< 1 Samuelova 12 >

1 Tada Samuel reče svemu Izraelu: “Evo, ispunio sam vašu želju u svemu što ste od mene tražili i postavih kralja nad vama.
Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
2 I od sada će kralj ići pred vama. A ja sam ostario i osijedio i moji sinovi eto su među vama. Ja sam išao pred vama od svoje mladosti pa do današnjega dana.
Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
3 Evo me! Posvjedočite protiv mene pred Jahvom i pred njegovim pomazanikom: kome sam oteo vola i kome sam oteo magarca? Koga sam prevario? Koga sam tlačio? Od koga sam primio mito da bih zažmirio na jedno oko? Ja ću vam sve natrag vratiti.”
Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
4 A oni odgovoriše: “Nisi nas prevario, nisi nas tlačio, nisi ni od koga primio ništa.”
Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
5 Još im reče: “Svjedok je Jahve protiv vas i svjedok je njegov pomazanik u ovaj dan da niste našli ništa u mojoj ruci.” A oni odgovoriše: “Tako je!”
Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
6 Tada Samuel reče narodu: “Jest, svjedok je Jahve koji je postavio Mojsija i Arona i koji je izveo vaše oce iz Egipta.
Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
7 Stanite sada ovamo da probesjedim s vama pred Jahvom i da vas podsjetim na sva velika djela koja je učinio Jahve vama i vašim ocima.
Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
8 Kad je Jakov došao u Egipat, Egipćani su ih pritisnuli, a vaši su oci vapili Jahvi za pomoć. I Jahve posla Mojsija i Arona, koji izvedoše oce vaše iz Egipta i naseliše ih na ovome mjestu.
“Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
9 Ali oni zaboraviše Jahvu, Boga svoga, i on ih predade u ruke Siseri, vojvodi hasorske vojske, i u ruke Filistejaca, i u ruke moapskome kralju, koji su vojevali na njih.
“Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
10 I opet su vapili Jahvi za pomoć govoreći: 'Zgriješili smo jer smo ostavili Jahvu i uzeli služiti baalima i aštartama; izbavi nas sada iz ruku naših neprijatelja pa ćemo ti služiti!'
Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
11 I Jahve posla Jerubaala i Baraka, Jiftaha i Samuela te vas izbavi iz ruku vaših neprijatelja unaokolo, tako da ste mogli živjeti bez straha.
Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
12 Ali kad vidjeste Nahaša, kralja amonskoga, kako ide na vas, rekoste mi: 'Ne, nego kralj neka vlada nad nama!' Pa ipak je vaš kralj Jahve, vaš Bog!
“Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
13 I eto vam sada kralja koga ste izabrali! Eto, Jahve je postavio kralja nad vama.
Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
14 Ako se budete bojali Jahve i njemu budete služili, ako budete slušali njegov glas i ne budete se protivili njegovim zapovijedima, slijedit ćete Jahvu, Boga svoga, vi i kralj koji kraljuje nad vama.
Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
15 Ako li ne budete slušali Jahvina glasa, ako se budete protivili njegovim zapovijedima, tada će se ruka Jahvina spustiti na vas i na vašega kralja da vas uništi.
Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
16 Sada još jednom pristupite i vidite veliki znak koji će Jahve učiniti pred vašim očima.
“Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
17 Nije li sada pšenična žetva? Ali ja ću zazvati Jahvu i on će poslati gromove i kišu. I jasno ćete razabrati kako je veliko zlo koje ste učinili pred Jahvom tražeći sebi kralja.”
Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
18 Tada Samuel zazva Jahvu i Jahve posla gromove i kišu u onaj dan i sav se narod vrlo poboja Jahve i Samuela.
Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
19 I sav narod reče Samuelu: “Moli se Jahvi, svome Bogu, za svoje sluge da ne pomremo, jer smo svim svojim grijesima dodali zlo tražeći sebi kralja.”
Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
20 Ali Samuel reče narodu: “Ne bojte se! Vi ste, doduše, učinili sve ovo zlo, ali sada ne ostavljajte više Jahvu, nego služite Jahvi svim svojim srcem.
Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
21 Ne priklanjajte se više ništavim idolima koji vam ništa ne koriste, ništa vam ne pomažu jer su samo ništavila.
Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
22 A Jahve neće odbaciti svoga naroda, radi velikog imena svoga, jer se Jahve udostojao da vas učini svojim narodom.
Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
23 A od mene neka je daleko da zgriješim Jahvi prestajući moliti za vas i upućivati vas na dobar i pošten put.
Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
24 Samo se bojte Jahve i njemu iskreno služite svim svojim srcem; jer, pogledajte kako se velikim očitovao među vama.
Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
25 Ako li budete činili zlo, propast ćete vi i vaš kralj.”
Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”

< 1 Samuelova 12 >