< 1 Ljetopisa 27 >

1 Izraelovi sinovi po svome broju. Poglavari porodica, tisućnici, stotnici i nadzornici služili su kralju u svakom poslu. U redovima su dolazili i odlazili od mjeseca do mjeseca, u svim godišnjim mjesecima; svaki je red imao dvadeset i četiri tisuće ljudi.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Nad prvim je redom, prvoga mjeseca, bio Zabdielov sin Jašobam. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće ljudi.
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 Pripadao je Peresovim sinovima i bio zapovjednik svih vojvoda u vojsci prvoga mjeseca.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 Nad redom drugoga mjeseca bio je Ahošanin Dodaj, a predstojnik u njegovu redu bio je Mikelot. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće ljudi.
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 Vojvoda treće vojske, trećega mjeseca, bio je sin svećenika Jojade, poglavar Benaja. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 Taj je Benaja bio junak među tridesetoricom i nad tridesetoricom i u njegovu je redu bio sin mu Amizabad.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 Četvrti, četvrtoga mjeseca, bio je Joabov brat Asahel, a za njim sin mu Zebadja. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 Peti, petoga mjeseca, bio je vojvoda Jizrahanin Šamhut. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 Šesti, šestoga mjeseca, bio je Ikešov sin Ira, Tekoanac. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 Sedmi, sedmoga mjeseca, bio je Pelonjanin Heles od Efrajimovih sinova. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 Osmi, osmoga mjeseca, bio je Hušaćanin Sibkaj, Zarhijevac. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 Deveti, devetoga mjeseca, bio je Anatoćanin Abiezer, Benjaminovac. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 Deseti, desetoga mjeseca, bio je Netofaćanin Mahraj, Zarhijevac. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 Jedanaesti, jedanaestoga mjeseca, bio je Piratonjanin Benaja, Efrajimovac. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 Dvanaesti, dvanaestoga mjeseca, bio je Netofaćanin Heldaj, Otnielovac. U svom je redu imao dvadeset i četiri tisuće.
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 Nad Izraelovim plemenima bili su knezovi: nad Rubenovim Zikrijev sin knez Eliezer; nad Šimunovim Maakin sin Šefatja;
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 nad Levijevim Kemuelov sin Hašabja; nad Aronovim Sadok;
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 nad Judinim Elihu od Davidove braće; nad Jisakarovim Mihaelov sin Omri;
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 nad Zebulunovim Obadjin sin Jišmaja; nad Naftalijevim Azrielov sin Jerimot.
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 Nad Efrajimovim sinovima Azazjin sin Hošea; nad polovinom Manašeova plemena Pedajin sin Joel,
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 nad drugom polovinom Manašeova plemena u Gileadu Zaharijin sin Jido; nad Benjaminom Abnerov sin Jaasiel;
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 nad Danom Jerohamov sin Azarel. To su bili knezovi izraelskih plemena.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 Ali David nije dao izbrojiti onih kojima bijaše dvadeset godina i manje, jer Jahve bijaše rekao da će umnožiti Izraelce kao nebeske zvijezde.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Sarvijin je sin Joab počeo vršiti popis, ali ga nije dovršio. Stoga je Srdžba došla na Izrael i zato taj broj nije bio primljen u brojčani izvještaj Ljetopisa kralja Davida.
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 Nadstojnik nad kraljevim blagom bio je Adielov sin Azmavet, a nadstojnik za blago u zemlji, u gradovima, selima i tvrđavama, bio je Uzijin sin Jonatan.
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 Nadstojnik nad poljskim radnicima koji su obrađivali zemlju bio je Kelubov sin Ezri.
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 Nadstojnik nad vinogradarima Ramaćanin Šimej. Nadstojnik nad vinogradrskim klijetima bio je Šifmejac Zabdi.
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 Nadstojnik nad maslinama i dudovima što su po Šefeli bio je Gederac Hanan; nadstojnik nad skladištima ulja Joaš.
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 Nadstojnik nad govedima što su pasla u Šaronu bio je Šaronac Šitraj. Nadstojnik nad krupnom stokom u dolinama bio je Edlajev sin Šafat.
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 Nadstojnik nad devama Jišmaelac Obil. Nadstojnik nad magaricama Meronoćanin Jehdeja.
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 Nadstojnik nad ovcama i kozama Hagrijac Jaziz. Svi su oni bili nadstojnici nad imanjem kralja Davida.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 Savjetnik je bio Davidov stric Jonatan, mudar čovjek; bio je i književnik; a Hakmonijev sin Jehiel bio je s kraljevim sinovima.
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 Ahitofel je bio kraljev savjetnik, Arkijac Hušaj kraljev prijatelj.
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 Ahitofela su naslijedili Benajin sin Jojada i Ebjatar, kraljev je vojvoda bio Joab.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

< 1 Ljetopisa 27 >