< 箴言 23 >
Uketipo kula chakula na mtawala, angalia vyema kile kilicho mbele yako,
na utie kisu kooni mwako kama ukiwa mlafi.
Usitamani vyakula vyake vitamu kwa kuwa chakula hicho ni cha hila.
Usijitaabishe ili kuupata utajiri, uwe na hekima kuonyesha kujizuia.
5 你豈要定睛在虛無的錢財上嗎? 因錢財必長翅膀,如鷹向天飛去。
Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka, huwa kama umepata mabawa ghafula, ukaruka na kutoweka angani kama tai.
Usile chakula cha mtu mchoyo, usitamani vyakula vyake vitamu,
7 因為他心怎樣思量, 他為人就是怎樣。 他雖對你說,請吃,請喝, 他的心卻與你相背。
kwa maana yeye ni aina ya mtu ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama. Anakuambia, “Kula na kunywa,” lakini moyo wake hauko pamoja nawe.
8 你所吃的那點食物必吐出來; 你所說的甘美言語也必落空。
Utatapika kile kidogo ulichokula, nawe utakuwa umepoteza bure maneno yako ya kumsifu.
9 你不要說話給愚昧人聽, 因他必藐視你智慧的言語。
Usizungumze na mpumbavu, kwa maana atadhihaki hekima ya maneno yako.
10 不可挪移古時的地界, 也不可侵入孤兒的田地;
Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima,
11 因他們的救贖主大有能力, 他必向你為他們辨屈。
kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu, atalichukua shauri lao dhidi yako.
Elekeza moyo wako kwenye mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13 不可不管教孩童; 你用杖打他,他必不至於死。
Usimnyime mtoto adhabu, ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.
14 你要用杖打他, 就可以救他的靈魂免下陰間。 (Sheol )
Mwadhibu kwa fimbo na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini. (Sheol )
Mwanangu, kama moyo wako una hekima, basi moyo wangu utafurahi,
utu wangu wa ndani utafurahi, wakati midomo yako itakapozungumza lililo sawa.
Usiuruhusu moyo wako kuwaonea wivu wenye dhambi, bali kila mara uwe na bidii katika kumcha Bwana.
Hakika kuna tumaini la baadaye kwa ajili yako, nalo tarajio lako halitakatiliwa mbali.
19 我兒,你當聽,當存智慧, 好在正道上引導你的心。
Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima, weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa.
Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo, au wale walao nyama kwa pupa,
21 因為好酒貪食的,必致貧窮; 好睡覺的,必穿破爛衣服。
kwa maana walevi na walafi huwa maskini, nako kusinzia huwavika matambara.
22 你要聽從生你的父親; 你母親老了,也不可藐視她。
Msikilize baba yako, aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.
23 你當買真理; 就是智慧、訓誨,和聰明也都不可賣。
Nunua kweli wala usiiuze, pata hekima, adabu na ufahamu.
24 義人的父親必大得快樂; 人生智慧的兒子,必因他歡喜。
Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa, naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia.
Baba yako na mama yako na wafurahi, mama aliyekuzaa na ashangilie!
26 我兒,要將你的心歸我; 你的眼目也要喜悅我的道路。
Mwanangu, nipe moyo wako, macho yako na yafuate njia zangu,
kwa maana kahaba ni shimo refu na mwanamke mpotovu ni kisima chembamba.
Kama mnyangʼanyi, hungojea akivizia, naye huzidisha wasio waaminifu miongoni mwa wanaume.
29 誰有禍患?誰有憂愁? 誰有爭鬥?誰有哀歎? 誰無故受傷?誰眼目紅赤?
Ni nani mwenye ole? Ni nani mwenye huzuni? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye malalamiko? Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu? Ni nani mwenye macho mekundu?
Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo, hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.
31 酒發紅,在杯中閃爍, 你不可觀看, 雖然下咽舒暢, 終久是咬你如蛇,刺你如毒蛇。
Usiukodolee macho mvinyo wakati ukiwa mwekundu, wakati unapometameta kwenye bilauri, wakati ushukapo taratibu!
Mwishowe huuma kama nyoka na kutia sumu yake kama nyoka mwenye sumu.
Macho yako yataona mambo mageni na moyo wako kuwazia mambo yaliyopotoka.
Utakuwa kama alalaye katikati ya bahari, alalaye juu ya kamba ya merikebu.
35 你必說:人打我,我卻未受傷; 人鞭打我,我竟不覺得。 我幾時清醒,我仍去尋酒。
Utasema, “Wamenipiga lakini sikuumia! Wamenichapa, lakini sisikii! Nitaamka lini ili nikanywe tena?”