< 箴言 4 >

1 眾子啊,要聽父親的教訓, 留心得知聰明。
Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu; sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
2 因我所給你們的是好教訓; 不可離棄我的法則。
Ninawapa mafundisho ya maana, kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
3 我在父親面前為孝子, 在母親眼中為獨一的嬌兒。
Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu, ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
4 父親教訓我說:你心要存記我的言語, 遵守我的命令,便得存活。
baba alinifundisha akisema, “Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote; yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
5 要得智慧,要得聰明,不可忘記, 也不可偏離我口中的言語。
Pata hekima, pata ufahamu; usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
6 不可離棄智慧,智慧就護衛你; 要愛她,她就保守你。
Usimwache hekima naye atakuweka salama; mpende, naye atakulinda.
7 智慧為首; 所以,要得智慧。 在你一切所得之內必得聰明。
Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima. Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
8 高舉智慧,她就使你高升; 懷抱智慧,她就使你尊榮。
Mstahi, naye atakukweza; mkumbatie, naye atakuheshimu.
9 她必將華冠加在你頭上, 把榮冕交給你。
Atakuvika shada la neema kichwani mwako na kukupa taji ya utukufu.”
10 我兒,你要聽受我的言語, 就必延年益壽。
Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia, nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
11 我已指教你走智慧的道, 引導你行正直的路。
Ninakuongoza katika njia ya hekima na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12 你行走,腳步必不致狹窄; 你奔跑,也不致跌倒。
Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa; ukimbiapo, hutajikwaa.
13 要持定訓誨,不可放鬆; 必當謹守,因為它是你的生命。
Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako.
14 不可行惡人的路; 不要走壞人的道。
Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
15 要躲避,不可經過; 要轉身而去。
Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
16 這等人若不行惡,不得睡覺; 不使人跌倒,睡臥不安;
Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
17 因為他們以奸惡吃餅, 以強暴喝酒。
Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.
18 但義人的路好像黎明的光, 越照越明,直到日午。
Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko, ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
19 惡人的道好像幽暗, 自己不知因甚麼跌倒。
Lakini njia ya waovu ni kama giza nene; hawajui kinachowafanya wajikwae.
20 我兒,要留心聽我的言詞, 側耳聽我的話語,
Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia; sikiliza kwa makini maneno yangu.
21 都不可離你的眼目, 要存記在你心中。
Usiruhusu yaondoke machoni pako, yahifadhi ndani ya moyo wako;
22 因為得着它的,就得了生命, 又得了醫全體的良藥。
kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
23 你要保守你心,勝過保守一切, 因為一生的果效是由心發出。
Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24 你要除掉邪僻的口, 棄絕乖謬的嘴。
Epusha kinywa chako na ukaidi; weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
25 你的眼目要向前正看; 你的眼睛當向前直觀。
Macho yako na yatazame mbele, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
26 要修平你腳下的路, 堅定你一切的道。
Sawazisha mapito ya miguu yako na njia zako zote ziwe zimethibitika.
27 不可偏向左右; 要使你的腳離開邪惡。
Usigeuke kulia wala kushoto; epusha mguu wako na ubaya.

< 箴言 4 >