< 詩篇 1 >
1 不從惡人的計謀, 不站罪人的道路, 不坐褻慢人的座位,
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 惟喜愛耶和華的律法, 晝夜思想, 這人便為有福!
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 他要像一棵樹栽在溪水旁, 按時候結果子, 葉子也不枯乾。 凡他所做的盡都順利。
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 因此,當審判的時候,惡人必站立不住; 罪人在義人的會中也是如此。
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 因為耶和華知道義人的道路; 惡人的道路卻必滅亡。
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.