< 詩篇 68 >
1 達味詩歌,交與樂官。 願天主興起,使他的仇敵四散,願仇恨他的人,由他面前逃竄!
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 願惡人在天主面前,滅亡消散,就像煙被風吹蠟被火化一般。
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 義人要在天主面前踴躍歡樂,我們也要在愉快中加倍喜悅。
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 為那乘車經過曠野者修平道路;祂的名叫雅威,應在他面前喜氣盈盈。
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 天主常在自己的聖所居住;天主是孤兒的慈父;天主是寡婦的保護,
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 天主給無靠的人備妥房屋,引領被擄的人重獲自由;叛逆者仍在乾旱居留。
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 天主,當您領導您的百姓出走,就在您踏入曠野的時候:
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 大地在天主面前震動,高天也滴下細雨,西乃在天主,以色列天主前也顫慄不休。
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 天主,您給您的產業降下甘霖,因而復蘇了疲倦的人民。
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 於是,您的羊群便在那裏安住,天主,以您的慈愛照顧了貧苦。
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 「領兵的君王已經逃走遠遁,家中的閨秀分得了戰利品。
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 正當您們在羊棧中尋夢,鴿子的翅翼塗上了白銀,翎毛閃爍著火紅的黃金,
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 當全能者驅逐列王的時間,飄飄的雪花落向匝耳孟山。
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 多峰的青山,您為何嫉視天主愛住的聖山?嫉視上主要永久居住的聖山?
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 您帶領俘虜升上高天,接受眾人作為貢品,不願住在上主天主前的人,也當貢品。
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 唯願上主受讚美!祂承擔了我們的重負,因祂是救助我們的天主。
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 我們的天主實在是拯救人的天主,上主天主使我們擺脫死亡的關口。
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 天主必要把他的頭顱擊穿,必要把固執於惡者的腦袋打爛。
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 我主說:「縱使他們逃至巴商,我也要把他們捉回來,縱使他們躲在海底,我也要把他們逮回來,
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 為使您在鮮血中洗滌您的腳,您的狗以舌頭舔食敵人的血。
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 天主,人都看見您的御輦,看見我主我王,光臨聖殿:
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 歌詠的人在前,奏樂的人在後,在中間還有一隊鳴鼓的少女。
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 您們應在盛會中讚美天主,以色列的子孫應讚美上主。
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 最幼小的本雅明領導在前,隨後有猶大的首領和隨員,則步隆和納斐塔里的長官。天主,求您顯示出您的威能,天主,顯出為我們行的大能。
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 為了您在耶路撒冷的聖殿,眾君王必要向您奉上祭獻,
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 懇求您怒叱蘆葦中的野獸,成群的公牛和列國的牛犢;願他們帶著銀塊前來降服,願您驅散喜愛戰爭的民族!
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 他自永遠就是駕御高天穹蒼的大主,聽!他的聲音發出,巨大的聲音已發出。
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 您們應承認天主的大能!他的榮耀光照以色列人,他的神威已發現在天雲。
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 天主,以色列的天主,在聖所中顯得可敬可畏,他曾將力量和權能賜於百姓。 願天主永受讚美!
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!