< 诗篇 4 >

1 大卫的诗,交与伶长。用丝弦的乐器。 显我为义的 神啊, 我呼吁的时候,求你应允我! 我在困苦中,你曾使我宽广; 现在求你怜恤我,听我的祷告!
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
2 你们这上流人哪,你们将我的尊荣变为羞辱要到几时呢? 你们喜爱虚妄,寻找虚假,要到几时呢? (细拉)
Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 你们要知道,耶和华已经分别虔诚人归他自己; 我求告耶和华,他必听我。
Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
4 你们应当畏惧,不可犯罪; 在床上的时候,要心里思想,并要肃静。 (细拉)
Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
5 当献上公义的祭, 又当倚靠耶和华。
Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
6 有许多人说:谁能指示我们什么好处? 耶和华啊,求你仰起脸来,光照我们。
Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 你使我心里快乐, 胜过那丰收五谷新酒的人。
Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 我必安然躺下睡觉, 因为独有你—耶和华使我安然居住。
Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.

< 诗篇 4 >