< 历代志上 16 >
1 众人将 神的约柜请进去,安放在大卫所搭的帐幕里,就在 神面前献燔祭和平安祭。
Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 大卫献完了燔祭和平安祭,就奉耶和华的名给民祝福,
Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
3 并且分给以色列人,无论男女,每人一个饼,一块肉,一个葡萄饼。
Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
4 大卫派几个利未人在耶和华的约柜前事奉,颂扬,称谢,赞美耶和华—以色列的 神:
Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
5 为首的是亚萨,其次是撒迦利雅、雅薛、示米拉末、耶歇、玛他提雅、以利押、比拿雅、俄别·以东、耶利,鼓瑟弹琴;惟有亚萨敲钹,大发响声;
Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
7 那日,大卫初次借亚萨和他的弟兄以诗歌称颂耶和华,说:
Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
8 你们要称谢耶和华,求告他的名, 在万民中传扬他的作为!
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10 要以他的圣名夸耀; 寻求耶和华的人,心中应当欢喜。
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12 他仆人以色列的后裔, 他所拣选雅各的子孙哪, 你们要记念他奇妙的作为和他的奇事, 并他口中的判语。
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 他是耶和华—我们的 神, 全地都有他的判断。
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15 你们要记念他的约,直到永远; 他所吩咐的话,直到千代,
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17 他又将这约向雅各定为律例, 向以色列定为永远的约,
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19 当时你们人丁有限,数目稀少, 并且在那地为寄居的;
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21 耶和华不容什么人欺负他们, 为他们的缘故责备君王,
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22 说:不可难为我受膏的人, 也不可恶待我的先知!
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24 在列邦中述说他的荣耀, 在万民中述说他的奇事。
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25 因耶和华为大,当受极大的赞美; 他在万神之上,当受敬畏。
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27 有尊荣和威严在他面前, 有能力和喜乐在他圣所。
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28 民中的万族啊, 你们要将荣耀能力归给耶和华,都归给耶和华!
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29 要将耶和华的名所当得的荣耀归给他, 拿供物来奉到他面前; 当以圣洁的妆饰敬拜耶和华。
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31 愿天欢喜,愿地快乐; 愿人在列邦中说: 耶和华作王了!
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32 愿海和其中所充满的澎湃; 愿田和其中所有的都欢乐。
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33 那时,林中的树木都要在耶和华面前欢呼, 因为他来要审判全地。
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
34 应当称谢耶和华; 因他本为善,他的慈爱永远长存!
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
35 要说:拯救我们的 神啊,求你救我们, 聚集我们,使我们脱离外邦, 我们好称赞你的圣名,以赞美你为夸胜。
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
36 耶和华—以色列的 神, 从亘古直到永远,是应当称颂的! 众民都说:“阿们!”并且赞美耶和华。
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
37 大卫派亚萨和他的弟兄在约柜前常常事奉耶和华,一日尽一日的职分;
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
38 又派俄别·以东和他的弟兄六十八人,与耶杜顿的儿子俄别·以东,并何萨作守门的;
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
39 且派祭司撒督和他弟兄众祭司在基遍的邱坛、耶和华的帐幕前燔祭坛上,每日早晚,照着耶和华律法书上所吩咐以色列人的,常给耶和华献燔祭。
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
41 与他们一同被派的有希幔、耶杜顿,和其余被选名字录在册上的,称谢耶和华,因他的慈爱永远长存。
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
42 希幔、耶杜顿同着他们吹号、敲钹,大发响声,并用别的乐器随着歌颂 神。耶杜顿的子孙作守门的。
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.