< 1 Kraljevima 1 >
1 Kralj David bijaše ostario i odmakao u godinama; premda su ga pokrivali mnogim pokrivačima, nije se mogao ugrijati.
Mfalme Daudi alipokuwa mzee sana, walimfunika kwa nguo, lakini hakupata joto.
2 Tada mu rekoše njegove sluge: “Trebalo bi potražiti za gospodara mladu djevojku koja bi dvorila kralja i služila mu: kad bude spavala na njegovu krilu, to će ugrijati kralja gospodara.”
Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Na tutafute msichana bikra kwa ajili ya mfalme bwana wetu. Ili amtumikie na kumtunza. Naye atalala kwenye mikono yake ili bwana mfalme wetu apate joto.
3 Potražiše, dakle, lijepu djevojku po svoj zemlji izraelskoj; i nađoše Abišagu Šunamku te je dovedoše kralju.
Kwa hiyo wakatafuta msichana mrembo katika mipaka yote ya Israeli. Wakampata Abishagi Mshunami wakamlte kwa mfalme.
4 Djevojka je bila izvanredno lijepa; njegovala je kralja i služila mu, ali je on ne upozna.
Yule msichana alikuwa mrembo sana. Naye akamtumikia mfalme na kumtunza, Lakini mfalme hakumjua.
5 Uto se Adonija, sin Hagitin, pooholi i pomisli: “Ja ću biti kralj!” Zato nabavi sebi kola i konjanika i pedeset ljudi koji su išli pred njim.
Wakati huo, Adoniya mwana wa Hagithi alijiinua akisema, “Nitakuwa mfalme.” Kwa hiyo akajiandalia magari na wapanda farasi hamsini ili wapige mbio mbele yake.
6 Njegov ga otac za svoga života nikad nije ukorio niti ga kad upitao: “Zašto tako činiš?” Bio je, osim toga, stasit i lijep, a mati ga rodila poslije Abšaloma.
Baba yake alikuwa hajawahi kumsumbua, kwa kusema, “kwa nini umefanya hili na lile?” Adoniya allikuwa mwanamume mzuri sana aliyezaliwa baada ya Absalomu.
7 On se dogovarao s Joabom, sinom Sarvijinim, i sa svećenikom Ebjatarom, pa se obojica priključiše Adoniji.
Akashauriana na Yoabu mwana wa Seruya na Abiathari kuhani. Wakamfuata Adoniya wakamsaidia.
8 Ali svećenik Sadok i Jojadin sin Benaja, prorok Natan, Šimej i Rei i junaci Davidovi ne pristadoše uz Adoniju.
Lakini Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Nathani, Shimei, Rei, na watu mashujaa wa Daudi hawakumfuata Adoniya.
9 Jednom nakla Adonija ovaca, volova i tovljene teladi za žrtvu kod Zoheledskog kamena, blizu izvora Rogela, te pozva svu svoju braću, sinove kraljeve, i sve Judejce u kraljevoj službi;
Adoniya akataoa dhabihu za Kondoo, na ndama walionona kwenye jiwe la Sohelethi, ambalo liko karibu na Eni Rogeli. Akawakaribisha ndugu zake wote, watoto wa mfalme, wanaume wote wa Yuda, na watumishi wa mfalme.
10 ali ne pozva proroka Natana, ni Benaje, ni ostalih junaka, a ni svoga brata Salomona.
Lakini hakumkaribisha nabii Nathan, Benaya, wanaume mashujaa, au ndugu yake Sulemani.
11 Tada reče Natan Bat-Šebi, majci Salomonovoj: “Zar nisi čula da je Adonija, sin Hagitin, postao kraljem, a da David, naš gospodar, o tome i ne zna?
Kisha Nathani akamwambia Bethisheba mama wa Sulemani, akaisema, “Je, haujasikia kuwa Adoniya mwana wa Hagathi amekuwa mfalme, na Daudi bwana wetu halijui hilo?
12 Dođi da te savjetujem kako bi mogla spasiti život svoj i svoga sina Salomona.
Kwa hiyo sasa nakupa ushauri, ili kwamba uweze kuokoa maisha yako na maisha ya mwanao Suleimani.
13 Hajde, otiđi kralju Davidu i reci mu: 'Zar se nisi ti, gospodaru moj kralju, zakleo svojoj službenici govoreći: Tvoj sin Salomon kraljevat će poslije mene, i on će sjediti na mome prijestolju! Kako sada Adonija posta kraljem?'
