< 詩篇 149 >

1 亞肋路亞!請您們向上主謳唱新歌,在聖者集會中向他祝賀!
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2 願以色列因自己的創造者而踴躍,願熙雍子民因自己的君王而歡樂!
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3 願他們以舞蹈讚美上主的名,願他們敲鼓彈琴向上主歌詠!
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 因為上主喜愛自己的百姓,賞賜謙虛的人凱旋而得勝。
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 願聖徒因所受的光榮而喜慶,在自己的床榻上歡呼而歌頌。
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6 願讚美天主的歌辭在他們的口中,願雙刃的寶劍掌握在他們的手中,
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 為向異邦報仇雪恥,為向列國進攻襲擊,
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8 要用鎖鍊捆住他們的國君,要用銬鐐鎖住他們的縉紳,
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 為向他們施行經上的審訊。這也就是一切聖徒的光榮。
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.

< 詩篇 149 >