< 诗篇 102 >
1 困苦人发昏的时候,在耶和华面前吐露苦情的祷告。 耶和华啊,求你听我的祷告, 容我的呼求达到你面前!
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2 我在急难的日子,求你向我侧耳; 不要向我掩面! 我呼求的日子,求你快快应允我!
Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
3 因为,我的年日如烟云消灭; 我的骨头如火把烧着。
Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
8 我的仇敌终日辱骂我; 向我猖狂的人指着我赌咒。
Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
10 这都因你的恼恨和忿怒; 你把我拾起来,又把我摔下去。
kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
12 惟你—耶和华必存到永远; 你可记念的名也存到万代。
Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
13 你必起来怜恤锡安, 因现在是可怜她的时候, 日期已经到了。
Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15 列国要敬畏耶和华的名; 世上诸王都敬畏你的荣耀。
Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
18 这必为后代的人记下, 将来受造的民要赞美耶和华。
Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
19 因为,他从至高的圣所垂看; 耶和华从天向地观察,
“Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
21 使人在锡安传扬耶和华的名, 在耶路撒冷传扬赞美他的话,
Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
24 我说:我的 神啊, 不要使我中年去世。 你的年数世世无穷!
Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
26 天地都要灭没,你却要长存; 天地都要如外衣渐渐旧了。 你要将天地如里衣更换, 天地就都改变了。
Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
28 你仆人的子孙要长存; 他们的后裔要坚立在你面前。
Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”