< 詩篇 145 >
1 我的天主,君王,我要頌揚您,歌頌您的名,世世代代不停止。
Wimbo wa Sifa. Wa Daudi. Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme, nitalisifu jina lako milele na milele.
Kila siku nitakusifu na kulitukuza jina lako milele na milele.
3 偉大的上主,實在應受讚美,上主的偉大,高深不可推測;
Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, ukuu wake haupimiki.
4 世世代代應宣揚上主的工程,世世代代應傳述上主的大能:
Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine, watasimulia matendo yako makuu.
Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako, nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.
Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha, nami nitatangaza matendo yako makuu.
Wataadhimisha wema wako mwingi, na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.
8 主慈悲為懷,寬宏大方;他常緩於發怒,仁愛無量。
Bwana ni mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.
9 上主對待萬有,溫和善良,對他的受造物,仁愛慈祥。
Bwana ni mwema kwa wote, ana huruma kwa vyote alivyovifanya.
10 上主,願您的一切受造物稱謝您,上主,願您的一切聖徒們讚美您,
Ee Bwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu, watakatifu wako watakutukuza.
Watasimulia utukufu wa ufalme wako na kusema juu ya ukuu wako,
ili watu wote wajue matendo yako makuu na utukufu wa fahari ya ufalme wako.
13 您的王國,是萬代的王國,您的王權,存留於無窮世;上主對自己的一切諾言,忠信不欺,上主對自己的一切受造,勝善無比。
Ufalme wako ni ufalme wa milele, mamlaka yako hudumu vizazi vyote. Bwana ni mwaminifu kwa ahadi zake zote na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
14 凡跌倒的,上主必要扶持,凡被壓抑的,使他們起立。
Bwana huwategemeza wote waangukao, na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.
Macho yao wote yanakutazama wewe, nawe huwapa chakula chao wakati wake.
Waufumbua mkono wako, watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.
17 上主在他的一切路徑上,至公至義;上主在他的一切化工上,聖善無比。
Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
18 上主接近一切呼求祂的人,就是一切誠心呼求祂的人。
Bwana yu karibu na wote wamwitao, karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.
19 他必成全敬愛自己者的心願,聽到他們的呼號,必施以救援。
Huwatimizia wamchao matakwa yao, husikia kilio chao na kuwaokoa.
20 凡愛慕上主的,上主必保護他們;凡作惡犯罪的,上主必消除他們。
Bwana huwalinda wote wampendao, bali waovu wote atawaangamiza.
21 願我的口舌稱述上主的光榮,願眾生讚美他的聖名於無窮!
Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana. Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu milele na milele.