< 民数记 33 >

1 以色列人按着军队,在摩西、亚伦的手下出埃及地所行的路程记在下面。
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 摩西遵着耶和华的吩咐记载他们所行的路程,其路程乃是这样:
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 正月十五日,就是逾越节的次日,以色列人从兰塞起行,在一切埃及人眼前昂然无惧地出去。
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 那时,埃及人正葬埋他们的长子,就是耶和华在他们中间所击杀的;耶和华也败坏他们的神。
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 以色列人从兰塞起行,安营在疏割。
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 从疏割起行,安营在旷野边的以倘。
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 从以倘起行,转到比哈·希录,是在巴力·洗分对面,就在密夺安营。
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 从比哈·希录对面起行,经过海中到了书珥旷野,又在伊坦的旷野走了三天的路程,就安营在玛拉。
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 从玛拉起行,来到以琳(以琳有十二股水泉,七十棵棕树),就在那里安营。
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 从以琳起行,安营在红海边。
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 从红海边起行,安营在汛的旷野。
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 从汛的旷野起行,安营在脱加。
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 从脱加起行,安营在亚录。
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 从亚录起行,安营在利非订;在那里,百姓没有水喝。
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 从利非订起行,安营在西奈的旷野。
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 从西奈的旷野起行,安营在基博罗·哈他瓦。
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 从基博罗·哈他瓦起行,安营在哈洗录。
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 从哈洗录起行,安营在利提玛。
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 从利提玛起行,安营在临门·帕烈。
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 从临门·帕烈起行,安营在立拿。
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 从立拿起行,安营在勒撒。
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 从勒撒起行,安营在基希拉他。
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 从基希拉他起行,安营在沙斐山。
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 从沙斐山起行,安营在哈拉大。
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 从哈拉大起行,安营在玛吉希录。
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 从玛吉希录起行,安营在他哈。
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 从他哈起行,安营在他拉。
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 从他拉起行,安营在密加。
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 从密加起行,安营在哈摩拿。
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 从哈摩拿起行,安营在摩西录。
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 从摩西录起行,安营在比尼·亚干。
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 从比尼·亚干起行,安营在曷·哈及甲。
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 从曷·哈及甲起行,安营在约巴他。
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 从约巴他起行,安营在阿博拿。
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 从阿博拿起行,安营在以旬·迦别。
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 从以旬·迦别起行,安营在寻的旷野,就是加低斯。
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 从加低斯起行,安营在何珥山,以东地的边界。
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 以色列人出了埃及地后四十年,五月初一日,祭司亚伦遵着耶和华的吩咐上何珥山,就死在那里。
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 亚伦死在何珥山的时候年一百二十三岁。
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 住在迦南南地的迦南人亚拉得王听说以色列人来了。
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 以色列人从何珥山起行,安营在撒摩拿。
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 从撒摩拿起行,安营在普嫩。
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 从普嫩起行,安营在阿伯。
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 从阿伯起行,安营在以耶·亚巴琳,摩押的边界。
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 从以耶·亚巴琳起行,安营在底本·迦得。
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 从底本·迦得起行,安营在亚门·低比拉太音。
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 从亚门·低比拉太音起行,安营在尼波对面的亚巴琳山里。
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 从亚巴琳山起行,安营在摩押平原—约旦河边、耶利哥对面。
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 他们在摩押平原沿约旦河边安营,从伯·耶施末直到亚伯·什亭。
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 耶和华在摩押平原—约旦河边、耶利哥对面晓谕摩西说:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 “你吩咐以色列人说:你们过约旦河进迦南地的时候,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 就要从你们面前赶出那里所有的居民,毁灭他们一切錾成的石像和他们一切铸成的偶像,又拆毁他们一切的邱坛。
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 你们要夺那地,住在其中,因我把那地赐给你们为业。
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 你们要按家室拈阄,承受那地;人多的,要把产业多分给他们;人少的,要把产业少分给他们。拈出何地给何人,就要归何人。你们要按宗族的支派承受。
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 倘若你们不赶出那地的居民,所容留的居民就必作你们眼中的刺,肋下的荆棘,也必在你们所住的地上扰害你们。
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 而且我素常有意怎样待他们,也必照样待你们。”
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< 民数记 33 >