< 诗篇 1 >
1 不从恶人的计谋, 不站罪人的道路, 不坐亵慢人的座位,
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 惟喜爱耶和华的律法, 昼夜思想, 这人便为有福!
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 他要像一棵树栽在溪水旁, 按时候结果子, 叶子也不枯干。 凡他所做的尽都顺利。
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 因此,当审判的时候、恶人必站立不住; 罪人在义人的会中也是如此。
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 因为耶和华知道义人的道路; 恶人的道路却必灭亡。
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.