< 詩篇 58 >
1 達味金詩,交與樂官。調寄「莫要毀壞」。 判官們!你們是否真正出言公平?世人們!你們是否照理審斷案情?
Je, ninyi watawala mnaongea haki? Mnahukumu kwa haki, ninyi watu?
2 可惜你們一心只想為非作惡,在地上你們的雙手只行宰割。
Hapana, mnafanya uovu mioyoni mwenu; munaeneza vurugu nchi yote kwa mikono yenu.
3 作惡者一離母胎,即背離正路;說謊者一出母腹,即走入歧途。
Waovu huenenda katika upotovu hata walipokuwa tumboni; wao wanaenenda katika upotovu tangu kuzaliwa, wakiongea uongo.
4 他們滿懷的毒素有如蛇毒;他們又像塞住耳朵的聾蝮,
Sumu yao ni kama sumu ya nyoka; wako kama fira kiziwi azibaye masikio yake,
ambaye hasikilizi sauti ya waganga, haijalishi ustadi walio nao.
6 天主,求你把他們口中的牙齒搗爛,上主,求你把少壯獅子的牙床打斷。
Vunja meno yao midomoni mwao, Mungu; uyatoe meno ya mwana simba, Yahwe.
7 他們有如奔湍的急水流去,他們有如被踏的青草枯萎;
Wayeyuke kama maporomoko ya maji; wafyatuapo mishale yao, iwe kama haina ncha.
8 他們有如蝸牛爬過溶化消失,又如流產的胎兒不得親見天日!
Wawe kama konokono ambaye huyeyuka na kutoweka, kama mtoto aliye zaliwa kabla ya wakati ambaye hakuona jua.
9 他們的鍋在未覺到荊火以前,願狂怒的烈風將他們全部吹散!
Kabla ya vyungu vyenu kupata joto la kuungua kwa miiba, yeye ataviondosha kwa upepo mkali, miiba ya kijani yote na ile inayoungua.
10 義人看見大仇己報時,必然喜樂,他要在惡人的血中洗自己的腳。
Mwenye haki atafurahia atakapoona kisasi cha Mungu; ataiosha miguu yake kwenye damu ya waovu,
11 如此,眾人都說:「義人果然獲得了好的報酬,世上確有執行審判的天主!
hivyo watu watasema, “Hakika kuna tuzo kwa ajili ya mtu wenye haki; hakika kuna Mungu ahukumuye ulimwengu.”