< 1 Ljetopisa 28 >

1 David sakupi u Jeruzalem sve izraelske knezove, plemenske knezove i poglavare od redova koji su služili kralja, tisućnike, stotnike i nadstojnike nad svim imanjem i blagom kraljevim i blagom njegovih sinova, zajedno s dvoranima i junacima i svim hrabrim vojnicima.
Daudi akawaita maafisa wote wa Israeli wakusanyike huko Yerusalemu: yaani, maafisa walio juu ya makabila, majemadari wa vikosi katika utumishi wa mfalme, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, maafisa wanaosimamia mali zote na mifugo ya mfalme na wanawe, wakiwemo maafisa wa jumba la kifalme, mashujaa na askari wote walio hodari.
2 Ustavši na noge, kralj David reče: “Čujte me, moja braćo i moj narode! Ja sam bio namislio u svom srcu da sagradim dom gdje bi počivao Kovčeg saveza Jahvina i da bude podnožje nogama našega Boga te sam pripravio što treba za gradnju.
Mfalme Daudi akainuka na kusema: “Nisikilizeni ndugu zangu nanyi watu wangu. Nilikuwa na nia ya kujenga nyumba ili iwe mahali pa kukaa Sanduku la Agano la Bwana kwa ajili ya kuwa mahali pa kuwekea miguu ya Mungu wetu, nami nikafanya maandalizi ya kuijenga.
3 Ali mi je Bog rekao: 'Nećeš ti sagraditi Doma mome imenu jer si ratnik i prolijevao si krv.'
Lakini Mungu akaniambia, ‘Wewe hutajenga nyumba kwa Jina langu, kwa sababu wewe umepigana vita na umemwaga damu.’
4 Jahve, Izraelov Bog, izabrao je mene od sveg moga roda da budem kralj nad Izraelom zauvijek; jer je Judu izabrao za kneza, a iz Judina doma dom moga oca; između sinova moga oca bilo mu je drago da mene postavi kraljem nad svim Izraelom.
“Hata hivyo, Bwana, Mungu wa Israeli, alinichagua mimi kutoka jamaa yangu yote niwe mfalme juu ya Israeli milele. Alimchagua Yuda kuwa kiongozi na kutoka nyumba ya Yuda akaichagua jamaa yangu na kutoka wana wa baba yangu ikampendeza kunifanya niwe mfalme juu ya Israeli yote.
5 Tako je između mojih sinova, jer mi je mnogo sinova dao Jahve, izabrao moga sina Salomona da sjedi na prijestolju Jahvina kraljevstva nad Izraelom.
Miongoni mwa wanangu wote, naye Bwana amenipa wengi, amemchagua Solomoni mwanangu ili kukikalia kiti cha enzi cha ufalme wa Bwana juu ya Israeli.
6 I rekao mi je: 'Tvoj sin Salomon sagradit će meni Dom i moja predvorja; jer sam njega izabrao sebi za sina i ja ću mu biti otac.
Aliniambia, ‘Solomoni mwanao ndiye atakayejenga nyumba yangu na nyua zangu, kwa maana nimemchagua yeye kuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake.
7 Utvrdit ću njegovo kraljevstvo zauvijek ako bude postojano vršio moje zapovijedi i moje zakone kao danas.'
Nitaufanya imara ufalme wake milele kama akiendelea kuzishika amri zangu na sheria zangu, kama afanyavyo hivi leo.’
8 Sada, dakle, pred očima sveg Izraela, Jahvina zbora, i pred svojim Bogom, koji nas sluša, velim: držite i tražite sve zapovijedi Jahve, svoga Boga, da biste zadržali u posjedu ovu dobru zemlju i ostavili je u baštinu svojim sinovima nakon sebe dovijeka.
“Hivyo basi ninawaagiza mbele za Israeli yote na kusanyiko hili la Bwana naye Mungu wetu akiwa anasikia: Kuweni na bidii kuzifuata amri za Bwana Mungu wenu, ili mpate kumiliki nchi hii nzuri na kuwaachia wana wenu kuwa urithi milele.
9 A ti, sine moj Salomone, poznaj Boga, svoga oca, i služi mu čitavim srcem i spremnom dušom, jer Jahve ispituje sva srca i zna sve misli i namjere; ako ga budeš tražio, dat će ti se da ga nađeš; ako li ga ostaviš, odbacit će te zauvijek.
“Nawe Solomoni mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa kujitoa kwa moyo wote na kwa nia ya kumkubali, kwa maana Bwana huuchunguza kila moyo na kujua kila kusudi la kila fikira. Ukimtafuta, ataonekana kwako; bali kama ukimwacha, yeye atakukataa milele.
10 Uvidi sada da te Jahve izabrao da gradiš Dom za Svetište, budi junak i radi!”
Angalia basi, kwa maana Bwana amekuchagua wewe ili ujenge Hekalu kuwa mahali patakatifu. Uwe hodari ukafanye kazi hiyo.”
