< 诗篇 145 >
1 大卫的赞美诗。 我的 神我的王啊,我要尊崇你! 我要永永远远称颂你的名!
Wimbo wa Sifa. Wa Daudi. Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme, nitalisifu jina lako milele na milele.
Kila siku nitakusifu na kulitukuza jina lako milele na milele.
Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, ukuu wake haupimiki.
4 这代要对那代颂赞你的作为, 也要传扬你的大能。
Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine, watasimulia matendo yako makuu.
Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako, nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.
6 人要传说你可畏之事的能力; 我也要传扬你的大德。
Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha, nami nitatangaza matendo yako makuu.
7 他们记念你的大恩就要传出来, 并要歌唱你的公义。
Wataadhimisha wema wako mwingi, na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.
8 耶和华有恩惠,有怜悯, 不轻易发怒,大有慈爱。
Bwana ni mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.
Bwana ni mwema kwa wote, ana huruma kwa vyote alivyovifanya.
10 耶和华啊,你一切所造的都要称谢你; 你的圣民也要称颂你,
Ee Bwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu, watakatifu wako watakutukuza.
Watasimulia utukufu wa ufalme wako na kusema juu ya ukuu wako,
12 好叫世人知道你大能的作为, 并你国度威严的荣耀。
ili watu wote wajue matendo yako makuu na utukufu wa fahari ya ufalme wako.
Ufalme wako ni ufalme wa milele, mamlaka yako hudumu vizazi vyote. Bwana ni mwaminifu kwa ahadi zake zote na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
14 凡跌倒的,耶和华将他们扶持; 凡被压下的,将他们扶起。
Bwana huwategemeza wote waangukao, na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.
Macho yao wote yanakutazama wewe, nawe huwapa chakula chao wakati wake.
Waufumbua mkono wako, watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.
17 耶和华在他一切所行的,无不公义; 在他一切所做的都有慈爱。
Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
18 凡求告耶和华的,就是诚心求告他的, 耶和华便与他们相近。
Bwana yu karibu na wote wamwitao, karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.
19 敬畏他的,他必成就他们的心愿, 也必听他们的呼求,拯救他们。
Huwatimizia wamchao matakwa yao, husikia kilio chao na kuwaokoa.
20 耶和华保护一切爱他的人, 却要灭绝一切的恶人。
Bwana huwalinda wote wampendao, bali waovu wote atawaangamiza.
21 我的口要说出赞美耶和华的话; 惟愿凡有血气的都永永远远称颂他的圣名。
Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana. Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu milele na milele.