< 啟示錄 15 >

1 看見在天上又出現了一個又大又奇妙的異兆:有七位天使拿著七種最後的災禍,因為天主的義怒就要藉著這些災禍發洩淨盡。
Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
2 我又看見好像有個攙雜著火的玻璃海;那些戰勝了獸和獸像及牠名號數字的人,站在玻璃海上,拿著天主的琴,
Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
3 歌唱天主的僕人梅瑟的歌曲和羔羊的歌曲說:「上主,全能的天主!你的功行偉大奇妙;萬民的君王!你的道路公平正直;
Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
4 誰敢不敬畏你?上主!誰敢不光榮你的名號?因為只有你是聖善的;萬民都要前來崇拜你,因為你正義的判斷,已彰明較著。」
Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
5 這些事以後,我又看見天上盟約的帳幕--聖殿敞開了,
Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
6 那七位拿著七種災禍的天使,從聖殿那裏出來,身穿潔白而明亮的亞麻衣,胸間佩有金帶。
Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
7 那時,四個活物中的一個,給了那七位天使七個滿盛萬世萬代永生天主義怒的金盂。 (aiōn g165)
Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn g165)
8 因著天主的榮耀和威能,殿內充滿了煙,沒有一個人能進入殿內,直到那七位天使的七樣災禍降完為止。
Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.

< 啟示錄 15 >