< 诗篇 1 >

1 不从恶人的计谋, 不站罪人的道路, 不坐亵慢人的座位,
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 惟喜爱耶和华的律法, 昼夜思想, 这人便为有福!
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 他要像一棵树栽在溪水旁, 按时候结果子, 叶子也不枯干。 凡他所做的尽都顺利。
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 恶人并不是这样, 乃像糠秕被风吹散。
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 因此,当审判的时候、恶人必站立不住; 罪人在义人的会中也是如此。
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 因为耶和华知道义人的道路; 恶人的道路却必灭亡。
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< 诗篇 1 >