< 1 Ljetopisa 6 >

1 Levijevi su sinovi bili Geršom, Kehat i Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
2 Kehatovi sinovi: Amram, Jishar, Hebron i Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
3 Amramovi sinovi: Aron, Mojsije i Mirjama. Aronovi sinovi: Nabad i Abihu, Eleazar i Itamar.
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
4 Eleazar rodi Pinhasa, Pinhas rodi Abišuu;
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
5 Abišua rodi Bukija, Buki rodi Uziju;
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
6 Uzija rodi Zerahju; Zerahja rodi Merajota.
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
7 Merajot rodi Amarju; Amarja rodi Ahituba;
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
8 Ahitub rodi Sadoka; Sadok rodi Ahimaasa;
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
9 Ahimaas rodi Azarju, Azarja rodi Johanana;
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
10 Johanan rodi Azarju, koji je bio svećenik u Hramu što ga je sagradio Salomon u Jeruzalemu.
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
11 Azarja rodi Amarju; Amarja rodi Ahituba;
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
12 Ahitub rodi Sadoka, Sadok rodi Šaluma;
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
13 Šalum rodi Hilkiju, Hilkija rodi Azarju;
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
14 Azarja rodi Seraju; Seraja rodi Josadaka.
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
15 Josadak je otišao kad je Jahve odveo u sužanjstvo Judu i Jeruzalem Nabukodonozorovom rukom.
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
16 Levijevi su sinovi bili Geršom, Kehat i Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
17 Evo imena Geršomovih sinova: Libni i Šimej.
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
18 Kehatovi su sinovi bili: Amram, Jishar, Hebron i Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
19 Merarijevi sinovi: Mahli i Muši. Ovo su rodovi Levijevaca po svojim ocima.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
20 Od Geršoma: sin mu Libni, njegov sin Jahat, njegov sin Zima,
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
21 njegov sin Joah, njegov sin Ido, njegov sin Zerah, njegov sin Jeatraj.
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
22 Kehatovi sinovi: sin mu Aminadab, njegov sin Korah, njegov sin Asir,
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
23 njegov sin Elkana, njegov sin Ebjasaf, njegov sin Asir;
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
24 njegov sin Tahat, njegov sin Uriel, njegov sin Uzija, njegov sin Šaul.
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
25 Elkanini sinovi: Amasaj i Ahimot;
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
26 njegov sin Elkana, njegov sin Sufaj, njegov sin Nahat;
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
27 njegov sin Eliab, njegov sin Jeroham, njegov sin Elkana. Elkanini sinovi:
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
28 Samuel, njegov prvenac, drugi Abija.
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
29 Merarijevi sinovi: Mahli, njegov sin Libni, njegov sin Šimej, njegov sin Uza,
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
30 njegov sin Šima, njegov sin Hagija, njegov sin Asaja.
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
31 Ovo su oni koje je postavio David da se brinu za pjevanje u Domu Jahvinu kad je Kovčeg ondje našao svoje počivalište;
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
32 oni koji su služili pred Prebivalištem, Šatorom sastanka, pjevajući, dok nije Salomon sagradio Dom Jahvin u Jeruzalemu i koji su obavljali službu po propisanom redoslijedu.
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
33 Evo onih što su obavljali službu i njihovih sinova: od Kehatovih sinova: pjevač Heman, sin Joela, sina Samuela,
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
34 sina Elkane, sina Jerohama, sina Eliela, sina Toaha,
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
35 sina Sifa, sina Elkane, sina Mahata, sina Amasaja,
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
36 sina Elkane, sina Joela, sina Azarje, sina Sefanije,
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
37 sina Tahata, sina Asira, sina Abjasafa, sina Koraha,
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
38 sina Jishara, sina Kehata, sina Levija, sina Izraelova.
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
39 Brat mu Asaf stajao je s desne strane; Asaf je bio sin Berekje, sina Šime,
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
40 sina Mihaela, sina Baaseja, sina Malkije,
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
41 sina Etnija, sina Zeraha, sina Adaje,
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
42 sina Etana, sina Zime, sina Šimeja,
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
43 sina Jahata, sina Geršoma, sina Levijeva.
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44 Merarijevi sinovi, njihova braća, stajala su mu s lijeve strane: Etan, sin Kušija, sina Abdija, sina Maluka,
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
45 sina Hašabje, sina Amasje, sina Hilkije,
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
46 sina Amsija, sina Banija, sina Šomera,
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
47 sina Mahlija, sina Mušija, sina Merarija, sina Levijeva.
