< 詩篇 1 >
1 【善惡二路】凡不隨從惡人的計謀,不插足於罪人的道路,不參與譏諷者的席位,
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 專心愛好上主法律的,畫夜默思上主誡命的,這樣的人才是有福的!
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 他像植在溪畔的樹木,準時結果,枝葉不枯,所作所為,隨心所欲。
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 惡人卻不如此,絕不如此! 他們像被風吹散的糠秕。
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 在審判的時日,惡人站立不住;在義人的會中,罪人不能立足:
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.