Nenda kwa mfalme Daudi; ukamwambie, 'Bwana wangu mfalme, Je, haukumwapia mtumishi wako, ukisema, “Hakika Sulemani mwanao atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?” Kwa nini basi Adoniya anatawala?'
14 I dok ti budeš ondje i razgovorala se s kraljem, doći ću ja za tobom i potvrditi tvoje riječi.”
Wakati ukiwa pale ukiongea na mfalme, Nitaingia baada yako na kuthibitisha hayo.
15 Bat-Šeba ode kralju u odaje - a on je bio vrlo star i Abišaga Šunamka služila mu.
Kwa hiyo Bathisheba akaingia chumbani kwa mfalme. Wakati huo mfalme alikuwa mzee sana, na Abishagi Mshunami alikuwa akimtunza mfalme.
16 Pokloni mu se Bat-Šeba i pade ničice pred kraljem, a kralj upita: “Što želiš?”
Bathisheba akaiinama kifudifudi mbele ya mfalme. Na kisha mfalme akasema, “Una haja gani?”
17 Ona mu odgovori: “Gospodaru, ti si se zakleo službenici svojoj Jahvom, Bogom svojim: 'Tvoj sin Salomon kraljevat će poslije mene, on će sjesti na moje prijestolje.'
Naye akamwambia, “Bwana wangu, ulimwapia mtumishi wako kwa jina la BWANA, Mungu wako, ukisema, 'Hakika Sulemani mwanao atatawala, baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha enzi.'
18 A sada je, evo, Adonija postao kraljem, a ti, kralju, gospodaru moj, ništa o tome i ne znaš!
Sasa, tazama, Adoniya ni mfalme, na bwana wangu mfalme hajui jambo hili.
19 Naklao je on mnogo volova, tovljene teladi i ovaca za žrtvu i pozvao je sve sinove kraljeve, svećenika Ebjatara i vojskovođu Joaba, ali slugu tvoga Salomona nije pozvao.
Ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, Abiathari kuhani, na Yoabu jemedari wa jeshi, lakini hajamkaribisha Sulemani mtumishi wako.
20 U tebe su sada, gospodaru moj i kralju, uprte oči svega Izraela da mu ti objaviš tko će te naslijediti na tvome prijestolju, kralju, gospodaru moj.
Mfalme bwana wangu, macho yote ya Israeli yako kwako, yakisubiri usemi wako juu ya nani atakayeti kwenye kiti cha enzi baada yako, bwana wangu.
21 Inače, čim počine kralj, gospodar moj, kraj svojih otaca, ja i moj sin Salomon bit ćemo krivci.”
Vinginevyo itatokea, wakati bwana wangu atakapolala na baba zake, kwamba Mimi na mwanangu Sulemani kuhesabiwa wahaini.”
22 Dok je ona još govorila s kraljem, dođe prorok Natan.
Wakati alipokuwa akiendelea na mfalme, nabii Nathani aliingia.
23 Javiše kralju: “Ovdje je prorok Natan.” On uđe kralju i pade ničice pred njim.
Watumshi wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa,” Naye alipoingia mbele ya mfalme, akalala kifudifudi mbele ya mfalme na uso wake ukielekea chini.
24 Natan reče: “Gospodaru moj i kralju, jesi li ti odredio: 'Adonija će kraljevati poslije mene i sjedit će na mome prijestolju?'
Nathani akamwambia, “Mfalme bwana wangu, Je, umesema, Adoniya atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?
25 Jer evo danas je sišao i naklao volova, ugojene teladi i ovaca za žrtvu i pozvao je sve sinove kraljeve, vojskovođe i svećenika Ebjatara; eno ih gdje jedu i piju s njim i kliču: 'Živio kralj Adonija!'
kwani leo ameshuka na ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, jemedari wa jeshi, na Abiatahari kuhani. Nao wanakuka na kunywa mbele zake, na kusema, 'Mfalme Adoniya na aishi milele!'
26 Ali mene, tvoga slugu, svećenika Sadoka, a ni Benaju, sina Jojadina, ni tvoga slugu Salomona nije pozvao.
Lakini mimi, mtumishi wako, Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, na mtumishi wako Suleimani, hajatukaribisha.
27 Zar se to dogodilo s voljom gospodara moga kralja, a da nisi obavijestio svoga vjernog sluge tko će biti nasljednik na prijestolju gospodara moga kralja?”
Je, bwana wangu mfalme amefanya haya pasipo kutuambia sisi, watumishi wako, ni nani atakayeketi kwenye kiti cha enzi baada yake?”