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48 Njihova braća leviti bili su postavljeni za svu službu u svetom Prebivalištu, u Domu Božjem.
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
49 Aron i njegovi sinovi prinosili su kad na žrtveniku za paljenice i na kadionom žrtveniku, obavljajući sav posao u Svetinji nad svetinjama i izvršujući obred pomirenja nad Izraelom, prema svemu što je zapovjedio Božji sluga Mojsije.
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
50 Ovo su Aronovi sinovi: sin mu Eleazar, njegov sin Pinhas, njegov sin Abišua,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
51 njegov sin Buki, njegov sin Uzi, njegov sin Zerahja,
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
52 njegov sin Merajot, njegov sin Amarja, njegov sin Ahitub,
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
53 njegov sin Sadok, njegov sin Ahimaas.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
54 Ovo su im boravišta po naseljima u njihovu području: Aronovim sinovima od Kehatove obitelji - jer na njih je pao ždrijeb -
Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
55 dali su Hebron u judejskoj zemlji s pašnjacima oko njega.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
56 Gradsko polje i njegova sela dali su Jefuneovu sinu Kalebu.
Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Dali su, dakle, Aronovim sinovima gradove-utočišta Hebron i Libnu s pašnjacima, Jatir i Eštemou s pašnjacima,
Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
58 Hilez s pašnjacima, Debir s pašnjacima,
Hileni, Debiri,
59 Ašan s pašnjacima i Bet Šemeš s pašnjacima.
Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
60 Od Benjaminova plemena: Gebu s pašnjacima, Alemet s pašnjacima i Anatot s pašnjacima; dakle trinaest gradova po njihovim rodovima.
Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
61 Ostalim Kehatovim sinovima prema plemenskim rodovima pripalo je ždrijebom deset gradova od polovine Manašeova plemena.
Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
62 Geršomovim sinovima po njihovim rodovima pripalo je od Jisakarova plemena, od Ašerova plemena, od Naftalijeva plemena i od Manašeova plemena u Bašanu trinaest gradova.
Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Merarijevim sinovima po njihovim rodovima pripalo je ždrijebom od Rubenova plemena, od Gadova plemena i od Zebulunova plemena dvanaest gradova.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
64 Tako su Izraelovi sinovi dali levitima te gradove s pašnjacima.
Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
65 Dali su ždrijebom od plemena Judinih sinova, od plemena Šimunovih sinova i od plemena Benjaminovih sinova te gradove koje su spomenuli poimence.
Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
66 Onima koji su bili od rodova Kehatovih sinova te dobili ždrijebom gradove od Efrajimova plemena
Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
67 dali su kao gradove-utočišta Šekem s pašnjacima u Efrajimovoj gori i Gezer s pašnjacima,
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
68 Jokmeam s pašnjacima, Bet Horon s pašnjacima,
Yokmeamu, Beth-Horoni,
69 Ajalon s pašnjacima i Gat-Rimon s pašnjacima.
Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
70 Od polovine Manašeova plemena dali su rodovima ostalih Kehatovih sinova: Aner s pašnjacima i Bileam s pašnjacima.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
71 Geršomovim sinovima dali su od rodova polovine Manašeova plemena Golan u Bašanu s pašnjacima i Aštarot s pašnjacima.
Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
72 Od Jisakarova plemena Kedeš s pašnjacima, Dobrat s pašnjacima,
Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
73 Ramot s pašnjacima i Anem s pašnjacima.
Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
74 Od Ašerova plemena Mašal s pašnjacima, Abdon s pašnjacima,
Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
75 Hukok s pašnjacima i Rehob s pašnjacima.
Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
76 Od Naftalijeva plemena Kedeš u Galileji s pašnjacima, Hamon s pašnjacima i Kirjatajim s pašnjacima.
Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
77 Ostalim Merarijevim sinovima dali su od Zebulunova plemena Rimon s pašnjacima i Tabor s pašnjacima.
Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
78 S onu stranu Jordana, prema Jerihonu, na istočnoj strani Jordana, dali su im od Rubenova plemena Beser u pustinji s pašnjacima, Jahsu s pašnjacima,
Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
79 Kedemot s pašnjacima i Mefaat s pašnjacima.
Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
80 Od Gadova plemena Ramot u Gileadu s pašnjacima, Mahanajim s pašnjacima,
Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
81 Hešbon s pašnjacima i Jazer s pašnjacima.
Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.

< 1 Ljetopisa 6 >