< 诗篇 137 >
1 我们曾在巴比伦的河边坐下, 一追想锡安就哭了。
Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza tulipokumbuka Sayuni.
Kwenye miti ya huko tulitundika vinubi vyetu,
3 因为在那里,掳掠我们的要我们唱歌, 抢夺我们的要我们作乐,说: 给我们唱一首锡安歌吧!
kwa maana huko hao waliotuteka walitaka tuwaimbie nyimbo, watesi wetu walidai nyimbo za furaha; walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja kati ya nyimbo za Sayuni!”
Tutaimbaje nyimbo za Bwana, tukiwa nchi ya kigeni?
5 耶路撒冷啊,我若忘记你, 情愿我的右手忘记技巧!
Nikikusahau wewe, ee Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6 我若不记念你, 若不看耶路撒冷过于我所最喜乐的, 情愿我的舌头贴于上膛!
Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu kama sitakukumbuka wewe, kama nisipokufikiri Yerusalemu kuwa furaha yangu kubwa.
7 耶路撒冷遭难的日子, 以东人说:拆毁!拆毁! 直拆到根基! 耶和华啊,求你记念这仇!
Kumbuka, Ee Bwana, walichokifanya Waedomu, siku ile Yerusalemu ilipoanguka. Walisema, “Bomoa, Bomoa mpaka kwenye misingi yake!”
8 将要被灭的巴比伦城啊, 报复你像你待我们的,那人便为有福!
Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa, heri yeye atakayekulipiza wewe kwa yale uliyotutenda sisi:
yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga na kuwaponda juu ya miamba.