28 Tada progovori David i reče: “Pozovite mi Bat-Šebu!” Ona dođe kralju i stupi preda nj.
Ndipo mfalme Daudi lipojibu na kusema, “Mwiteni Bathisheba arudi.” Naye akaja akasimama mbele ya mfalme.
29 Kralj se tada zakle: “Tako mi Jahve živoga koji me izbavio iz svih nevolja!
Mfalme akafanya kiapo akasema, “Kama BWANA aishivyo, ambaye ameniokoa toka tabu zote,
30 Danas ću ti ispuniti kako sam ti se zakleo Jahvom, Bogom Izraelovim: tvoj će sin Salomon kraljevati poslije mene, on će sjediti na mome prijestolju!”
kama nilivyokuapia kwa BWANA, Mungu wa Israeli, nikisema, 'Sulemani mwanao atatawala baada yangu, naye ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha enzi, mahali pangu,' Nitafanya hivi leo.”
31 Nato se nakloni Bat-Šeba licem do zemlje, pokloni se pred kraljem i reče: “Neka vječno živi gospodar moj kralj David!”
Kisha Bathisheba akalala kifudifudi na sura yake ikielekea chini mbele ya mfalme akasema, “Bwana wangu mfalme Daudi n a aishi milele!”
32 A kralj David reče: “Pozovite mi svećenika Sadoka, proroka Natana i Benaju, sina Jojadina.” I dođoše oni pred kralja,
Mflme Daudi akasema, “Niitieni Sadoki kuhani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Nao wakaja mbele ya mfalme.
33 a on im reče: “Uzmite sluge svoga gospodara sa sobom, posadite moga sina Salomona na moju mazgu i odvedite ga do Gihona.
Mfalme akawaambia, “Uwachukue watumishi wangu, bwana wako, na umfanye Sulemani mwanangu apande juu ya nyumba yangu mimi na mkamtelemshe mpaka chini Gihoni.
34 Ondje neka ga svećenik Sadok i prorok Natan pomažu za kralja nad Izraelom. Zatrubite tada i obznanite: 'Živio kralj Salomon!'
Na Sadoki kuhani na nabii Nathani wamtawaze awe mfalme wa Israeli na tarumbeta zipigwe, 'Mfalme Suleimani na uishi milele!'
35 Zatim se uspnite amo s njim i neka uđe i sjedne na moje prijestolje i neka kraljuje mjesto mene, jer moja je volja: on neka bude glava nad Izraelom i nad Judom.”
Kisha njoni mkiwa nyuma yake, naye atakuja na kukaa kwenye kiti changu cha enzi; kwani yeye ndiye atakayekuwa mfalme mahali pangu. Nimemchagua yeye kuwa mtawala wa Israeli na Yuda.”
36 Benaja, sin Jojadin, reče kralju: “Amen - tako neka bude! To je i riječ Jahve, Gospodara kraljeva!
Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, akasema, “Na iwe hivyo! Na BWANA, Mungu wa mfalme bwana wangu, alithibitishe hilo.
37 Kao što je Jahve bio s mojim gospodarem kraljem, tako neka bude i sa Salomonom! Neka uzvisi prijestolje njegovo još više nego prijestolje kralja Davida, gospodara moga!”
Kama vile BWANA alivyokuwa na mfalme bwana wangu na awe na Sulemani hivyo hivyo, na kuifanya enzi yake kuwa kubwa kuliko zaidi ya enzi ya bwana wangu Daudi.”
38 Svećenik Sadok, prorok Natan, Jojadin sin Benaja, Kerećani i Pelećani siđoše i posadiše Salomona na kraljevu mazgu i odvedoše ga na Gihon.
Kwa hiyo Sadoki kuhani, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi na Wapelethi wakamfanya Sulemani akapanda juu ya nyumba ya mfalme Daudi; wakamleta Gihoni.
39 Svećenik Sadok donese iz Šatora rog s uljem i pomaza Salomona. Tada odjeknuše trube i sav narod povika: “Živio kralj Salomon!”
Naye Sadoki kuhani akachukua pembe lenye mafuta hemani akamtia mafuta Sulemani kisha wakapiga tarumbeta, na watu wote wakasema, 'Mfalme Sulemani na aishi milele!'
40 I sav narod pođe za njim gore i sviraše puk u svirale i klicaše tako da se sva zemlja tresla.
Kisha watu wote wakamfuata, na watu wakapiga zomari wakafurahi furaha kubwa mno, kiasi kwamba dunia ikatetemeka kwa sauti zao.
41 Čuo to Adonija i svi njegovi uzvanici. Baš su bili pri kraju gozbe. I Joab je čuo trube pa upita: “Čemu ta buka u gradu?”
