< 約伯記 23 >

1 約伯回答說:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 如今我的哀告還算為悖逆; 我的責罰比我的唉哼還重。
“Hata leo malalamiko yangu ni chungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
3 惟願我能知道在哪裏可以尋見上帝, 能到他的臺前,
Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
4 我就在他面前將我的案件陳明, 滿口辯白。
Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
5 我必知道他回答我的言語, 明白他向我所說的話。
Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
6 他豈用大能與我爭辯嗎? 必不這樣!他必理會我。
Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
7 在他那裏正直人可以與他辯論; 這樣,我必永遠脫離那審判我的。
Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
8 只是,我往前行,他不在那裏, 往後退,也不能見他。
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
9 他在左邊行事,我卻不能看見, 在右邊隱藏,我也不能見他。
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
10 然而他知道我所行的路; 他試煉我之後,我必如精金。
Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
11 我腳追隨他的步履; 我謹守他的道,並不偏離。
Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
12 他嘴唇的命令,我未曾背棄; 我看重他口中的言語,過於我需用的飲食。
Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
13 只是他心志已定,誰能使他轉意呢? 他心裏所願的,就行出來。
“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
14 他向我所定的,就必做成; 這類的事他還有許多。
Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
15 所以我在他面前驚惶; 我思念這事便懼怕他。
Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
16 上帝使我喪膽; 全能者使我驚惶。
Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
17 我的恐懼不是因為黑暗, 也不是因為幽暗蒙蔽我的臉。
Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.

< 約伯記 23 >