< 詩篇 17 >

1 大衛的祈禱。 耶和華啊,求你聽聞公義, 側耳聽我的呼籲! 求你留心聽我這不出於詭詐嘴唇的祈禱!
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 願我的判語從你面前發出; 願你的眼睛觀看公正。
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 你已經試驗我的心; 你在夜間鑒察我; 你熬煉我,卻找不着甚麼; 我立志叫我口中沒有過失。
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 論到人的行為,我藉着你嘴唇的言語自己謹守, 不行強暴人的道路。
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 我的腳踏定了你的路徑; 我的兩腳未曾滑跌。
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 上帝啊,我曾求告你,因為你必應允我; 求你向我側耳,聽我的言語。
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 求你顯出你奇妙的慈愛來; 你是那用右手拯救投靠你的脫離起來攻擊他們的人。
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 求你保護我,如同保護眼中的瞳人; 將我隱藏在你翅膀的蔭下,
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 使我脫離那欺壓我的惡人, 就是圍困我要害我命的仇敵。
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 他們的心被脂油包裹; 他們用口說驕傲的話。
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 他們圍困了我們的腳步; 他們瞪着眼,要把我們推倒在地。
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 他像獅子急要抓食, 又像少壯獅子蹲伏在暗處。
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 耶和華啊,求你起來,前去迎敵,將他打倒! 用你的刀救護我命脫離惡人。
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 耶和華啊,求你用手救我脫離世人, 脫離那只在今生有福分的世人! 你把你的財寶充滿他們的肚腹; 他們因有兒女就心滿意足, 將其餘的財物留給他們的嬰孩。
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 至於我,我必在義中見你的面; 我醒了的時候,得見你的形像就心滿意足了。
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

< 詩篇 17 >