< 詩篇 104 >

1 我的心哪,你要稱頌耶和華! 耶和華-我的上帝啊,你為至大! 你以尊榮威嚴為衣服,
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 披上亮光,如披外袍, 鋪張穹蒼,如鋪幔子,
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 在水中立樓閣的棟樑, 用雲彩為車輦, 藉着風的翅膀而行,
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 以風為使者, 以火焰為僕役,
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 將地立在根基上, 使地永不動搖。
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 你用深水遮蓋地面,猶如衣裳; 諸水高過山嶺。
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 你的斥責一發,水便奔逃; 你的雷聲一發,水便奔流。
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 諸山升上,諸谷沉下, 歸你為它所安定之地。
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 你定了界限,使水不能過去, 不再轉回遮蓋地面。
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 耶和華使泉源湧在山谷, 流在山間,
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 使野地的走獸有水喝, 野驢得解其渴。
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 天上的飛鳥在水旁住宿, 在樹枝上啼叫。
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 他從樓閣中澆灌山嶺; 因他作為的功效,地就豐足。
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 他使草生長,給六畜吃, 使菜蔬發長,供給人用, 使人從地裏能得食物,
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 又得酒能悅人心, 得油能潤人面, 得糧能養人心。
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 佳美的樹木,就是黎巴嫩的香柏樹, 是耶和華所栽種的,都滿了汁漿。
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 雀鳥在其上搭窩; 至於鶴,松樹是牠的房屋。
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 高山為野山羊的住所; 巖石為沙番的藏處。
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 你安置月亮為定節令; 日頭自知沉落。
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 你造黑暗為夜, 林中的百獸就都爬出來。
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 少壯獅子吼叫,要抓食, 向上帝尋求食物。
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 日頭一出,獸便躲避, 臥在洞裏。
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 人出去做工, 勞碌直到晚上。
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 耶和華啊,你所造的何其多! 都是你用智慧造成的; 遍地滿了你的豐富。
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 那裏有海,又大又廣; 其中有無數的動物, 大小活物都有。
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 那裏有船行走, 有你所造的鱷魚游泳在其中。
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 這都仰望你按時給牠食物。
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 你給牠們,牠們便拾起來; 你張手,牠們飽得美食。
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 你掩面,牠們便驚惶; 你收回牠們的氣,牠們就死亡,歸於塵土。
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 你發出你的靈,牠們便受造; 你使地面更換為新。
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 願耶和華的榮耀存到永遠! 願耶和華喜悅自己所造的!
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 他看地,地便震動; 他摸山,山就冒煙。
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 我要一生向耶和華唱詩! 我還活的時候,要向我上帝歌頌!
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 願他以我的默念為甘甜! 我要因耶和華歡喜!
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 願罪人從世上消滅! 願惡人歸於無有! 我的心哪,要稱頌耶和華! 你們要讚美耶和華!
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< 詩篇 104 >