< 1 Petrova 4 >
1 Dakle, budući da je Krist trpio u tijelu, i vi se oboružajte istim mišljenjem - jer tko trpi u tijelu okanio se grijeha -
Maadamu Kristo aliteseka kimwili, nanyi pia mnapaswa kujiimarisha kwa nia hiyo yake; maana mtu akisha teseka kimwili hahusiki tena na dhambi.
2 da vrijeme što vam u tijelu još preostaje proživite ne više po ljudskim požudama nego po Božjoj volji.
Tangu sasa, basi, maisha yaliowabakia kuishi hapa duniani yanapaswa kuongozwa na matakwa ya Mungu, si na tamaa za kibinadamu.
3 Dosta je uistinu što ste u prošlom vremenu vršili volju pogana, hodeći u razvratnostima, požudama, pijančevanjima, pijankama, opijanjima i bezakoničkim idolopoklonstvima.
Wakati uliopita mlikuwa na muda mrefu wa kufanya mambo wanayofanya watu wasiomjua Mungu. Mliishi maisha ya anasa, ubinafsi, ulevi, ugomvi, kunywa mno na ya ibada haramu za sanamu.
4 Stoga se čude što se ne slijevate u tu istu rijeku raskalašenosti te proklinju.
Sasa, watu hao wasiomjua Mungu wanashangaa wanapoona kwamba hamwandamani nao tena katika hali ya kuishi vibaya, na hivyo wanawatukaneni.
5 Polagat će oni račun Onomu tko je već spreman suditi žive i mrtve.
Lakini watapaswa kutoa hoja juu ya jambo hilo mbele yake Mungu aliye tayari kuwahukumu wazima na wafu!
6 Zato je i mrtvima naviješteno evanđelje da osuđeni doduše po ljudsku, u tijelu, žive po Božju - u duhu.
Kwa sababu hiyo, hao waliokufa ambao walikuwa wamehukumiwa katika maisha yao ya kimwili kama anavyohukumiwa kila mmoja, walihubiriwa Habari Njema kusudi katika maisha yao ya kiroho waishi kama aishivyo Mungu.
7 Približio se svršetak svega! Osvijestite se i otrijeznite za molitvu!
Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na nidhamu, ili mweze kusali.
8 Prije svega imajte žarku ljubav jedni prema drugima jer ljubav pokriva mnoštvo grijeha!
Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi.
9 Gostoljubivo primajte jedni druge bez mrmljanja!
Muwe na ukarimu ninyi kwa ninyi bila kunung'unika.
10 Jedni druge poslužujte - svatko po primljenom daru - kao dobri upravitelji različitih Božjih milosti!
Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine, kama vile uwakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu.
11 Govori li tko? Neka govori kao riječi Božje! Poslužuje li tko? Neka poslužuje kao snagom koju daje Bog da se u svemu slavi Bog po Isusu Kristu, komu slava i vlast u vijeke vijekova! Amen. (aiōn )
Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumika anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina. (aiōn )
12 Ljubljeni! Ne čudite se požaru što bukti među vama da vas iskuša, kao da vam se događa štogod neobično!
Wapenzi wangu, msishangae kuhusu majaribio makali mnayopata kana kwamba mnapatwa na kitu kisicho cha kawaida.
13 Naprotiv, radujte se kao zajedničari Kristovih patnja da i o Objavljenju njegove slave mognete radosno klicati.
Ila furahini kwamba mnashiriki mateso ya Kristo ili mweze kuwa na furaha tele wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
14 Pogrđuju li vas zbog imena Kristova, blago vama, jer Duh Slave, Duh Božji u vama počiva.
Heri yenu ikiwa mnatukanwa kwa sababu ya jina la Kristo; jambo hilo lamaanisha kwamba Roho mtukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yetu.
15 Tek neka nitko od vas ne trpi kao ubojica, ili kradljivac, ili zločinac, ili makar i kao nametljivac;
Asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu ambaye anapaswa kuteseka kwa sababu ni muuaji, mwizi, mhalifu au mwovu.
16 ako li kao kršćanin, neka se ne stidi, nego slavi Boga zbog tog imena.
Lakini kama mtu akiteseka kwa sababu ni Mkristo, basi asione aibu, bali amtukuze Mungu, kwa sababu mtu huyo anaitwa kwa jina la Kristo.
17 Ta vrijeme je da započne Sud - od doma Božjega. No ako već od vas započinje, kakav je onda svršetak onih što nisu poslušni Božjem evanđelju?
Wakati wa hukumu umefika, na hukumu hiyo inaanza na watu wake Mungu mwenyewe. Ikiwa hukumu hiyo inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasioamini Habari Njema ya Mungu?
18 I ako se pravednik jedva spasava, opak i grešnik gdje da se pojavi?
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Ni vigumu kwa watu waadilifu kuokolewa; itakuwaje basi kwa wasiomcha Mungu na wenye dhambi?”
19 Stoga oni koji po volji Božjoj trpe, neka dobrim djelima povjere duše svoje vjernom Stvoritelju.
Kwa hiyo, wale wanaoteseka kufuatana na matakwa ya Mungu, wanapaswa, kwa matendo yao mema, kujiweka chini ya Muumba wao ambaye ni wa kuaminika kabisa.