< 箴言 14 >
Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake, bali mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe.
2 行動正直的,敬畏耶和華; 行事乖僻的,卻藐視他。
Yeye ambaye njia zake ni nyofu humcha Bwana, bali yeye ambaye njia zake zimepotoka humdharau Mungu.
3 愚妄人口中驕傲,如杖責打己身; 智慧人的嘴必保守自己。
Mazungumzo ya mpumbavu huleta fimbo mgongoni mwake, bali mwenye hekima hulindwa na maneno ya midomo yake.
Pale ambapo hakuna mafahali, hori ni tupu, bali kutokana na nguvu za fahali huja mavuno mengi.
Shahidi mwaminifu hadanganyi, bali shahidi wa uongo humimina uongo.
Mwenye mzaha huitafuta hekima na haipati, bali maarifa huja kwa urahisi kwa anayepambanua.
Kaa mbali na mtu mpumbavu, kwa maana hutapata maarifa katika midomo yake.
8 通達人的智慧在乎明白己道; 愚昧人的愚妄乃是詭詐。
Hekima ya mwenye busara ni kufikiria njia zake, bali upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.
Wapumbavu hudhihaki kujirekebisha kutoka dhambi, bali wema hupatikana miongoni mwa wanyofu.
10 心中的苦楚,自己知道; 心裏的喜樂,外人無干。
Kila moyo hujua uchungu wake wenyewe, wala hakuna yeyote awezaye kushiriki furaha yake.
Nyumba ya mwovu itaangamizwa, bali hema la mnyofu litastawi.
Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu, bali mwisho wake huelekeza mautini.
Hata katika kicheko moyo waweza kuuma, nayo furaha yaweza kuishia katika majonzi.
14 心中背道的,必滿得自己的結果; 善人必從自己的行為得以知足。
Wasio na imani watapatilizwa kikamilifu kwa ajili ya njia zao, naye mtu mwema atapewa thawabu kwa ajili ya njia yake.
Mtu mjinga huamini kila kitu, bali mwenye busara hufikiria hatua zake.
16 智慧人懼怕,就遠離惡事; 愚妄人卻狂傲自恃。
Mtu mwenye hekima humcha Bwana na kuepuka mabaya, bali mpumbavu hukasirika kwa hamaki na uzembe.
17 輕易發怒的,行事愚妄; 設立詭計的,被人恨惡。
Mtu anayekasirika kwa haraka hufanya mambo ya upumbavu, naye mtu wa hila huchukiwa.
Mjinga hurithi upumbavu, bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.
Watu wabaya watasujudu mbele ya watu wema, nao waovu kwenye malango ya wenye haki.
Maskini huepukwa hata na majirani zao, bali matajiri wana marafiki wengi.
21 藐視鄰舍的,這人有罪; 憐憫貧窮的,這人有福。
Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi, bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.
22 謀惡的,豈非走入迷途嗎? 謀善的,必得慈愛和誠實。
Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki? Bali wale wanaopanga kilicho chema hupata upendo na uaminifu.
Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida, bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.
24 智慧人的財為自己的冠冕; 愚妄人的愚昧終是愚昧。
Utajiri wa wenye hekima ni taji yao, bali upumbavu wa wapumbavu huzaa upumbavu.
25 作真見證的,救人性命; 吐出謊言的,施行詭詐。
Shahidi wa kweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo ni mdanganyifu.
26 敬畏耶和華的,大有倚靠; 他的兒女也有避難所。
Yeye amchaye Bwana ana ngome salama, na kwa watoto wake itakuwa kimbilio.
27 敬畏耶和華就是生命的泉源, 可以使人離開死亡的網羅。
Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima, ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.
Wingi wa watu ni utukufu wa mfalme, bali pasipo watu mkuu huangamia.
29 不輕易發怒的,大有聰明; 性情暴躁的,大顯愚妄。
Mtu mwenye subira ana ufahamu mwingi, bali anayekasirika haraka huonyesha upumbavu.
Moyo wenye amani huupa mwili uzima, bali wivu huozesha mifupa.
31 欺壓貧寒的,是辱沒造他的主; 憐憫窮乏的,乃是尊敬主。
Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao, bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.
32 惡人在所行的惡上必被推倒; 義人臨死,有所投靠。
Waovu huangamizwa kwa matendo yao maovu, bali hata katika kifo wenye haki hupata kimbilio.
33 智慧存在聰明人心中; 愚昧人心裏所存的,顯而易見。
Hekima hukaa katika moyo wa mwenye ufahamu bali haijulikani miongoni mwa wapumbavu.
Haki huinua taifa, bali dhambi ni aibu kwa watu wote.
Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima, bali ghadhabu yake humwangukia mtumishi mwenye kuaibisha.