< 詩篇 51 >

1 大衛與拔示巴同室以後,先知拿單來見他;他作這詩,交與伶長。 上帝啊,求你按你的慈愛憐恤我! 按你豐盛的慈悲塗抹我的過犯!
Unirehemu, Mungu, kwa sababu ya uaminifu wa agano lako; kwa ajili ya wingi wa matendo yako ya rehema, uyafute makosa yangu.
2 求你將我的罪孽洗除淨盡, 並潔除我的罪!
Unioshe kabisa uovu wangu na unisafishe dhambi zangu.
3 因為,我知道我的過犯; 我的罪常在我面前。
Kwa maana ninayajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yako siku zote.
4 我向你犯罪,惟獨得罪了你; 在你眼前行了這惡, 以致你責備我的時候顯為公義, 判斷我的時候顯為清正。
Dhidi yako, wewe pekee, nimetenda dhambi na kufanya uovu mbele ya macho yako; uko sawa usemapo; wewe uko sahahi utoapo hukumu.
5 我是在罪孽裏生的, 在我母親懷胎的時候就有了罪。
Tazama, nilizaliwa katika uovu; pindi tu mama yangu aliponibeba mimba, nilikuwa katika dhambi. Tazama, wewe unahitaji uaminifu ndani ya moyo wangu;
6 你所喜愛的是內裏誠實; 你在我隱密處,必使我得智慧。
katika moyo wangu wewe utanifanya niijue hekima.
7 求你用牛膝草潔淨我,我就乾淨; 求你洗滌我,我就比雪更白。
Unisafishe kwa hisopo, nami nitakuwa safi; unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 求你使我得聽歡喜快樂的聲音, 使你所壓傷的骨頭可以踴躍。
Unifanye kusikia furaha na shangwe ili kwamba mifupa ulioivunja ifurahi.
9 求你掩面不看我的罪, 塗抹我一切的罪孽。
Uufiche uso wako mbali na dhambi zangu na uyafute maovu yangu yote.
10 上帝啊,求你為我造清潔的心, 使我裏面重新有正直的靈。
Uniumbie moyo safi, Mungu, na uifanye upya roho ya haki ndani yangu.
11 不要丟棄我,使我離開你的面; 不要從我收回你的聖靈。
Usiniondoe uweponi mwako, na usimuondoe roho Mtakatifu ndani yangu.
12 求你使我仍得救恩之樂, 賜我樂意的靈扶持我,
Unirudishie furaha ya wokovu wako, na unihifadhi mimi kwa roho ya utayari.
13 我就把你的道指教有過犯的人, 罪人必歸順你。
Ndipo nitawafundisha wakosaji jia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
14 上帝啊,你是拯救我的上帝; 求你救我脫離流人血的罪! 我的舌頭就高聲歌唱你的公義。
Unisamehe kwa ajili ya umwagaji damu, Mungu wa wokovu wangu, nami nitapiga kelele za shangwe ya haki yako.
15 主啊,求你使我嘴唇張開, 我的口便傳揚讚美你的話!
Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na mdomo wangu itazieleza sifa zako.
16 你本不喜愛祭物,若喜愛,我就獻上; 燔祭,你也不喜悅。
Kwa maana wewe haufurahishwi katika sadaka, vinginevyo ningekutolea sadaka; wewe hauwi radhi katika sadaka ya kuteketezwa.
17 上帝所要的祭就是憂傷的靈; 上帝啊,憂傷痛悔的心,你必不輕看。
Sadaka ya Mungu ni roho iliyovunjika. Wewe, Mungu hautadharau moyo uliopondeka na kujutia.
18 求你隨你的美意善待錫安, 建造耶路撒冷的城牆。
Uitendee mema Sayuni katika nia yako nzuri; uzijenge tena kuta za Yerusalem.
19 那時,你必喜愛公義的祭 和燔祭並全牲的燔祭; 那時,人必將公牛獻在你壇上。
Kisha wewe utafurahia sadaka yenye haki, katika sadaka za kuteketeza; ndipo watu wetu watatoa ng'ombe kwenye madhabahu yako.

< 詩篇 51 >