< 約伯記 6 >
2 惟願我的煩惱稱一稱, 我一切的災害放在天平裏;
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 因全能者的箭射入我身; 其毒,我的靈喝盡了; 上帝的驚嚇擺陣攻擊我。
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 我因沒有違棄那聖者的言語, 就仍以此為安慰, 在不止息的痛苦中還可踴躍。
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 我有甚麼氣力使我等候? 我有甚麼結局使我忍耐?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 我的氣力豈是石頭的氣力? 我的肉身豈是銅的呢?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 在我豈不是毫無幫助嗎? 智慧豈不是從我心中趕出淨盡嗎?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 那將要灰心、離棄全能者、 不敬畏上帝的人, 他的朋友當以慈愛待他。
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 我的弟兄詭詐,好像溪水, 又像溪水流乾的河道。
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 天氣漸暖就隨時消化, 日頭炎熱便從原處乾涸。
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 結伴的客旅離棄大道, 順河偏行,到荒野之地死亡。
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 我豈說:請你們供給我, 從你們的財物中送禮物給我?
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 豈說:拯救我脫離敵人的手嗎? 救贖我脫離強暴人的手嗎?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 請你們教導我,我便不作聲; 使我明白在何事上有錯。
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 正直的言語力量何其大! 但你們責備是責備甚麼呢?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 絕望人的講論既然如風, 你們還想要駁正言語嗎?
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 請你們轉意,不要不公; 請再轉意,我的事有理。
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 我的舌上豈有不義嗎? 我的口裏豈不辨奸惡嗎?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?