.
29 David se odande uspe i nastani u engadskim gorskim skloništima.
Daudi akapanda kutoka huko na kukaa katika ngome ya Engedi.