< 诗篇 129 >

1 上行之诗。 以色列当说:从我幼年以来, 敌人屡次苦害我,
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 从我幼年以来,敌人屡次苦害我, 却没有胜了我。
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 如同扶犁的在我背上扶犁而耕, 耕的犁沟甚长。
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 耶和华是公义的; 他砍断了恶人的绳索。
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 愿恨恶锡安的都蒙羞退后!
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 愿他们像房顶上的草, 未长成而枯干,
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 收割的不够一把, 捆禾的也不满怀。
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 过路的也不说: 愿耶和华所赐的福归与你们! 我们奉耶和华的名给你们祝福!
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”

< 诗篇 129 >