< 约翰一书 5 >

1 凡信耶稣是基督的,都是从 神而生,凡爱生他之 神的,也必爱从 神生的。
Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ni Kristo, huyo ni mtoto wa Mungu; na, anayempenda mzazi humpenda pia mtoto wa huyo mzazi.
2 我们若爱 神,又遵守他的诫命,从此就知道我们爱 神的儿女。
Hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu: Kwa kumpenda Mungu na kuzitii amri zake;
3 我们遵守 神的诫命,这就是爱他了,并且他的诫命不是难守的。
maana kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake. Na, amri zake si ngumu,
4 因为凡从 神生的,就胜过世界;使我们胜了世界的,就是我们的信心。
maana kila aliye mtoto wa Mungu anaweza kuushinda ulimwengu. Hivi ndivyo tunavyoushinda ulimwengu: kwa imani yetu.
5 胜过世界的是谁呢?不是那信耶稣是 神儿子的吗?
Nani, basi, awezaye kuushinda ulimwengu? Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
6 这借着水和血而来的,就是耶稣基督;不是单用水,乃是用水又用血,
Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kifo chake. Hakuja kwa maji tu, bali kwa maji na kwa damu. Naye Roho anashuhudia kwamba ni kweli, kwani Roho ni ukweli.
7 并且有圣灵作见证,因为圣灵就是真理。
Basi, wako mashahidi watatu:
8 作见证的原来有三:就是圣灵、水,与血,这三样也都归于一。
Roho, maji na damu; na ushahidi wa hawa watatu waafikiana.
9 我们既领受人的见证, 神的见证更该领受了,因 神的见证是为他儿子作的。
Ikiwa twaukubali ushahidi wa binadamu, ushahidi wa Mungu una uzito zaidi; na huu ndio ushahidi alioutoa Mungu mwenyewe juu ya Mwanae.
10 信 神儿子的,就有这见证在他心里;不信 神的,就是将 神当作说谎的,因不信 神为他儿子作的见证。
Anayemwamini mwana wa Mungu anao ushahidi huo ndani yake; lakini asiyemwamini Mungu, anamfanya yeye kuwa mwongo, maana hakuamini ushahidi alioutoa Mungu juu ya Mwanae.
11 这见证就是 神赐给我们永生;这永生也是在他儿子里面。 (aiōnios g166)
Na, ushahidi wenyewe ndio huu: Mungu alitupatia uzima wa milele, na uzima huo uko kwa Bwana. (aiōnios g166)
12 人有了 神的儿子就有生命,没有 神的儿子就没有生命。
Yeyote, aliye na Mwana wa Mungu anao uzima huo; asiye na Mwana wa Mungu, hana uzima.
13 我将这些话写给你们信奉 神儿子之名的人,要叫你们知道自己有永生。 (aiōnios g166)
Nawaandikieni mpate kujua kwamba mnao uzima wa milele ninyi mnaoamini kwa jina la Mwana wa Mungu. (aiōnios g166)
14 我们若照他的旨意求什么,他就听我们,这是我们向他所存坦然无惧的心。
Na sisi tuko thabiti mbele ya Mungu kwani tuna hakika kwamba tukimwomba chochote kadiri ya mapenzi yake, yeye hutusikiliza.
15 既然知道他听我们一切所求的,就知道我们所求于他的,无不得着。
Yeye hutusikiliza kila tunapomwomba; na kwa vile tunajua kwamba yeye hutusikiliza kila tunapomwomba, twajua pia kwamba atupatia yote tunayomwomba.
16 人若看见弟兄犯了不至于死的罪,就当为他祈求, 神必将生命赐给他;有至于死的罪,我不说当为这罪祈求。
Mtu akimwona ndugu yake ametenda dhambi isiyompeleka kwenye kifo anapaswa kumwombea kwa Mungu, naye Mungu atampatia uzima. Nasema jambo hili kuhusu wale waliotenda dhambi ambazo si za kifo. Lakini ipo dhambi yenye kumpeleka mtu kwenye kifo nami sisemi kwamba mnapaswa kumwomba Mungu kwa ajili ya hiyo.
17 凡不义的事都是罪,也有不至于死的罪。
Kila tendo lisilo adilifu ni dhambi, lakini kuna dhambi isiyompeleka mtu kwenye kifo.
18 我们知道凡从 神生的,必不犯罪,从 神生的,必保守自己,那恶者也就无法害他。
Tunajua kwamba kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, kwa sababu Mwana wa Mungu humlinda salama, na yule Mwovu hawezi kumdhuru.
19 我们知道,我们是属 神的,全世界都卧在那恶者手下。
Tunajua kwamba sisi ni wake Mungu ingawa ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu.
20 我们也知道, 神的儿子已经来到,且将智慧赐给我们,使我们认识那位真实的,我们也在那位真实的里面,就是在他儿子耶稣基督里面。这是真神,也是永生。 (aiōnios g166)
Twajua pia kwamba Mwana wa Mungu amekuja, akatupa elimu ili tumjue Mungu wa kweli; tuishi katika muungano na Mungu wa kweli—katika muungano na Mwanae, Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na huu ndio uzima wa milele. (aiōnios g166)
21 小子们哪,你们要自守,远避偶像!
Watoto wangu, epukaneni na sanamu za miungu.

< 约翰一书 5 >