< 诗篇 74 >

1 亚萨的训诲诗。 神啊,你为何永远丢弃我们呢? 你为何向你草场的羊发怒,如烟冒出呢?
Utenzi wa Asafu. Ee Mungu, mbona umetukataa milele? Mbona hasira yako inatoka moshi juu ya kondoo wa malisho yako?
2 求你记念你古时所得来的会众, 就是你所赎、作你产业支派的, 并记念你向来所居住的锡安山。
Kumbuka watu uliowanunua zamani, kabila la urithi wako, ambao uliwakomboa: Mlima Sayuni, ambamo uliishi.
3 求你举步去看那日久荒凉之地, 仇敌在圣所中所行的一切恶事。
Geuza hatua zako kuelekea magofu haya ya kudumu, uharibifu wote huu ambao adui ameuleta pale patakatifu.
4 你的敌人在你会中吼叫; 他们竖了自己的旗为记号。
Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi, wanaweka bendera zao kama alama.
5 他们好像人扬起斧子, 砍伐林中的树。
Walifanya kama watu wanaotumia mashoka kukata kichaka cha miti.
6 圣所中一切雕刻的, 他们现在用斧子锤子打坏了。
Walivunjavunja milango yote iliyonakshiwa kwa mashoka na vishoka vyao.
7 他们用火焚烧你的圣所, 亵渎你名的居所,拆毁到地。
Waliteketeza kabisa mahali pako patakatifu, wakayanajisi makao ya Jina lako.
8 他们心里说:我们要尽行毁灭; 他们就在遍地把 神的会所都烧毁了。
Walisema mioyoni mwao, “Tutawaponda kabisa!” Walichoma kila mahali ambapo Mungu aliabudiwa katika nchi.
9 我们不见我们的标帜,不再有先知; 我们内中也没有人知道这灾祸要到几时呢!
Hatukupewa ishara za miujiza; hakuna manabii waliobaki, hakuna yeyote kati yetu ajuaye hali hii itachukua muda gani.
10 神啊,敌人辱骂要到几时呢? 仇敌亵渎你的名要到永远吗?
Ee Mungu, mtesi atakudhihaki mpaka lini? Je, adui watalitukana jina lako milele?
11 你为什么缩回你的右手? 求你从怀中伸出来,毁灭他们。
Kwa nini unazuia mkono wako, mkono wako wa kuume? Uutoe kutoka makunjo ya vazi lako na uwaangamize!
12 神自古以来为我的王, 在地上施行拯救。
Lakini wewe, Ee Mungu, ni mfalme wangu tangu zamani, unaleta wokovu duniani.
13 你曾用能力将海分开, 将水中大鱼的头打破。
Ni wewe uliyeigawanya bahari kwa uweza wako; ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa kutisha katika maji.
14 你曾砸碎鳄鱼的头, 把它给旷野的禽兽为食物。
Ni wewe uliyeponda vichwa vya Lewiathani nawe ukamtoa kama chakula kwa viumbe vya jangwani.
15 你曾分裂磐石,水便成了溪河; 你使长流的江河干了。
Ni wewe uliyefungua chemchemi na vijito, ulikausha mito ambayo ilikuwa ikitiririka daima.
16 白昼属你,黑夜也属你; 亮光和日头是你所预备的。
Mchana ni wako, nao usiku ni wako pia, uliziweka jua na mwezi.
17 地的一切疆界是你所立的; 夏天和冬天是你所定的。
Ni wewe uliyeiweka mipaka yote ya dunia, ulifanya kiangazi na masika.
18 耶和华啊,仇敌辱骂, 愚顽民亵渎了你的名,求你记念这事。
Ee Bwana, kumbuka jinsi mtesi alivyokudhihaki, jinsi watu wapumbavu walivyolitukana jina lako.
19 不要将你斑鸠的性命交给野兽; 不要永远忘记你困苦人的性命。
Usiukabidhi uhai wa njiwa wako kwa wanyama wakali wa mwitu; usisahau kabisa uhai wa watu wako wanaoteseka milele.
20 求你顾念所立的约, 因为地上黑暗之处都满了强暴的居所。
Likumbuke agano lako, maana mara kwa mara mambo ya jeuri yamejaa katika sehemu za giza nchini.
21 不要叫受欺压的人蒙羞回去; 要叫困苦穷乏的人赞美你的名。
Usiruhusu walioonewa warudi nyuma kwa aibu; maskini na wahitaji hebu walisifu jina lako.
22 神啊,求你起来为自己伸诉! 要记念愚顽人怎样终日辱骂你。
Inuka, Ee Mungu, ujitetee; kumbuka jinsi wapumbavu wanavyokudhihaki mchana kutwa.
23 不要忘记你敌人的声音; 那起来敌你之人的喧哗时常上升。
Usipuuze makelele ya watesi wako, ghasia za adui zako, zinazoinuka mfululizo.

< 诗篇 74 >