< 詩篇 55 >

1 達味訓誨歌,交與槳官。 天主,求你側耳傾聽我的祈禱,求你不要迴避我的哀告。
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, sikiliza maombi yangu, wala usidharau hoja yangu.
2 求你俯視我,並垂允我,我痛苦憂傷,嘆息悲號:
Nisikie na unijibu. Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
3 由於仇敵的叫囂,並因惡人的吵鬧,因加於我的災禍,怒中給我的騷擾,
kwa sauti ya adui, kwa kukaziwa macho na waovu, kwa sababu wananiletea mateso juu yangu na kunitukana kwa hasira zao.
4 我的心在我胸內焦灼,死亡的恐怖籠罩了我,
Moyo wangu umejaa uchungu, hofu ya kifo imenishambulia.
5 驚懼與戰慄侵襲了我,恐怖與煩惱淹沒了我。
Woga na kutetemeka vimenizunguka, hofu kuu imenigharikisha.
6 我於是說:但願我有鴿子般的翅膀,為能飛翔而去,棲身安藏!
Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa! Ningeruka niende mbali kupumzika.
7 看,我必要逃往遠處,在荒涼的地方暫住;
Ningalitorokea mbali sana na kukaa jangwani,
8 從速尋找一個避難所,避過這一場風狂雨暴。
ningaliharakisha kwenda mahali pa salama, mbali na tufani kali na dhoruba.”
9 我主,求你分散擾亂他們的語言,因我在城中只見到鬥爭與紛亂:
Ee Bwana, uwatahayarishe waovu na uwachanganyishie semi zao, maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.
10 他們日夜在城牆上巡行,邪惡與欺壓在城中叢生。
Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake, uovu na dhuluma vimo ndani yake.
11 城池中已滿布詭計,霸道欺詐橫行街市。
Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini, vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.
12 若是我的仇人辱罵我,我還可容忍;若是惱恨我者欺凌我,我尚可退隱;
Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione.
13 可惜是你,我的同僚,我的伙伴,我的友好;
Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu,
14 我們曾經推心置腹,無所諱言,在人群中走進了天主的聖殿。
ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri, tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.
15 願死亡突襲他們,活活的墜入陰府!因為他們的居處和內心滿是惡毒。 (Sheol h7585)
Kifo na kiwajie adui zangu ghafula, na washuke kuzimu wangali hai, kwa maana uovu upo ndani yao. (Sheol h7585)
16 但我卻要呼號天主,上主必定予我救助。
Lakini ninamwita Mungu, naye Bwana huniokoa.
17 不論在黃昏在清晨或在中午,我哀聲悲嘆,祂必聽我的苦訴。
Jioni, asubuhi na adhuhuri ninalia kwa huzuni, naye husikia sauti yangu.
18 祂必從迫害我的人中,救我然脫險,因為那些反對我的人,實在眾多難算。
Huniokoa nikawa salama katika vita vilivyopangwa dhidi yangu, ingawa watu wengi hunipinga.
19 永遠為王的天主必要俯聽我,而把他們趕走,因為他們不知回心轉意,又不知敬愛天主。
Mungu anayemiliki milele, atawasikia na kuwaadhibu, watu ambao hawabadilishi njia zao, wala hawana hofu ya Mungu.
20 他們伸手攻擊自己的友好,他們任意訂立違背的盟約。
Mwenzangu hushambulia rafiki zake, naye huvunja agano lake.
21 他們的容貌比奶油更光滑,心卻是好戰;他們的言語比脂粉還柔和,但口蜜腹劍。
Mazungumzo yake ni laini kama siagi, hata hivyo vita vimo moyoni mwake. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
22 將你的重擔卸交上主,祂必扶持你,祂決對不會讓義人永遠動搖不止。
Mtwike Bwana fadhaa zako, naye atakutegemeza, hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.
23 天主,求你使他們墮入滅亡的深穴!兇手和奸詐的歹徒必定中年夭折。上主,但我卻要時常一心唯你是賴。
Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha waovu katika shimo la uharibifu. Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila, hawataishi nusu ya siku zao. Lakini mimi ninakutumaini wewe.

< 詩篇 55 >