< 詩篇 104 >
1 我的心哪,你要稱頌耶和華! 耶和華-我的上帝啊,你為至大! 你以尊榮威嚴為衣服,
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 在水中立樓閣的棟樑, 用雲彩為車輦, 藉着風的翅膀而行,
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 你的斥責一發,水便奔逃; 你的雷聲一發,水便奔流。
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 你定了界限,使水不能過去, 不再轉回遮蓋地面。
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 他從樓閣中澆灌山嶺; 因他作為的功效,地就豐足。
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 他使草生長,給六畜吃, 使菜蔬發長,供給人用, 使人從地裏能得食物,
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 又得酒能悅人心, 得油能潤人面, 得糧能養人心。
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 佳美的樹木,就是黎巴嫩的香柏樹, 是耶和華所栽種的,都滿了汁漿。
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 耶和華啊,你所造的何其多! 都是你用智慧造成的; 遍地滿了你的豐富。
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 那裏有海,又大又廣; 其中有無數的動物, 大小活物都有。
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 你給牠們,牠們便拾起來; 你張手,牠們飽得美食。
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 你掩面,牠們便驚惶; 你收回牠們的氣,牠們就死亡,歸於塵土。
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 你發出你的靈,牠們便受造; 你使地面更換為新。
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 願耶和華的榮耀存到永遠! 願耶和華喜悅自己所造的!
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 我要一生向耶和華唱詩! 我還活的時候,要向我上帝歌頌!
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 願罪人從世上消滅! 願惡人歸於無有! 我的心哪,要稱頌耶和華! 你們要讚美耶和華!
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.