< 詩篇 21 >

1 【頌賜勝利的天主】 達味詩歌,交與樂官。 上主,君王因你的威能而欣喜,因你的救助狂歡而快樂無比。
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, mfalme huzifurahia nguvu zako. Tazama jinsi ilivyo kuu furaha yake kwa ushindi unaompa!
2 你滿全了他心中的渴想,沒有拒絕他口中的盼望。
Umempa haja ya moyo wake na hukumzuilia maombi ya midomo yake.
3 因為你已賜給了他卓越的福寵,以純金的冠冕加在他的頭頂;
Ulimkaribisha kwa baraka tele na kumvika taji ya dhahabu safi kichwani pake.
4 他雖只向你乞求確保性命,你卻賜給他萬世無疆的長生。
Alikuomba maisha, nawe ukampa, wingi wa siku milele na milele.
5 你協助他獲得偉大的光榮,你加給他無比的榮耀與尊崇;
Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa, umeweka juu yake fahari na utukufu.
6 你使他成為萬世的福源,使他在你面前踴躍喜歡。
Hakika umempa baraka za milele, umemfanya awe na furaha kwa shangwe ya uwepo wako.
7 君王既已全心對上主信賴,憑至高者的慈愛不再移改。
Kwa kuwa mfalme anamtumaini Bwana; kwa upendo usiokoma wa Aliye Juu Sana hatatikiswa.
8 願你的手將你的一切仇敵搜羅,願你的右手將憎恨你的人捕捉!
Mkono wako utawashika adui zako wote, mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.
9 當你顥示你尊容的時候,處置他們有如放在火爐;願上主以震怒消滅他們,讓火焰也盡情吞滅他們!
Wakati utakapojitokeza utawafanya kama tanuru ya moto. Katika ghadhabu yake Bwana atawameza, moto wake utawateketeza.
10 願你從地上滅盡他們的子女,使他們的後裔全絕跡於人世!
Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani, uzao wao kutoka wanadamu.
11 他們雖為陷害你而設計,策畫的陰謀卻無濟於事;
Ingawa watapanga mabaya dhidi yako na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,
12 因為你朝他們張弓搭箭,已使他們嚇得轉身逃竄。
kwa kuwa utawafanya wakimbie utakapowalenga usoni pao kwa mshale kutoka kwenye upinde wako.
13 上主,請起來,顯示你的英勇,讓我們歌頌稱揚你的威能。
Ee Bwana, utukuzwe katika nguvu zako, tutaimba na kusifu nguvu zako.

< 詩篇 21 >