11 Tada David predade sinu Salomonu uzorak trijema, njegovih kuća, riznica, gornjih soba, ćelija i doma Pomirilišta;
Ndipo Daudi akampa Solomoni mwanawe kielelezo kwa ajili ya ukumbi wa Hekalu, nyumba zake, vyumba vyake vya hazina, ghorofa zake, vyumba vyake vya ndani na mahali pa kufanyia upatanisho.
12 uzorak svega što bijaše smislio u duhu za predvorja Jahvina Doma, za sve sobe unaokolo, za riznicu Doma Božjega, za riznicu posvećenih stvari,
Akampa vielelezo vya yote Roho alikuwa ameviweka moyoni mwake kwa ajili ya kumbi za Hekalu la Bwana na vyumba vyote vilivyolizunguka, kwa ajili ya hazina za Hekalu la Mungu na kwa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
13 za svećeničke i levitske redove, za svaki posao u službi oko Doma Jahvina:
Mfalme pia akampa Solomoni maelekezo kwa ajili ya migawanyo ya huduma za makuhani na Walawi, pia kwa ajili ya kazi zote za huduma katika Hekalu la Bwana. Akampa pia maelezo kuhusu vifaa vyote vya kutumika katika huduma ya Hekalu.
14 zlato u šipkama, zlato potrebno za sve zlatno posuđe ove ili one službe; srebro u šipkama potrebno za sve srebrno posuđe, za sve posuđe ove ili one službe;
Akamwagizia uzito wa dhahabu kwa ajili ya vitu vyote vya dhahabu vya kutumika katika huduma mbalimbali, uzito wa fedha kwa ajili ya vitu vyote vya fedha vya kutumika katika huduma mbalimbali.
15 šipke za zlatne svijećnjake sa zlatnim svjetiljkama, prema težini svakoga svijećnjaka i njegovih svjetiljaka, i za srebrne svijećnjake prema težini svakoga svijećnjaka i njegovih svjetiljaka i prema namjeni svakog svijećnjaka;
Uzito wa dhahabu kwa ajili ya vinara vya dhahabu na taa zake, kukiwa na uzito kwa ajili ya kila kinara na taa zake, pamoja na uzito wa fedha kwa ajili ya kila kinara cha fedha na taa zake, kulingana na matumizi ya kila kinara;
16 zlato u šipkama za stolove na kojima će stajati prineseni hljebovi, za svaki stol; srebro za srebrne stolove,
uzito wa dhahabu kwa ajili ya meza ya mikate iliyowekwa wakfu, uzito wa fedha kwa ajili ya meza ya fedha;
17 za viljuške i kotliće, za čaše od čista zlata, za zlatne pehare, zlato u šipkama za svaki pehar; za srebrne pehare, srebro u šipkama za svaki pehar,
uzito wa dhahabu safi kwa ajili ya nyuma, mabakuli ya kunyunyizia na vikombe, masinia; uzito wa dhahabu kwa ajili ya kila bakuli la dhahabu; uzito wa fedha kwa ajili ya kila bakuli la fedha;
18 za kadioni žrtvenik žeženoga zlata u šipkama; za uzorak od kola sa zlatnim kerubinima koji će raširenim krilima zaklanjati Jahvin Kovčeg.
na uzito wa dhahabu safi kwa ajili ya madhabahu ya kufukizia uvumba. Pia alimpa kielelezo kwa ajili ya gari, yaani, wale makerubi wa dhahabu waliokunjua mbawa zao na kuweka kivuli juu ya Sanduku la Agano la Bwana.
19 Sve to u skladu s onim što Jahve napisa vlastitom rukom da bi razjasnio cijelo djelo za koje on pribavi uzorak.
Daudi akasema, “Hii yote, ninayo kwa maandishi kutoka mkononi mwa Bwana ulio juu yangu, naye amenipa ufahamu kwa ajili ya habari zote za kielelezo hiki.”
20 Tada David reče svome sinu Salomonu: “Budi junak, hrabar, i radi! Ne boj se i ne plaši se, jer će Jahve, Bog, moj Bog, biti s tobom! Neće te napustiti niti te ostaviti dok ne svršiš sav posao za službu oko Jahvina Doma.
Daudi pia akamwambia Solomoni mwanawe, “Uwe hodari na moyo mkuu, ukafanye kazi hii. Usiogope wala usifadhaike, kwa maana Bwana aliye Mungu, Mungu wangu yu pamoja nawe. Hatakuacha wala hatakupungukia mpaka kazi hii yote kwa ajili ya utumishi wa Hekalu la Bwana itakapokamilika.
21 Evo svećeničkih i levitskih redova za svaku službu u Božjem Domu; imaš uza se za svaki posao svakovrsnih ljudi, spremnih i vještih svakoj službi, knezovi i sav narod pod tvojim su zapovjedništvom.”
Migawanyo ya makuhani na Walawi iko tayari kwa ajili ya kazi yote katika Hekalu la Mungu, naye kila mtu mwenye moyo wa kupenda mwenye ustadi katika aina yoyote ya ufundi atakusaidia katika kazi yote. Maafisa na watu wote watatii kila agizo lako.”

< 1 Ljetopisa 28 >