< 詩篇 126 >

1 上主帶領俘虜回到熙雍,我們覺得仿佛是在夢中;
Wimbo wa kwenda juu. Bwana alipowarejeza mateka Sayuni, tulikuwa kama watu walioota ndoto.
2 那時我們滿口喜氣盈盈,我們雙脣其樂融融。那時外邦異民讚歎不已:上主向他們行了何等奇事!
Vinywa vyetu vilijaa kicheko, ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe. Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa, “Bwana amewatendea mambo makuu.”
3 上主向我們行偉大奇蹟,我們的確覺得滿心歡喜。
Bwana ametutendea mambo makuu, nasi tumejaa furaha.
4 上主,求您轉變我們的命運!就像乃革布有流水的澆淋。
Ee Bwana, turejeshee watu wetu waliotekwa, kama vijito katika Negebu.
5 含淚播種的人,必含笑的收成;
Wapandao kwa machozi watavuna kwa nyimbo za shangwe.
6 他們邊行邊哭,出去播種耕耘,他們載欣載奔,回來背著禾捆。
Yeye azichukuaye mbegu zake kwenda kupanda, huku akilia, atarudi kwa nyimbo za shangwe, akichukua miganda ya mavuno yake.

< 詩篇 126 >