< 箴言 30 >
1 雅基的兒子亞古珥的言語就是真言。 這人對以鐵和烏甲說:
Misemo ya Aguri mwana wa Yake, usia: Huyu mtu alimwambia Ithieli, naam, kwa Ithieli na kwa Ukali:
“Mimi ni mjinga kuliko wanadamu wote; sina ufahamu wa kibinadamu.
Sijajifunza hekima, wala sina maarifa ya kumjua yeye Aliye Mtakatifu.
4 誰升天又降下來? 誰聚風在掌握中? 誰包水在衣服裏? 誰立定地的四極? 他名叫甚麼? 他兒子名叫甚麼? 你知道嗎?
Ni nani ameshapanda mbinguni na kushuka? Ni nani ameshakusanya upepo kwenye vitanga vya mikono yake? Ni nani ameshafungia maji kwenye nguo yake? Ni nani ameimarisha miisho yote ya dunia? Jina lake ni nani, na mwanawe anaitwa nani? Niambie kama unajua!
5 上帝的言語句句都是煉淨的; 投靠他的,他便作他們的盾牌。
“Kila neno la Mungu ni kamilifu; yeye ni ngao kwa wale wanaomkimbilia.
6 他的言語,你不可加添, 恐怕他責備你,你就顯為說謊言的。
Usiongeze kwenye maneno yake, ama atakukemea na kukuthibitisha kuwa mwongo.
“Ninakuomba vitu viwili, Ee Bwana; usininyime kabla sijafa:
8 求你使虛假和謊言遠離我; 使我也不貧窮也不富足; 賜給我需用的飲食,
Uutenge mbali nami udanganyifu na uongo; usinipe umaskini wala utajiri, bali unipe chakula cha kunitosha kila siku.
9 恐怕我飽足不認你,說: 耶和華是誰呢? 又恐怕我貧窮就偷竊, 以致褻瀆我上帝的名。
Nisije nikawa na vingi vya kuzidi nikakukana na kusema, ‘Bwana ni nani?’ Au nisije nikawa maskini nikaiba, nami nikaliaibisha jina la Mungu wangu.
10 你不要向主人讒謗僕人, 恐怕他咒詛你,你便算為有罪。
“Usimchongee mtumishi kwa bwana wake, asije akakulaani, ukapatilizwa kwalo.
“Wako watu wale ambao huwalaani baba zao na wala hawawabariki mama zao;
12 有一宗人,自以為清潔, 卻沒有洗去自己的污穢。
wale ambao ni safi machoni pao wenyewe kumbe hawakuoshwa uchafu wao;
wale ambao daima macho yao ni ya kiburi, ambao kutazama kwao ni kwa dharau;
14 有一宗人,牙如劍,齒如刀, 要吞滅地上的困苦人和世間的窮乏人。
wale ambao meno yao ni panga na ambao mataya yao yamewekwa visu kuwaangamiza maskini katika nchi, na wahitaji kutoka miongoni mwa wanadamu.
15 螞蟥有兩個女兒, 常說:給呀,給呀! 有三樣不知足的, 連不說「夠的」共有四樣:
“Mruba anao binti wawili waliao, ‘Nipe! Nipe!’ “Kuna vitu vitatu visivyotosheka kamwe, naam, viko vinne visivyosema, ‘Yatosha!’:
16 就是陰間和石胎, 浸水不足的地,並火。 (Sheol )
Ni kaburi, tumbo lisilozaa, nchi isiyoshiba maji kamwe, na moto, usiosema kamwe, ‘Yatosha!’ (Sheol )
17 戲笑父親、藐視而不聽從母親的, 他的眼睛必為谷中的烏鴉啄出來,為鷹雛所吃。
“Jicho lile limdhihakilo baba, lile linalodharau kumtii mama, litangʼolewa na kunguru wa bondeni, litaliwa na tai.
18 我所測不透的奇妙有三樣, 連我所不知道的共有四樣:
“Kuna vitu vitatu vinavyonishangaza sana, naam, vinne nisivyovielewa:
19 就是鷹在空中飛的道; 蛇在磐石上爬的道; 船在海中行的道; 男與女交合的道。
Ni mwendo wa tai katika anga, mwendo wa nyoka juu ya mwamba, mwendo wa meli katika maji makuu ya bahari, nao mwendo wa mtu pamoja na msichana.
20 淫婦的道也是這樣: 她吃了,把嘴一擦就說: 我沒有行惡。
“Huu ndio mwendo wa mwanamke mzinzi, hula akapangusa kinywa chake na kusema, ‘Sikufanya chochote kibaya.’
“Kwa mambo matatu nchi hutetemeka, naam, kwa mambo manne haiwezi kuvumilia:
Mtumwa awapo mfalme, mpumbavu ashibapo chakula,
mwanamke asiyependwa aolewapo, naye mtumishi wa kike achukuapo nafasi ya bibi yake.
“Vitu vinne duniani vilivyo vidogo, lakini vina akili nyingi sana:
Mchwa ni viumbe wenye nguvu ndogo, hata hivyo hujiwekea akiba ya chakula chao wakati wa kiangazi.
Pelele ni viumbe vyenye uwezo mdogo hata hivyo hujitengenezea nyumba zao kwenye miamba.
Nzige hawana mfalme, hata hivyo huenda pamoja vikosi vikosi.
Mjusi anaweza kushikwa kwa mkono, hata hivyo huonekana katika majumba ya kifalme.
“Viko vitu vitatu ambavyo vinapendeza katika mwendo wao, naam, vinne ambavyo hutembea kwa mwendo wa madaha:
simba, mwenye nguvu miongoni mwa wanyama, asiyerudi nyuma kwa chochote;
jogoo atembeaye kwa maringo, pia beberu, naye mfalme pamoja na jeshi lake lililomzunguka.
32 你若行事愚頑,自高自傲, 或是懷了惡念,就當用手摀口。
“Ikiwa umefanya upumbavu na ukajitukuza mwenyewe, au kama umepanga mabaya, basi funika mdomo wako na mkono wako.
33 搖牛奶必成奶油; 扭鼻子必出血。 照樣,激動怒氣必起爭端。
Kwa maana kama vile kusukasuka maziwa hutoa siagi, na pia kule kufinya pua hutoa damu, kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.”