Kisha Adoniya na wageni wake waliokuwa pamoja naye wakasikia hayo walipomaliza kula. Yoabu alipozisikia sauti za panda, akasema, “Kwa nini jiji lilko katika hali ya taharuki?”
42 Dok je on još govorio, stiže Jonatan, sin svećenika Ebjatara, i Adonija mu reče: “Ti si valjan čovjek, zacijelo nosiš dobru vijest!”
Wakati alipokuwa akiongea, Yonatahani mwana wa Abiathari kuhani alifika. Adoniya akamwambia, “Karibu, 'kwa kuwa wewe wastahili kutuletea habari.”
43 Jonatan odgovori: “Jest, naš gospodar, kralj David, učinio je Salomona kraljem!
Naye Yonathani akamjibu Adoniya, “Mfalme bwana wetu Daudi amemfanya Sulemani kuwa mfalme.
44 Kralj je poslao s njim svećenika Sadoka, proroka Natana i Jojadina sina Benaju, i Kerećane i Pelećane. Oni ga posadiše na kraljevu mazgu,
Na mfalme amemtuma pamoja naye Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi pamoja na Wapelethi. Wamempandisha Sulemani juu ya nyumba ya mfalme.
45 i svećenik Sadok i prorok Natan pomazaše ga na Gihonu za kralja. Zatim su sišli radosno kličući, i sav je grad uzavreo; to je buka koju ste čuli.
Sadoki kuhani na nabii Nathani wamemtawaza kuwa mfalme kule Gihoni, na wametokea huko wakifurahi, ndiyo maana jiji liko katika taharuki. Na hizi ndizo sauti ulizosikia.
46 Još više: Salomon je već sjeo na kraljevsko prijestolje
Pia, Sulemani ameketi kwenye kiti cha enzi cha ufalme.
47 i došle su sluge kraljeve čestitati našem gospodaru kralju Davidu govoreći: 'Neka Bog tvoj proslavi ime Salomonovo više od imena tvoga i prijestolje njegovo uzvisi više od tvoga.' Kralj se tada poklonio na svojoj postelji
Zaidi ya yote, watumishi wa mfalme walikuja kumbariki mfalme bwana wetu Daudi, wakisema, 'Mungu wako na alifanye jina la Sulemani kuwa zuri kuliko jina lako, na kuifanya enzi yako kuwa kubwa kuliko yako.' na mfalme akasujudu mwenyewe kitandani.
48 i ovako rekao: 'Neka je blagoslovljen Jahve, Bog Izraelov, koji mi dade danas da mogu vidjeti svojim očima jednoga od mojih kako sjedi na mome prijestolju.'”
Mfalme pia alisema, 'Abarikiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amempa mtu kuketi kwenye enzi yangu siku hii ya leo, na kwamba macho yangu yamejionea hilo.'”
49 Svi uzvanici Adonijini, uplašeni, ustadoše od stola i raziđoše se svaki svojim putem.
Ndipo wageni wote wa Adoniya walipoogopa sana. Wakasimama na kila mtu akaenda njia yake.
50 Adonija pak, u strahu od Salomona, usta i ode te se uhvati za rogove žrtvenika.
Pia Adoniya alimwaogopa Sulemani na akasimama, na akaondoka, akachukua pembe la madhabahuni.
51 Javiše Salomonu: “Gle, Adonija se uplašio kralja Salomona i eno se drži za rogove žrtvenika govoreći: 'Neka mi se danas kralj Salomon zakune da neće sluge svoga mačem pogubiti.'”
Kisha Sulemani akaambiwa hilo, wakasema, “Tazama, Adoniya amemwogopa mfalme Sulemani, kwa kuwa ameshikilia pembe la madhabahuni, akisema, 'Mfalme Sulemani na aniapie kwanza kuwa hatamwua mtumishi wake kwa upanga.'”
52 Salomon reče nato: “Ako se pokaže poštenim čovjekom, neće mu ni vlas s glave pasti na zemlju; a nađe li se u zlu, poginut će.”
Sulemani akasema, “Kama atajionyesha kuwa ni mtu wa kweli, hakuna hata unywele mmoja utakaoanguka duniani, bali kama uovu utaonekana kwake, atakufa.”
53 Tada zapovjedi Salomon da ga odmaknu od žrtvenika; on dođe i pade ničice pred Salomonom, koji mu reče: “Pođi svome domu!”
Kwa hiyo mfalme Sulemani akatuma watu, waliomleta Adoniya kutoka madhabahuni. Naye akaja akapiga magoti kwa Sulemani, na Sulemani akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”