< 詩篇 104 >

1 我的心哪,你要稱頌耶和華! 耶和華-我的上帝啊,你為至大! 你以尊榮威嚴為衣服,
Nitamsifu Yahwe maisha yangu yote, Ewe Yahwe Mungu wangu, wewe ni mkubwa sana; umevikwa kwa utukufu na enzi.
2 披上亮光,如披外袍, 鋪張穹蒼,如鋪幔子,
Unajifunika mwenyewe kwa nuru kama kwa mavazi; umetandaza mbingu kama pazia za hema.
3 在水中立樓閣的棟樑, 用雲彩為車輦, 藉着風的翅膀而行,
Umeweka mawinguni mihimili ya vyumba vyako; huyafanya mawingu gari lako; hutembea juu ya mbawa za upepo.
4 以風為使者, 以火焰為僕役,
Yeye huufanya upepo kuwa wajumbe wake, miale ya moto kuwa watumishi wake.
5 將地立在根基上, 使地永不動搖。
Aliiweka misingi ya nchi, nayo haitahamishwa kamwe.
6 你用深水遮蓋地面,猶如衣裳; 諸水高過山嶺。
Wewe uliifunika nchi kwa maji kama kwa mavazi; maji yalifunika milima.
7 你的斥責一發,水便奔逃; 你的雷聲一發,水便奔流。
Kukemea kwako kulifanya maji kupungua; kwa sauti ya radi yako yakaondoka kasi.
8 諸山升上,諸谷沉下, 歸你為它所安定之地。
Milima iliinuka, na mabonde yakaenea mahali ambapo wewe ulikwisha pachagua kwa ajili yao.
9 你定了界限,使水不能過去, 不再轉回遮蓋地面。
Umeweka mipaka kwa ajili yao ambao hayawezi kuupita; hayawezi kuifunika nchi tena.
10 耶和華使泉源湧在山谷, 流在山間,
Yeye alifanya chemchemi kutiririsha maji mabondeni; mito kutiririka katikati ya milima.
11 使野地的走獸有水喝, 野驢得解其渴。
Inasambaza maji kwa ajili ya wanyama wote wa shambani; punda wa porini hukata kiu yao.
12 天上的飛鳥在水旁住宿, 在樹枝上啼叫。
Kandokando ya mito ndege hujenga viota vyao; huimba kati ya matawi.
13 他從樓閣中澆灌山嶺; 因他作為的功效,地就豐足。
Humwagilia milima kutoka katika chumba chake cha maji mawinguni. Nchi imejazwa kwa matunda ya kazi yake.
14 他使草生長,給六畜吃, 使菜蔬發長,供給人用, 使人從地裏能得食物,
Huzifanya nyasi kukua kwa ajili ya mifugo na mimea kwa ajili ya binadamu kulima ili kwamba mwanadamu aweze kuzalisha chakula toka nchini.
15 又得酒能悅人心, 得油能潤人面, 得糧能養人心。
Hutengeneza mvinyo kumfurahisha mwanadamu, mafuta yakumfanya uso wake ung'ae, na chakula kwa ajili ya kuimarisha uhai wake.
16 佳美的樹木,就是黎巴嫩的香柏樹, 是耶和華所栽種的,都滿了汁漿。
Miti ya Yahwe hupata mvua nyingi; Mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 雀鳥在其上搭窩; 至於鶴,松樹是牠的房屋。
Hapo ndege hutengeneza viota vyao. Na korongo, misunobari ni nyuma yake.
18 高山為野山羊的住所; 巖石為沙番的藏處。
Mbuzi mwitu huishi kwenye milima mrefu; na urefu wa milima ni kimilio la wibari.
19 你安置月亮為定節令; 日頭自知沉落。
Aliuchagua mwezi kuweka alama ya majira; jua latambua kuchwa kwake.
20 你造黑暗為夜, 林中的百獸就都爬出來。
Wewe hufanya giza la usiku ambapo wanyama wote wa msituni hutoka nje.
21 少壯獅子吼叫,要抓食, 向上帝尋求食物。
Wana simba huunguruma kwa ajili ya mawindo na hutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 日頭一出,獸便躲避, 臥在洞裏。
Jua linapochomoza, huenda zao na kujilaza mapangoni mwao.
23 人出去做工, 勞碌直到晚上。
Wakati huo huo, watu hutoka nje kuelekea kazi zao na utumishi wake mpaka jioni.
24 耶和華啊,你所造的何其多! 都是你用智慧造成的; 遍地滿了你的豐富。
Yahwe, ni jinsi gani kazi zako zilivyo nyingi na za aina mbalimbali! Kwa hekima ulizifanya zote; nchi inafurika kwa kazi zako.
25 那裏有海,又大又廣; 其中有無數的動物, 大小活物都有。
Kule kuna bahari, yenye kina kirefu na pana, ikiwa na viume vingi visivyo hesabika, vyote vidogo na vikubwa.
26 那裏有船行走, 有你所造的鱷魚游泳在其中。
Meli husafili humo, na ndimo alimo Lewiathani uliye muumba acheze baharini.
27 這都仰望你按時給牠食物。
Hawa wote hukutazama wewe uwape chakula kwa wakati.
28 你給牠們,牠們便拾起來; 你張手,牠們飽得美食。
Unapowapa chakula, hukusanyika; ufunguapo mkono wako, wanatosheka.
29 你掩面,牠們便驚惶; 你收回牠們的氣,牠們就死亡,歸於塵土。
Unapouficha uso wako, wanateseka; ukiiondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 你發出你的靈,牠們便受造; 你使地面更換為新。
Unapotuma Roho yako, wanaumbwa, nawe unaifanya upya nchi.
31 願耶和華的榮耀存到永遠! 願耶和華喜悅自己所造的!
Utukufu wa Yahwe na udumu milele; Yahwe na aufurahie uumbaji wake.
32 他看地,地便震動; 他摸山,山就冒煙。
Yeye hutazama nchi, nayo hutikisika; huigusa milima, nayo hutoa moshi.
33 我要一生向耶和華唱詩! 我還活的時候,要向我上帝歌頌!
Nitamwimbia Yahwe maisha yangu yote; nitamwimbia sifa Mungu wangu nigali ninaishi.
34 願他以我的默念為甘甜! 我要因耶和華歡喜!
Mawazo yangu na yawe matamu kwake; nitafurahia katika Yahwe.
35 願罪人從世上消滅! 願惡人歸於無有! 我的心哪,要稱頌耶和華! 你們要讚美耶和華!
Wenye dhambi na waondoshwe katika nchi, na waovu wasiwepo tena. Ninamsifu Yahwe maisha yangu yote. Msifuni Yahwe.

< 詩篇 104 >